name
stringclasses 429
values | text
stringlengths 0
767k
⌀ |
|---|---|
Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba amesisitiza umuhimu wa kufanyika mambo matano kuelekea uchaguzi
|
Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba amesisitiza umuhimu wa kufanyika mambo matano kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa, akiyataja kuwa nyenzo ya kuongeza ushiriki wa wananchi na imani yao kwa uchaguzi huo.
Miongoni mwa mambo hayo ni wananchi kuhakikishiwa dosari zilizotokea mwaka 2019 hazitokei tena, kupewa uhuru wa kuwachagua viongozi wanaowataka na meza ya mazungumzo kati ya Serikali na vyama vya siasa juu ya mambo yanayolalamikiwa.
Warioba anaibuka na mambo hayo, ikiwa umesalia mwezi mmoja na siku chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi huo, Novemba 27, mwaka huu.
Jaji Warioba alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana, alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa.
Mazungumzo
Katika mkutano wake huo, kiongozi huyo aliyewahi kuiongoza tume ya mabadiliko ya katiba mwaka 2014, alisema Serikali inapaswa kufanya jitihada za kukutana na vyama vya siasa kukubaliana namna nzuri ya kuuendea uchaguzi huo.
Umuhimu wa kufanyika hilo, unatokana na kile aliochofafanua, Serikali imefanya maandalizi lakini wakati wote vyama vya siasa havionyeshi kuamini kwamba uchaguzi wa mwaka huu utakuwa tofauti na zilizopita.
“Ni juu ya Serikali kufanya hatua za kuwahakikishia wananchi kwamba yaliyotokea hayatatokea. Serikali iandae mipango kuvikaribisha vyama vya siasa kuwaeleza kwamba hakitafanyika hivi na vile,” alisema.
Alikifananisha kinachoendelea sasa na mapambano, akisema kila upande kati ya Serikali na vyama vya siasa unazungumza lake, ilhali kulipaswa kuwa na mazungumzo ya pamoja.
“Inaonekana ni mapambano tu vyama vya upinzani vinasema tunaweza kuchukua hatua hizi wakati Serikali inasema tutalinda amani Polisi wapo,” alisema.
Pamoja na elimu ya mpigakura inayotolewa, alitaka wananchi wahakikishiwe kuwa wanakwenda kupiga kura ya wazi, huru na kuwachagua wale wanaowataka.
Hakikisho kwa wananchi
Kuelekea uchaguzi huo, Warioba alisema ni muhimu kuwahakikishia wananchi kuwa, dosari zilizoshuhudiwa katika uchaguzi kama huo mwaka 2019, hazijitokezi tena.
Dosari zinazozungumziwa na Warioba katika uchaguzi huo wa mwaka 2019, zinahusisha kuenguliwa kwa wagombea wa vyama vya upinzani, mawakala kuondolewa, jambo lililosababisha wagombea wengi wa chama tawala CCM kupita bila kupingwa.
“Tuepushe kabisa yale yaliyotokea huko nyuma na hili ni jukumu kubwa kwa Serikali kwa sababu ndiyo inayosimamia uchaguzi, hatua zichukuliwe kwa yaliyotokea nyuma ili kuwahakikishia wananchi kwamba mambo yako sawa,” alisema.
Umuhimu wa hakikisho hilo ni kile alichofafanua, aliyesimama uchaguzi wa mwaka 2019 ndiye anayesimamia huu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu, hivyo bado watu wana wasiwasi kwamba atarudia yale au atafanya tofauti.
Uhuru kuchagua wanaowataka
Jaji Warioba alisema pamoja na kutolewa kwa elimu inayowapa uhuru wananchi kuwachagua viongozi wanaowataka la msingi ni maandalizi ya kuhakikisha raia wanawachagua viongozi kulingana na matakwa yao.
“Ukifika uchaguzi wananchi wana uhuru huo wa kusema sisi tunayemtaka ni huyu, au wanaletewa watu wa kuwachagua? Hili ni tatizo lingine lililopo,” alisema.
Aliijenga hoja hiyo akitolea mfano juhudi za zamani kuhakikisha wananchi wanawachagua viongozi wanaowataka, akisema kulikuwa na utaratibu wa kujua kuwa anayegombea anakubalika.
Kama ilivyokuwa wakati huo, alisema vyama vya siasa viwe na utaratibu unaozingatia kama wanaoteuliwa wanakubalika katika maeneo husika kinyume na hivyo watapatikana viongozi wasiostahili.
Mazingira hayo, alisema ndiyo yanayosababisha uongozi ngazi ya chini ukose nguvu, kiasi cha kila mwananchi anaona bora awasilishe lalamiko lake kwa ngazi ya taifa.
“Siku hizi kwa sababu ya haya yanayotokea unaona kama nguvu iliyokuwepo kule chini imepungua sana, wananchi hawatazami viongozi wao waliopo kule chini wanatazama juu. Ukiwauliza wananchi wanasema wanaomba Rais awatazame kutatua tatizo fulani,” alisema.
Demokrasia
Kwa mujibu wa Warioba, wengi wanaozungumzia demokrasia wamejikita katika madaraka, badala ya utawala bora ambao ndiyo msingi sahihi.
Alieleza hilo linaonyesha watu wanafikiria zaidi kuhusu madaraka, kwa kuwa demokrasia wanayoielezea inahusu tume ya uchaguzi, uchaguzi wa rais kupingwa mahakamani na ushindi wa kura za rais uwe kwa zaidi ya asilimia 50.
Akiijenga hoja hiyo aligusia suala la uchaguzi huo kusimamiwa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mi9koa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), akisema kilichobaki ni mazungumzo ya kukubaliana namna ya uchaguzi huu kufanyika kama ulivyopaswa kufanywa iwapo ungesimamiwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC).
Amani
Kuhusu amani, Warioba alisema polisi sio chombo cha kulinda amani, isipokuwa amani inalindwa na wananchi wenyewe.
“Amani haikuletwa na mtutu wa bunduki wala umoja, ni makubaliano ya wananchi kwamba tunapaswa kuwa na amani kwa mtindo huu,” alisema.
Katika mazingira hayo, alisema ni vigumu kulinda amani kwa kutumia bunduki na kuwafanya wananchi waamini.
“Kulinda amani yetu, umoja wetu, tusirudishe ukabila udini na sasa hivi ukanda unaanza kupata nguvu, nasema hivi kama tukivikataa tutaweza kulinda umoja wetu na amani yetu,” alisema.
Hata hivyo, alitumia jukwaa hilo, kueleza angalau kwa kiwango fulani Tanzania imefikia kiwango kizuri cha maridhiano, ukilinganisha na miaka mitatu iliyopita.
“Katika kipindi hicho, hali ya siasa haikuwa nzuri. Rais Samia Suluhu Hassan alirithi matatizo mengi tu, mikutano ya siasa ilizuiwa, maandamano yalizuiwa,” alisema.
Alieleza kwa sasa nchi inaongozwa katika namna ambayo matatizo mengi yaliyokuwepo yameondolewa, akisisitiza ni kweli maridhiano hayajafikiwa kwa kiasi kikubwa, lakini msingi bado upo.
|
Mwanahabari wa kujitegemea, Erick Kabendera ametangaza uamuzi wa kukata rufaa dhidi ya pingamizi lil
|
Mwanahabari wa kujitegemea, Erick Kabendera ametangaza uamuzi wa kukata rufaa dhidi ya pingamizi lililozuia kuendelea kwa kesi yake anayokabiliana na Kampuni ya mtandao wa simu ya Vodacom Tanzania Ltd.
Kabendera aliifungua kesi hiyo, Julai mwaka huu, akiituhumu kampuni hiyo kuhusika na utoaji wa taarifa za mahali alipo hadi kukamatwa kwake Julai, mwaka 2019 nyumbani kwake Mbweni, jijini Dar es Salaam.
Baada ya kufungua kesi hiyo namba (12799/2024), iliwekewa pingamizi lililosababisha Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam kuifuta.
Kabendera alitangaza uamuzi wa kukata rufaa juzi, alipozungumza na waandishi wa habari kwa njia ya mtandao, akidokeza anafanya hivyo baada ya kushauriana na mawakili wake.
Alisema anatarajia kukata rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa dhidi za pingamizi lililowekwa kwa kuwa wanaamini kesi hiyo ina mashiko na inastahili kusikilizwa ili wawasilishe ushahidi.
“Kutokana na ushahidi tulioukusanya baada ya miaka mitatu ya uchunguzi, tumeona kuwa ushahidi ni mkubwa kiasi kwamba unatosha kuishitaki Vodacom Tanzania na kampuni zake tanzu nchini Afrika ya Kusini na Uingereza,” alisema.
Sambamba na uamuzi huo, Kabendera alisema wanasheria wake kutoka Uingereza na Afrika ya Kusini wanakamilisha utaratibu wa kufungua kesi dhidi ya Vodacom Group South Africa na Vodafone Group PLC yenye makao yake makuu nchini Uingereza haraka iwezekanavyo.
Kwanini anaituhumu Vodacom
Katika maelekezo yake kwa wanahabari, Kabendera alisema kabla ya kukamatwa simu yake yenye laini ya mtandao wa kampuni hiyo ilizimwa na kila alipofanya juhudi za kuwasiliana na huduma kwa wateja alitakiwa kwenda makao makuu.
Katika juhudi hizo, alieleza ulifika wakati laini hiyo ilifunguliwa, lakini wahudumu kwa mteja walikuwa wakimpigia mara kwa mara kumuuliza alipo na zilisikika sauti za watu wakipanga kuizungumza nyumba yake.
“Muda mfupi baadae, nilipigiwa simu kutoka kwenye namba ya Vodacom Huduma kwa Wateja na sauti ya kiume ilijitambulisha kama mhudumu kutoka Huduma kwa Wateja. Alinitaka nijitambulishe na kumwambia eneo nilipokuwa.
Nikapata wasiwasi na kujizuia kusema jambo lolote. Hata, kunilikuwa na muungurumo mkubwa sana kwenye laini na muungurumo huo uliniumiza masikio. Nilisikia pia kikundi cha watu wakibishana kwenye laini na kusema kuwa nilikuwa nyumbani kwangu na kwamba wasogee na kuzunguka nyumba yangu,” alisema.
Alieleza baada ya kauli hiyo alishtuka na kuchungulia nje, ndipo alipogundua nyumba yake imezingirwa na watu waliovaa nguo za kiraia, wakiwa na silaha na magari kadhaa.
“Niliwapigia simu majirani na vijana kadhaa wanaofanya shughuli za kuendesha pikipiki ili wafike nyumbani. Baadhi ya watu waliofika nyumbani kwangu na kuanza kuchukua video za tukio zima walitishiwa na simu zao kuchukuliwa. Baadhi yao walifanikiwa kusambaza video kwa watu mbalimbali,” alisema.
Alisema kwa kuwa kulikuwepo na kundi kubwa nje ya nyumba na kampuni ya ulinzi iliyokuwa inalinda nyumba hiyo ilishatuma wawakilishi wake, aliamua kutoka nje.
“Watu waliovaa kiraia wakiwa na mitutu walinifunga pingu na kuniweka kwenye gari. Kutokana na taarifa za kutekwa kwangu kusambaa kwa kasi, walianza kupata wasiwasi na kuamua kunihimishia kwenye gari lingine baada ya kutembea kwa takribani kilomita tano kutoka nyumbani kwangu kwa kuhofia kuwa watu wangelitambua gari hilo ambalo lilikuwa limepigwa picha,” alieleza.
Kutokana na maelezo hayo, alisema kwa mtazamo wake kuwa kampuni ya Vodacom ilihusika moja kwa moja katika kufanikisha kutekwa kwake.
“Bila watumiaji wa mitandao ya kijamii, yombo vya habari kusambaza taarifa kwa kasi, ni wazi kwamba ningeweza kupotezwa na pengine kuuwawa,” alisema.
Hata hivyo, alisema kilichofanya achelewe kufungua kesi tangu alipotoka mahabusu ni ugonjwa uliomsumbua na juhudi za kutafuta fedha alizopaswa kulipa ili awe huru.
“Kutokana na hali hiyo kipaumbele hakikuwa kufungua kesi mahakamani bali kupata matibabu ya uhakika,” alisema.
|
Kama mara yako ya mwisho kufika Dar es Salaam ni miaka 10 iliyopita, pengine unahitaji mwenyeji wa k
|
Kama mara yako ya mwisho kufika Dar es Salaam ni miaka 10 iliyopita, pengine unahitaji mwenyeji wa kukupokea na kukuelekeza maeneo mbalimbali ya jiji hili.
Hilo linatokana na ukweli kwamba, karibu kila kitu kimebadilika kuanzia barabara, majengo marefu kwa mafupi na hata kuwapo kwa miji mipya kumeibadili Dar es Salaam kwa kiwango kikubwa.
Baadhi ya maeneo yaliyoonekana ya kawaida zamani sasa ni kivutio kiasi cha watu kuyatumia kupiga picha wakiambatanisha na maelezo kuwa, hii ni Tanzania si nchi za nje.
Ujumbe huo ni tafsiri inayobeba uhalisia wa mfanano wa baadhi ya maeneo ya Jiji hilo na miji mingine ya mataifa ya nje, ambayo aghalabu ilitumika kama mfano kwa uzuri.
Eneo la Barabara ya Bagamoyo kuanzia Sayansi hadi Morocco katika Wilaya ya Kinondoni ni kielelezo cha maeneo yaliyopitia mabadiliko ya mandhari kiasi cha kushangaza.
Mvuto wa eneo hilo, umetokana na nyumba za ghorofa, zilizopangwa zikapangika, nakshi za aina yake na barabara iliyonyooka, hakika Dar es Salaam ya leo sio ya jana.
Kama unastaajabu mwonekano wa mchana, utakachokiona usiku kitakushangaza, ni mvuto unaoambatana na mwangaza wa taa zenye mitindo mbalimbali katika kuta na baraza za maghorofa.
Badala ya Posta iliyozoeleka kama makao makuu ya ofisi mbalimbali, kwa sasa eneo hili ndiko yaliko makao makuu ya kampuni kadhaa za simu, ikiwemo Tigo, Halotel na Vodacom.
Migahawa yenye hadhi ya kipato cha kati na juu, ndizo ofisi nyingine zinazopatikana katika eneo hilo, ni tafsiri halisi ya mabadiliko ya Jiji.
Mabadiliko ya Dar es Salaam hayahusishi majengo peke yake, mawasiliano ya barabara za zege na lami katika mitaa mbalimbali ni jambo lingine litakalokupoteza kama hujakanyaga jiji hili kwa miaka kadhaa.
Kama hiyo haitoshi, madaraja na barabara za juu sio Afrika Kusini na Kenya pekee, hadi Dar es Salaam zinapatikana kwa sasa, lipo lile la Kijazi Interchange lililopo Ubungo, Daraja la juu la Mfugale, Daraja la Juu Kurasini na Uhasibu.
Unapoingia Dar es Salaam kwa njia ya Morogoro, unakaribishwa na makutano ya barabara ya Kijazi (Kijazi Interchange), lile eneo lililokuwa kitovu cha msongamano wa magari, sasa ni kuteleza tu.
Achilia mbali kuleta mandhari murua, ujenzi wa barabara hizo uliofanyika kwa vipindi tofauti, umesaidia kupunguza msongamano wa magari, hivyo kurahisisha maisha ya wananchi.
Ujenzi wa barabara za lami katika mitaa mbalimbali ulioambatanishwa na uwekwaji taa za barabarani ni moja ya vitu vilivyolifanya jiji hili libadilike.
Madaraja ya juu
Daraja la Mfugale ndiyo lililokuwa la kwanza kujengwa na kisha kuzinduliwa Septemba 28, 2018.
Ujenzi wa daraja hilo ulilenga kuondoa foleni kwa watumiaji wa barabara wanaotoka katikati ya jiji kwenda Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na wale wanaotoka Ubungo kwenda bandarini na Mbagala.
Siku ambayo daraja hilo linazinduliwa ndipo ujenzi wa daraja la juu la Chang’ombe ulitangazwa lengo ikiwa ni kuendelea kuboresha na kuondoa foleni baada ya awali kubainika kuwa tatizo hilo lilipotatuliwa Tazara shida ilihamia Chang'ombe.
Hata hivyo, changamoto imeendelea kubaki katika eneo la kutoka Buguruni kuvuka eneo hilo kwenda Temeke na Kurasini kwani bado foleni imeendelea kuwa kubwa katika baadhi ya siku na saa.
Mbali na ujenzi huo, pia mkakati wa kumaliza foleni katika jiji ulihamia katika mradi wa makutano ya barabara ya Ubungo maarufu Kijazi interchange na baadaye Kurasini.
Jitihada hizo zilienda mbali zaidi na sasa watu wanaotoka Posta kwenda Masaki hawalazimiki kupita Daraja la Selander na badala yake kuna Daraja jipya la Tanzanite.
Mbali na kupunguza msonganani pia limekuwa ni kivutio kipya cha utalii kutokana na jinsi lilivyojengwa likichuana kwa ubora na uzuri na lile la Julius Nyerere linalounganisha Kurasini na Kigamboni ambalo pia limekatisha baharini.
Haya yote yaliyofanyika yamebadilisha mandhari ya jiji la Dar es Salaam na kulifanya kuwa jipya.
Barabara za mitaa
Mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP) nao umechangia kwa kiasi kikubwa kulifanya jiji hilo kuwa na mwonekano wa kuvutia.
Chini ya mradi huo, barabara za lami zimejengwa katika maeneo tofauti ambayo awali isingekuwa rahisi kupitika. Kwa sasa yamewekwa na taa na kuongeza mvuto na urahisi wa usafiri kwa wananchi.
Eneo kama Mtoni Kijichi, Mbagala Kuu ambalo linatajwa kuteuliwa kuwa la mfano, ni sehemu ambayo uwekaji wa barabara za lami umebadilisha asilimia 90 ya mwonekano wake na kwa kiasi kikubwa, hata aina ya maisha.
Miundombinu hiyo imeongeza sifa ya eneo hilo na mtazamo wa watu juu ya wenzao wanaoishi umebadilika na sasa wanaonekana kuwa ni wenye maisha bora tofauti na awali.
Uboreshaji huo ulikwenda sambamba na ujenzi wa daraja linalounganisha Vikunai na Kigamboni ambalo pia linatumika kama njia ya haraka kwa wale wanaotoka Mbagala kwenda maeneo ya karibu ikiwamo Toangoma.
Magomeni Kota
Sina shaka kama uliwahi kuishi Dar es Salaam, unakumbuka taswira ya Magomeni inayounganisha Mwembechai na Usalama, eneo lililokuwa na nyumba za watumishi wa umma wa enzi hizo Magomeni Kota.
Ninaposema watumishi wa umma wa enzi hizo na nyumba hizo ziliakisi enzi haswa, maana ni mithiri ya mabanda yanayotumika kama kambi za siku kadhaa na wakati wowote ungedhani zinaanguka.
Mambo hayako hivyo tena kwa sasa, eneo hilo limetapakaa nyumba zenye ngorofa sita na ndani yake kuna kila huduma kwa ajili ya kukidhi haja ya kaya 644.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Daud Kondoro anakaririwa akisema kuwa mradi huo wa nyumba za ghorofa una uwezo wa kuchukua kaya 644.
Kadhalika anasema kuna eneo la uwekezaji la Machinga Center ambalo lina vizimba 286, vyoo vya kulipia na uwekezaji wa sakafu juu na chini.
Barabara za mwendokasi
Ujenzi wa barabara za mabasi yaendayo haraka ni jambo lingine lililobadili sura ya jiji la Dar es Salaam. Huduma hiyo imekuwa kivutio sio kwa watu wa ndani pekee, bali hata mataifa mengine ya Afrika yamefika nchini kuona namna huduma hiyo inavyoendeshwa.
Baada ya kukamilika katika eneo hilo na kutoa huduma kwa miaka kadhaa, mradi huo umeanza kutanuka na hivi karibuni, wakazi wa Mbagala na maeneo ya jirani wataanza kunufaika.
Kwa mujibu wa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, awamu ya pili ya ujenzi wa barabara za mabasi yaendayo haraka kutoka Gerezani hadi Mbagala Rangi tatu, utakamilika mwezi ujao.
Mradi huo unahusisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 20.3, vituo 27, barabara za juu tatu na njia za maji za chini zenye urefu wa kilomita 40.
Mradi huo hauishii hapo, Profesa Mbarawa alisema hayo wakati akikagua ujenzi wa awamu ya tatu ya barabara ya kiwango cha zege ya mabasi yaendayo haraka kutoka Posta ya zamani hadi Gongo la Mboto yenye urefu wa kilomita 23.3 utakaogharimu Sh231 bilioni unaotarajiwa kukamilika Aprili mwakani.
Barabara za njia nane, nne
Moja ya vitu vilivyobadili mandhari ya Dar es Salam ni ujenzi wa barabara za njia nane wenye urefu wa kilomita 19.2 kuanzia Kimara hadi Kibaha.
Kati ya njia hizo, tatu zinatumiwa na magari yanayoelekea mikoani na tatu yanayoingia Jiji la Dar es Salaam na mbili za katikati ni mahsusi kwa ajili ya mabasi yaendayo haraka.
Miundombinu hiyo iliyogharimu zaidi ya Sh161 bilioni imefanya maisha ya wakazi wa Kibaha wanaofanya shughuli zao jiji la Dar es Salaam kuwa rahisi kwani foleni ambayo ilikuwa mwiba hivi sasa haipo tena.
Hiyo haina tofauti na upanuzi wa barabara kuanzia Morocco hadi Mwenge ambao kujengwa kwake kulitokana na amri ya aliyekuwa Rais wa Tanzania hayati John Magufuli baada ya kufuta shamrashamra za sherehe ya Uhuru, Desemba 2015 na kuamuru Sh4 billioni zilizokuwa zimetengwa zitumike kugharimia ujenzi huo.
Kwa hiyo kama unajijua kwamba hujafika Dar es Salam kwa miaka 10. Badili fikra zako, Manzese, Kijitonyama, Magomeni, Mbezi, Kigamboni na maeneo mengine mengi uliyokuwa na picha zake kichwani, zifute, fika upate picha na taswira mpya za jiji hili.
Bernard Kiluwa ambaye ni mkazi wa mkoa wa Katavi alisema mara ya mwisho kufika Dar es Salaam ni wakati kituo cha daladala kipo Ubungo nyuma ya Tanesco tofauti na sasa kuwa Mawasiliano.
“Nilipotea, nilipoambiwa hapa ndiyo Ubungo, daraja, kituo hakipo, barabara zilivyojengwa nilishindwa kujizuia kuuliza hapa ni wapi kila wakati,” anasema.
Alisema hata ujenzi wa barabara ya njia nane ya Kimara hadi Kibaha umefanya maeneo mengi kuwa na muonekano wa tofauti kuliko ilivyokuwa imezoeleka.
“Eneo kama Mbezi kwa Msuguri, Stop Over, Kimara Bucha, watu walikuwa wakipanga biashara zao hadi barabarani na ilikuwa ni alama kwetu tukiwaona tunajua hapa ni sehemu Fulani, sasa hivi kondakta asipotaja vituo unapotea,” alisema Bernard.
Bagamoyo road
Lakini siyo kusafiri tu na kurudi ndani ya jiji hili la Dar es Salaam ndiyo kumefanya baadhi ya watu kushangaa kubadilika kwa maeneo hayo, bali hata wale waliopo ndani ya jiji wakati mwingine hushangaa kilichofanyika.
“Hili eneo la Makumbusho hadi Morocco nilikuwa nina muda sijapita hiyo barabara, nilianza kwa kuona picha mtandaoni nikajua ni nje ya nchi nilipojaribu kufuatilia maoni nikagundua ni Tanzania tena Dar es Salaam ndipo niligundua nina siku nyingi sijatembea,” alisema Grace Richard.
Alisema mara nyingi amekuwa mtu wa kutoka nyumbani kwake Mbagala kwenda Posta kazini huku akieleza kuwa kupanuka kwa mji kumefanya huduma nyingi zilizokuwa zikifuatwa sehemu fulani kupatikana karibu kila eneo jambo linalofanya watu wasiende maeneo mengine.
“Kumebadilika, miaka sita nyuma na sasa kulivyo ukimuonyesha mtu hawezi kuamini,” alisema Richard.
Kurasini
“Kuna wakati ulikuwa unaweza kusubiri hadi saa zima ili upite hapa mataa ya Uhasibu, japokuwa ujenzi wa hili daraja la juu haujakamilika ila tumeshaanza kuona tofauti, magari yanayotoka Mbagala kwenda Posta hayakai foleni,” alisema Qauthar Alhamdu mkazi wa Kijichi.
“Ni hatua kubwa kwani hili limepunguza hata muda tunaotumia barabarani kwenda kazini tunaamini ujenzi ukikamilika itakuwa na faida,” alisema.
|
Kama uliwahi kujiuliza ni lini Tanzania itatekeleza miradi yake kwa makandarasi wake wa ndani, huu n
|
Kama uliwahi kujiuliza ni lini Tanzania itatekeleza miradi yake kwa makandarasi wake wa ndani, huu ni wakati sahihi na jawabu la swali hilo kupatikana.
Sababu ya maswali kama hayo ni uhalisia wa mwenendo wa utekelezwaji wa miradi mbalimbali nchini, ambayo aghalabu walipewa makandarasi kutoka nje ya nchi.
Kilichosababisha hali hiyo ni kile kilichowahi kuelezwa kuwa, kulikuwa na ombwe la utaalamu kwa makandarasi wazawa juu ya teknolojia za utekelezaji wa miradi hiyo.
Katika mazingira hayo, makandarasi wazawa walijiona kinachowastahili ni miradi midogomidogo ambayo hata thamani yake ni ndogo pia.
Lakini sasa mambo yamebadilika na hilo kinakwenda kuwa historia, baada ya Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuweka mpango wa kuhakikisha makandarasi wazawa wakiwemo wanawake wanapewa miradi.
Utekelezwaji wa adhma hiyo, umeanza kwa Serikali kutenga asilimia 10 ya bajeti ya kila mwaka ya maendeleo kwa ajili ya miradi ya mafunzo kwa vitendo.
Sambamba na hilo, angalau asilimia thelathini ya bajeti ya maendeleo imetengwa kwa ajili ya upendeleo kwa wazawa, huku asilimia tano ya bajeti ya miradi ya maendeleo ikitengwa kwa ajili ya makundi maalumu.
Hayo yote yanakwenda sambamba na ushiriki wa wanafunzi na wahitimu katika miradi mbalimbali ya ujenzi.
Mageuzi hayo ni matokeo ya marekebisho ya Sera ya Ujenzi ya Mwaka 2003, yaliyosababisha kutengwa kwa nafasi maalumu kwa wakandarasi wa ndani kushiriki katika miradi ya umma, ikiwemo barabara, maji na miundombinu.
Kwa mujibu wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi Tanzania (ERB), kufikia mwaka 2023, kulikuwa na wahandisi 23,000 waliosajiliwa nchini.
Kati yao, karibu 4,000 walikuwa wanawake, ikiwa ni takriban asilimia 17 ya wahandisi wote.
Makandarasi hao sio tu wanachangia moja kwa moja katika ujenzi wa miundombinu, bali pia wanasaidia kukuza uchumi wa ndani kwa kutoa ajira na kuimarisha sekta ya ujenzi.
Kwa mujibu wa Benki ya Dunia, sekta ya ujenzi inachangia takriban asilimia 13 ya Pato la Taifa (GDP) la Tanzania na sehemu kubwa ya ukuaji huo inatokana na ushiriki wa makandarasi wazawa.
Zaidi ya hayo, makandarasi wazawa wanahamasisha matumizi ya malighafi za ndani kama vile saruji, nondo na mbao, jambo ambalo linasaidia kukuza viwanda vya ndani.
Pia, inakadiriwa makandarasi wazawa wanazalisha takriban ajira 700,000 kila mwaka, idadi ambayo inatoa mchango mkubwa katika kupunguza tatizo la ajira nchini.
Juhudi zinaendelea kuhamasisha ushiriki wa wanawake kwenye sekta hii kupitia programu maalumu za mafunzo, ruzuku na usaidizi wa kifedha unaotolewa na Serikali pamoja na mashirika binafsi.
Kupitia uwezeshaji huo, Tanzania inaweza kujenga uchumi imara zaidi na miundombinu inayokidhi viwango vya kimataifa huku ikiwanufaisha raia wake moja kwa moja.
Wahandishi wanawake
Rais wa Chama cha Makandarasi Wanawake Tanzania, Judith Odunga anautazama mpango huo kama fursa kwa wakandarasi wazawa.
Anasema fursa hiyo itawaondoa kwenye mazoea ya kufanya kazi ndogondogo na zenye maslahi madogo, wakati zile kubwa zinafanywa na wakandarasi wa nje.
“Ni miaka mingi imepita tukiwa tunafanya miradi midogo ambayo thamani yake pia ni ndogo, lakini sasa hivi tumeambiwa tutaweza kufanya miradi mikubwa, fedha nyingi zilikuwa zinachukuliwa na wageni kwenda kwenye nchi zao,” anasema.
Anasema ni jambo jema Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia imeona umuhimu wa kuwakomboa wakandarasi wa ndani kwa kuwawezesha kutekeleza miradi mikubwa.
Kwa mujibu wa Judith, hatua hiyo ni furaha kwa mkandarasi, huku akiisihi Serikali kuharakisha mpango huo ili kuwanufaisha wanataaluma hiyo.
“Sisi tutakapoiona fursa naomba wakandarasi wenzangu tuichangamkie kwa kuomba kazi ili tuweze kuingia katika ulingo wa kupambania miradi hii,” anasema Judith.
Judith anasema ni imani yake wakandarasi wa ndani hasa wanawake wanafanya vizuri katika miradi hiyo na kwamba utaratibu huo utawahamasisha watoto wa kike kusoma masomo ya sayansi.
Wakandarasi wazawa wanasemaje
Mkandarasi mzawa ambaye pia ni Mkurugenzi wa kampuni ya Lazafa Co. Ltd, Magira Magira anasema kilichofanyika kitawakwamua makandarasi kwa kuwa watakuwa na uwezo wa kukua zaidi kitaaluma kama walivyo wa nje.
“Namshukuru Rais Dkt. Samia kwa namna alivyojipambanua kwamba sio mtu wa maneno mengi bali mtu wa vitendo pia namshukuru kwa namna ambavyo ameamua kuwainua makandarasi wa ndani,” anasema.
Anasema hatua hiyo, itawezesha miradi yote inayotekelezwa nchini ifanywe na wakandarasi wa ndani na hivyo kuifaidisha nchi kiuchumi.
“Nikuhakikishie kwamba tunakwenda kusimamia ujenzi wa daraja hili kuhakikisha kila kazi inakamilika kwa viwango vinavyokubalika, kulingana na mkataba,” anasema.
Anachosema Bashungwa
Akiwa katika mkutano wa mashauriano kati ya Serikali, makandarasi wazawa na washauri elekezi wa ndani jijini Dodoma, Novemba 21, 2023, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa anasema Serikali inaendelea kutenga miradi mingi kwa ajili ya makandarasi wazawa.
"Lengo la Serikali ya Awamu ya Sita ni kusaidia kujenga uwezo wa makandarasi wazawa, ili wakue na kupata uzoefu," anasema.
Katika mwaka wa fedha 2023/2024, anasema jumla ya miradi minne ya barabara yenye urefu wa Kilomita 50, imetengwa kwa ajili ya makandarasi wa ndani.
Si hivyo tu, anasema katika mwaka wa fedha 2023/2024 jumla ya Kilomita 20 za barabara zimetengwa kwa ajili ya makandarasi wanawake.
Anasema kazi hizo zitakazogawanywa katika vipande vya kilomita tano na kushindanishwa kwa kampuni za wanawake pekee.
"Hii inafanya jumla ya Kilomita 220 zijengwe na makandarasi wazawa kwa mwaka 2023/2024," anasema.
Pia, Bashungwa anasema kazi za matengenezo ya barabara zinazosimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara zenye thamani ya Shilingi Bilioni 600 zitatekelezwa na makandarasi wa ndani katika mikoa yote 26 nchini.
“Katika mwaka wa fedha 2023/2024, Rais Dkt Samia ameamua kazi zote za matengenezo ya barabara Kwa mikoa yote 26 nchini, zitekelezwe na makadarasi wa ndani,” anaeleza.
Kwa mujibu wa Waziri huyo, Sheria ya Ununuzi wa Umma imefanyiwa marekebisho kwa kuongeza kiwango cha thamani ya mradi utakaotekelezwa na makandarasi wa ndani, bila kushindanishwa na makandarasi wa nje.
Naye Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta anasema daraja hilo linajengwa kwa fedha za Serikali kwa asilimia 100.
Anasema litakapokamilika litarahisisha usafiri kwa majira yote ya mwaka, kwa saa 24 za siku.
|
Moja ya alama kuu za juhudi za Serikali katika kuimarisha miundombinu na kukuza uchumi, ni ujenzi wa
|
Moja ya alama kuu za juhudi za Serikali katika kuimarisha miundombinu na kukuza uchumi, ni ujenzi wa Daraja la JP Magufuli, ambalo awali liliitwa Kigongo Busisi.
Mabadiliko ya jina la daraja hilo lenye urefu wa kilomita 3.2 yana uhusiano wa moja kwa moja na historia ya Rais wa awamu ya tano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Magufuli.
Mitazamo ya wengi ilikuwa kufariki kwa Hayati Dkt. Magufuli, kungezima ndoto ya kukamilika kwa mradi huo, unaogharimiwa kwa Shilingi bilioni 716.3 zote zikitolewa na Serikali.
Aliyeipa uhai ndoto hiyo ni Rais wa Serikali ya awamu ya sita, Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye muda mchache baada ya kuapa kuwa Rais, alijipambanua kuiendeleza miradi iliyoachwa na mtangulizi wake, huku akianzisha mipya pia.
Daraja la JP Magufuli ni miongoni mwa miradi hiyo, ambayo mkuu huyo wa nchi sio tu anaiendelea mradi huo kuakisi ndoto ya Hayati Magufuli, bali pia analenga kuwaondolea changamoto wakazi wa Busisi na Kigongo mkoani Mwanza za kuvuka kutoka eneo moja kwenda lingine.
Ujenzi wa daraja hili ulianza rasmi mwaka 2019 na linatarajiwa kukamilika mwaka 2024.
Historia ya daraja na Hayati Magufuli
Katika ziara yake Desemba 31, mwaka 2020 kutembelea mradi huo, Dkt. Magufuli, aliwaambia wakazi wa eneo hilo kuwa anayo historia na daraja hilo, tangu wakati ambao hakuwa na wadhifa wa Urais.
“Siku moja niliondoka Mwanza kwenda Busisi kuposa, nimefika pale kwa Mzee mmoja ni Askari Magereza anaitwa Mathias Mbiza, nikamaliza kuposa na mahali tukapatana, wakati wa kurudi Kivuko kilikuwa MV Geita au Sengerema.”
Anaongeza, “Kikawa kimeharibika na kilikuwa kinafanya hivyo kila siku, nilikuwa na pikipiki yangu XL 125 Honda, kwahiyo kulikuwa na mitumbwi walikuwa wanavusha kwa pesa, kila mara kivuko kilipoharibika watu walipakiwa kwenye mitumbwi”.
Anasema alisogea karibu na eneo hilo na wavushaji walimtaka kuingia kwenye Mtumbwi na pikipiki yake, alipofikiria moyo ulikataa, wakati huo kulikuwepo na familia na baskeli yao walipakiwa.
“Mimi nikazunguka Kamanga, nilipofika Mwanza ule Mtumbwi ukawa umezama na ukaua watu 11, kwahiyo ninaifahamu na ndiyo maana nilipofanikiwa kuwa Waziri wa ujenzi mawazo yangu yalikuwa niokoe maisha ya watu wa hapa,” anasema.
Lafikia asilimia 90.5
Rais Dkt. Samia aliingia madarakani pamoja na mambo mengine, mradi huo ulikuwa sehemu ya ile aliyoiangazia kuhakikisha inakamilika.
Juhudi zilizofanywa na Serikali, zimewezesha kazi ziendelee kufanyika usiku na mchana na hatimaye, daraja hilo kufikia sasa ujenzi wa daraja hilo, umefikia asilimia 90.5.
Hilo, linathibitishwa na Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa daraja hilo, Abdulkarim Majuto Septemba 17, mwaka 2024.
Kwa mujibu wa Majuto, kazi zinaendelea kufanyika usiku na mchana na kwamba matarajio hadi kufikia mwanzoni mwa Oktoba 2024, daraja hilo liwe limeunganishwa.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Innocent Bashungwa anasema daraja hilo linaunganisha barabara kuu ya Usagara - Sengerema - Geita katika Ziwa Victoria na sasa lipo mbioni kukamilika, kwani kimebaki kipande cha mita mbili kuunganishwa.
Anasema ujenzi wa daraja hilo unaenda sambamba na ujenzi wa barabara unganishi zenye urefu wa kilometa 1.66 upande wa Kigongo na Busisi.
“Nimetembea kilometa tatu za Daraja la J.P Magufuli kujionea kazi, nimejiridhisha tumebakiza mita mbili ndicho kipande kilichobaki kukamilisha ujenzi wa kilometa tatu za daraja hili pamoja na barabara za maungio kiliometa 1.66 ambazo pia ujenzi unaendelea,” anasema Bashungwa.
Bashungwa aliyetembelea mradi huo Septemba 17, 2024 anamshukuru Rais Dkt. Samia kwa kusimamia maono yake na kuendeleza miradi yote iliyoasisiwa na mtangulizi wake.
Anasema Rais Dkt. Samia ameendelea kutoa fedha, ili ujenzi wa daraja ukamilike kwa wakati na kuanza kutoa huduma.
Anaeleza Serikali inaendelea kuhakikisha mkandarasi analipwa malipo yake, hivi karibuni amepokea Shilingi bilioni 18 zitakazomwezesha kukamilisha ujenzi wa daraja hilo ifikapo Desemba 2024.
Aidha, Bashungwa anampongeza Meneja wa Wakala ya Barabara (TANROADS) Mkoa wa Mwanza, mhandisi mshauri kampuni ya Yooshin Engineering Corporation (Korea) na mkandarasi wa kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation kwa kuendelea kutekeleza majukumu yao kikamilifu.
Bashungwa anaeleza ujenzi wa daraja hilo umetoa fursa kwa wataalamu wa ndani na wahitimu wa kada ya ujenzi kupata ujuzi na uzoefu, utakaosaidia kupunguza utegemezi wa wataalamu kutoka nje ya nchi.
La sita kwa urefu Afrika
Daraja la JP Magufuli limetajwa kuwa refu zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na kati, huku likishika nafasi ya sita kwa bara la Afrika.
Hilo lilithibitishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Barabara, Joseph Haule Julai mwaka juzi, alipokagua ujenzi wa mradi huo mkoani Mwanza.
Katika orodha ya madaraja marefu, linaloongoza ni 6th October lililopo nchini Misri lenye urefu wa kilomita 20.5.
“Kama mnavyoona Tanzania sasa tunazidi kupaa, tumeona madaraja mengine mengi makubwa na mazuri yakichukua rekodi lakini sasa daraja hili ndilo litakalovunja rekodi nchini, Afrika Mashariki na Kati,” anasema.
Mengine marefu ni Third Mainland la Nigeria (kilomita 11.8), Suez Canal la Misri (kilomita 3.9), Kisiwa cha Msumbiji (kilomita 3.8), na Dona Ana la Msumbiji (kilomita 3.67), kisha JP Magufuli linafuata.
Manufaa kiuchumi
Utekelezwaji wa mradi huo, siyo tu utaunganisha pande mbili za wakazi wa maeneo ya jirani, bali pia linafungua fursa nyingi za kiuchumi na kijamii.
Mradi huo pia, utapunguza gharama za usafirishaji kwa kuwa kwa sasa, kivuko cha Kigongo-Busisi kinabeba abiria na bidhaa kuvuka Ziwa Victoria, jambo linalosababisha msongamano mrefu na ucheleweshaji.
Kwa mujibu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, takriban magari 1,600 huvuka kwa kivuko hicho kila siku, huku abiria zaidi ya 2,000 wakikabiliwa na changamoto ya kungoja kwa muda mrefu.
Kwa kukamilika kwa daraja hilo, gharama za usafirishaji zinatarajiwa kupungua kwa asilimia 25 hadi 30, huku muda wa kusafiri kati ya mikoa hiyo ukipungua kutoka zaidi ya saa mbili hadi dakika chache.
Daraja hilo pia litaunganisha maeneo ya uzalishaji wa mazao kama dhahabu, pamba na samaki kutoka mkoa wa Geita na masoko ya Mwanza, ambayo ni kitovu cha biashara cha Kanda ya Ziwa.
Takwimu za Benki ya Dunia mwaka 2023, zinaonesha mradi huu unatarajiwa kuongeza thamani ya biashara kati ya mikoa hii kwa zaidi ya asilimia 40 katika kipindi cha miaka mitano baada ya kukamilika.
Ujenzi wa daraja hilo, umeajiri zaidi ya wafanyakazi 700 wa ndani, wengi wao wakiwa vijana wa kitanzania. Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2022 ya Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), ajira hizo zimechangia kuboresha hali ya maisha ya wakazi wa maeneo ya Kigongo na Busisi.
Pia, ripoti inakadiria kwamba ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja zitokanazo na mradi huo zinaweza kufikia zaidi ya 5,000 baada ya kukamilika, kutokana na kuanzishwa kwa shughuli za kibiashara kama migahawa, huduma za usafiri na biashara ndogondogo.
Utalii ni faida nyingine ya daraja hilo kwa kuwa Ziwa Victoria ni kivutio kikubwa cha watalii, mradi huo unatarajiwa pia kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea mkoa wa Mwanza na maeneo mengine ya Kanda ya Ziwa.
Kwa mujibu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), takwimu za mwaka 2022 zinaonyesha idadi ya watalii katika Kanda ya Ziwa iliongezeka kwa asilimia 10, huku matarajio ya ongezeko zaidi yakiwa ni asilimia 20 baada ya daraja kukamilika, kutokana na urahisi wa usafiri wa barabara.
|
Licha ya uwepo wa vivuko vya watembea kwa miguu kutazamwa kama muarobaini wa ajali barabarani, kwa b
|
Licha ya uwepo wa vivuko vya watembea kwa miguu kutazamwa kama muarobaini wa ajali barabarani, kwa baadhi ya wananchi vimekuwa kama vikwazo.
Hatua ya kuviona vikwazo inatokana na kile kinachoelezwa na baadhi yao kuwa, urefu wake, uvivu wa kupanda unawalazimu wakatize barabara badala ya kutumia vivuko hivyo.
Hata hivyo, uwepo wa vivuko hivyo kwa mujibu wa wananchi hao hao, umepunguza kwa kiwango kikubwa matukio ya ajali za barabarani zinazowahisisha watembea kwa miguu.
Mathalan, kwa kipindi cha mwaka huu eneo la Buguruni lilipo kimoja ya vivuko hivyo, zimetokea ajali tano pekee ukilinganisha na 12 za mwaka uliopita.
Hata hivyo, idadi hiyo ni pungufu ya ajali kwa asilimia 70, ukilinganisha na zile zilizokuwa zinatokea kabla ya kujengwa kwa kivuko hicho.
Mitazamo ya wananchi
Uwepo wa vivuko hivyo, umewapa wazazi uhakika wa usalama wa watoto wao ambao kila siku hulazimika kuvuka barabara wanapotoka na kwenda shuleni.
Rehema Mapande, anayeishi Mbagala jijini Dar es Salaam analithibitisha hilo, akisema awali walilazimika ama kuwasubiri watoto wawavushe, au wapate usaidizi kutoka kwa watu wazima.
“Kwa watoto wetu wanaosoma Chamazi kutokea Mbagala Rangitatu, kila siku walikuwa wanapata shida. Wakifika eneo hili lazima wamwombe mtu mzima awavushe,” anasema.
Anaeleza kwa kiasi kikubwa uwepo wa daraja hilo, umewasaidia watoto hao kuepuka ajali ingawa wapo wanaolitazama kama kero.
Kwa mujibu wa Rehema, kero hiyo inatokana na urefu wa daraja husika unaosababisha mvukaji kutumia muda mrefu, kuliko yule anayeamua kukatisha barabara.
“Daraja ni refu mtu anaona anazunguka anapopanda, kwa hiyo anaona afadhali akatishe barabara ambayo ni hatari kwake,” anasema.
Kwa mtazamo wa Rehema anayefanya biashara ya chakula lilipo daraja hilo, idadi ya ajali za watembea kwa miguu zimepungua kwa kuwa awali zilishuhudiwa mara kwa mara.
“Sisi wenzangu na mie waoga wa barabara tunapita juu kwenye daraja, wachache ndiyo wanalazimisha kupita chini,” anasema.
Pamoja na urefu wa daraja unaolalamikiwa na baadhi ya wananchi, Nas Everist dereva wa bodaboda anayeegesha karibu na kivuko hicho Mbagala anasema bora njia ndefu itakayokuepusha na ajali kuliko kukatisha na ukagongwa.
“Bora upite njia ndefu ya kupanda kivuko, kuliko ukatishe alafu ukapatwa na ajali. Sasa kipi bora upite hapo juu uende sokoni na kurudi au upite chini ugongwe na gari au bodaboda,” anaeleza.
Hata hivyo, anaibua changamoto nyingine ya baadhi ya watembea kwa miguu kupenya katika kingo za daraja hilo ili wakatishe barabara, kwa uvivu wa kupanda daraja.
Wingi wa ajali za watembea kwa miguu kabla ya uwepo wa daraja hilo, unathibitishwa pia na Everist, akisema kwa sasa zimepungua.
“Watu waliokuwa wanavuka kwenda sokoni hasa ndiyo waliokuwa wanagongwa, lakini kwa sasa wanapita juu hawakutani na shida hizo,” anaeleza.
Daniel Mgala Machinga katika daraja la watembea kwa miguu Buguruni jijini Dar es Salaam, anasema idadi ya ajali alizokuwa akizishuhudia kwa siku katika eneo hilo ni tofauti na sasa baada ya kuwepo kwa daraja.
Ingawa ajali zimepungua, Daniel anasema bado zinaendelea kutokea kutokana na uzembe wa baadhi ya watembea kwa miguu wanaoamua kuvuka barabara bila kupitia darajani.
“Lakini sasa wamepunguza sana ajali kupitia hili daraja, nashukuru Serikali kwa kuamua kujenga daraja hili,” anasema.
Anasema wanaopuuzia kutumia daraja hilo, wameamua kwa makusudi kuvunja utaratibu ilhali Serikali ilishauweka ili kuwaepusha na ajali.
“Uelewa ndiyo tatizo kwa hawa wanaopita chini kuvuka barabara, ningependa waendelee kuelimishwa na kuonywa ili waache tabia hiyo,” anasisitiza.
Pamoja na uwepo wa daraja hilo kuwa matumaini kwa wananchi wengi, Lilian Patrick anasema ni changamoto kwa wajawazito ambao kwa hali zao inakuwa vigumu kupanda daraja.
“Kwa wanawake hasa wajawazito inakuwa vigumu kupandisha daraja kwa hiyo, hawa mara nyingi ndiyo wanakatisha barabara,” anasema.
Anapendekeza watu wenye mahitaji maalumu wakiwemo wajawazito kuwekewa utaratibu maalumu ili kuwarahisishia kuvuka.
Hata hivyo, anasema daraja limesaidia kupunguza matukio ya ajali katika eneo hilo, ambayo kila siku alikuwa akiyashuhudia.
Dereva bodaboda anayeegesha katika daraja hilo la Buguruni, Hamisi Ally anaibua changamoto mpya baada ya uwepo wa daraja hilo, akisema linatumika kama hifadhi ya wahalifu.
“Hili ni daraja la waenda kwa miguu lakini unakuta hadi usiku mtu amekaa hajui kwamba hafanyi shughuli yoyote anaishia kuwaibia watu na kufanya vitendo vingine vya kihalifu,” anasema.
Hata hivyo, anasema uongozi wa Serikali ya Mtaa wa Maruzuku lilipo daraja hilo unaendelea kuwadhibiti wahalifu hao kwa kuwafanya bodaboda wawe walinzi.
“Sisi bodaboda wa hapa ndiyo tumepewa jukumu la ulinzi wa usalama wa eneo hili, kwa hiyo angalau matukio haya yamepungua kwa kiasi kikubwa,” anasema.
Anasema ajali hazikwisha isipokuwa zimepungua kwa kuwa wapo baadhi ya watembea kwa miguu wanaokatisha barabara badala ya kupanda darajani.
Kauli ya Serikali
Godfrey Malinda ni Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Maruzuku anayesimamia masuala ya ulinzi na usalama, anasema kabla ya daraja hilo, ajali zaidi ziliwahusisha wanafunzi wanaovuka kutoka na kwenda shuleni.
Hali hiyo, anasema imepungua maradufu kwa sasa kwa kuwa kuna daraja linalotumika na wananchi kuvuka, ingawa baadhi yao wanapuuzia.
Kuhusu wanaopuuzia, anasema wanatumia mianya iliyotokana na kuvunjwa kwa kingo za barabara kukatisha na kuacha kutumia daraja.
Anaeleza hao ndiyo wanaendelea kusababisha ajali za watembea kwa miguu ziendelee katika eneo hilo.
Akizungumza matukio ya uhalifu, anakiri yalikuwepo lakini ilipogundulika walianzisha utaratibu wa kuweka walinzi shirikishi.
“Kwa siku za sikukuu, walinzi hawa wanakaa kuanzia asubuhi hadi usiku na tumeweka marufuku ya mtu kufika katika eneo lile na kuzurura tu.
“Mara nyingi tukiwakuta tunawapeleka Polisi wanahojiwa waeleze kama wana sababu za msingi za kukaa katika eneo hilo usiku,” anasema.
Malinda anapendekeza kuboreshwa zaidi kwa daraja hilo, kutoka kuwa la kuhamisha sasa lijengwe la zege litakalokuwa inara zaidi na kutumika na wananchi wengi.
Takwimu
Mjumbe huyo, anasema mwaka huu pekee katika eneo hilo zimetokea jumla ya ajali tano zinazohusisha bodaboda na watembea kwa miguu.
Idadi hiyo imepungua ukilinganisha na ajali 12, zilizotokea katika eneo hilo mwaka 2023.
“Kuna wengine wamekufa kabisa, wengine wamepata ulemavu wa kudumu. Lakini ajali nyingi zinatokea kwa wale wazembe wanaotaka kuvuka barabara bila kutumia daraja,” anasema.
Hata hivyo, anasema idadi hiyo ya ajali ni upungufu wa asilimia 70 ya zile zilizokuwa zinatokea kabla ya uwepo wa daraja hilo.
Kauli ya Polisi
Ofisa kutoka Dawati la Elimu ya Usalama Barabara kutoka Ofisi ya Mkuu wa Usalama Barabarani jijini Dar es Salaam, Edwin Mtenga anasema kujengwa kwa vivuko hivyo ni matokeo ya mapendekezo ya askari hao.
“Vivuko hivi vilijengwa katika maeneo tete ili kusaidka kuwavusha watu, lakini kusaidia kupunguza msongamano kwenye maeneo hayo,” anasema.
Anasema vivuko hivyo vimejengwa hasa kwenye maeneo yenye makutano ya barabara kubwa ili kupunguza uwezekano wa ajali.
Kwa Dar es Salaam anasema vivuko hivyo vipo Buguruni, Manzese, Kimara, Mbagala, Mbezi na maeneo mengine.
“Vimetusaidia kupunguza ajali katika maeneo hayo. Lakini tuliyabainisha hayo maeneo kama ni tete. Kulikuwa na matukio mengi a watu kugongwa na gari au pikipiki, baada ya kujengwa kwa vivuko vimesaidia kupunguza matukio hayo,” anasema.
Kuhusu wanaolazimisha kupita chini, anasema jeshi hilo linaendelea kutoa elimu kwa wananchi hao kuhakikisha wanavitumia vivuko hivyo badala ya kupuuzia.
|
Ni saa 144 zinazounda siku sita, ndio jumla ya muda ambao Rais Samia Suluhu Hassan ameutumia mkoani
|
Ni saa 144 zinazounda siku sita, ndio jumla ya muda ambao Rais Samia Suluhu Hassan ameutumia mkoani Ruvuma kwa ziara ya kikazi.
Kwa mtazamo wa wanazuoni, ziara hiyo kwa maneno machache inatafsiriwa kuwa ya maelekezo, utatuzi kero, fursa na matumaini kwa wakulima.
Mtazamo huo wa wanazuoni, unaakisi uhalisia wa mlolongo wa matukio na kauli za Rais Samia akiwa katika ziara hiyo iliyoanza Septemba 23 na kuihitimisha Septemba 28, mwaka huu.
Ukiachana na zawadi nyingi ambazo aghalabu mkuu huyo wa nchi huzawadiwa anapotembelea maeneo mbalimbali, katika ziara hii alipokea zawadi ya Sh1,800 kutoka kwa wanafunzi wa shule ya awali na msingi ya Mchepuo wa Kiingereza ya Chief Zulu, jambo alilosema limeugusa moyo wake.
Awajibu wanaomwita muuaji
Ni ziara hiyo mkoani Ruvuma, ndiyo iliyoibua kauli ya Rais Samia dhidi ya shutuma zinazotolewa na wanasiasa hasa wa upinzani, wakimhusisha na matukio ya kutekwa, kutoweka na kuuawa kwa watu.
Rais Samia alitumia hotuba yake katika hafla ya kufunga Kikao cha Mafunzo cha Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa CCM, kuweka wazi kuwa, hakuwahi kuua mtu, labda umasikini na giza.
Katika hotuba yake hiyo ya takriban nusu saa, aliipa UWT jukumu la kuwajibu wanaotoa kauli hizo dhidi yake, akiwasisitiza wasihofu kujibu.
“Ombi langu kwenu (UWT) ni kusimama imara ukweli mnaujua, mdomo wa Mwenyekiti mmoja kujibu hoja zile hautoshelezi na Pengine Mwenyekiti wakati mambo yale yanatoka nipo kwenye majukumu mengine, msimame tu mjibu mnahofia nini,” alisema.
Alikwenda mbali zaidi na kuwaeleza, wakiambiwa Mwenyekiti wao ni muuaji wanapaswa kujibu ameuwa njia zote za kuzidisha umasikini katika nchi na amekuza uchumi.
Kadhalika, katika hoja hiyo hiyo ya kuitwa muuaji, amewataka wajibu kwa kusema ni kweli ameua giza lililokuwa limegubika Tanzania na sasa nchi ipo katika kiwango cha kimataifa cha kung’aa.
“Hayo ndiyo niliyouwa Rais wenu na Mwenyekiti wenu, sijawahi kuua mtu labda sisimizi nimeuwa, lakini sio mtu. Kwa hiyo ndugu zangu simameni tu mjibu,” amesema.
Akizungumzia hilo, Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Dk Conrad Masabo alisema ingawa ni sahihi kutoa majibu kwa wanaojenga hoja hizo, pia alisisitiza umuhumu wa changamoto za utekaji kushughulikiwa.
Alieleza kauli dhidi ya Rais zisiaminiwe kuwa yeye ndiye anayehusika moja kwa moja na vitendo hivyo, isipokuwa mamlaka aliyonayo yanafanya baadhi ya watu watupe lawama kwake, akifananisha na msemo 'ukubwa kalala.'
Katika mazingira hayo, alisema kuwataka UWT wajibu ni sahihi kisiasa, lakini naye anapaswa kuzungumza asiwaache waendelee kumchafua.
"Ninaona hatari ya watu kimesema vibaya zaidi Rais, maana wakati UWT wanajibu naamini na upande mwingine utajibu, sasa atakayeathirika zaidi ni mwenye dhamana ya uongozi," alifafanua.
Matumaini kwa wakulima
Ziara hiyo ilihitimishwa na kauli ya matumaini kwa wakulima hasa wa Kahawa kwa kile alichoeleza Rais Samia kuwa, kuanzia mwakani Serikali inafanya mageuzi ya mfumo wa mauzo ya kahawa.
Mageuzi hayo kwa mujibu wa Rais Samia, yanahusisha kuondoa utaratibu wa malipo ya wakulima, kupitia Vyama Vikuu vya Ushirika, kisha vyama vya msingi ndipo yawafikie.
Alisema mwakani, mkulima atkayeuza kahawa yake na mazao mengine, fedha zake atazipokea kutoka kwenye chama chake kikuu cha ushirika na haitapita kwingine kokote.
Msingi wa maelekezo yake hayo ni kile alichobinisha, kuna harufu ya kukatwakatwa kwa fedha hizo za wakulima, pia mfumo huo unatengeneza urasimu na kuwachelewesha wakulima kupata haki zao.
Baadhi ya wakulima wanasema hatua hiyo itawafaidisha zaidi na shughuli zao, wakisisitiza utekelezwaji wa hilo ungepaswa kuanza sasa.
“Kwa kuwa wameambiwa mwakani wanatumia muda uliobaki kutukata malipo yetu ili wafaidishe matumbo yao.
“Yote haya wanayafanya kwa sababu hawajui uchungu wa kulima. Wengi sio wakulima wa jembe la mkono, wanakaa ofisini tu kuelekeza,” alisema Mtutula Mtutula mkulima mkoani Ruvuma.
Wakulima wawaepuke walanguzi
Vitendo vya baadhi ya wakulima kuendelea kuwauzia mahindi walanguzi wanaonunua kwa bei ya chini, ilhali Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) inanunua kwa bei nzuri, ni jambo lingine lililomwibua mkuu huyo wa nchi katika ziara yake hiyo.
Akiwasalimia wananchi wa Mbinga Sokoni, Septemba 25, mwaka huu, Rais Samia aliwataka wakulika wabadilike na kuacha kuwauzia mazao walanguzi.
Aliijenga hoja yake hiyo kwa ufafanuzi kuwa, walanguzi hununua kilo moja ya mahindi chini ya Sh400, huku NFRA imewekwa kununua kuanzia Sh400 na kuendelea, ni vema wakulima wawaepuke walanguzi.
Alisema kuwauzia walanguzi kunawafanya wakulima wasinufaike na shughuli zao, huku akiitaka NFRA kuendelea kusalia eneo hilo, hadi mahindi yote ya wakulima yatkaponunuliwa.
“Serikali inataka vizuri na imejitahidi kila inapoona kuna changamoto za wakulima inazitatua, lakini wakulima wenyewe nanyi mnapaswa kubadilika,” alisema.
Maagizo kwa Bashe, Aweso, Pindi
Baada ya kuweka Jiwe la Msingi la ujenzi wa mradi wa maji Mtyangimbole katika Halmashauri ya Madaba mkoani Songea, Rais Samia alimtaka Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ahakikishe mradi huo unatoa huduma hiyo baada ya miezi mitatu.
Hatua ya kuelekea hivyo, inatokana na uhalisia wa changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo, inayowakabili wakazi wa eneo hilo, waliosema aghalabu hutegemea maji ya visima na mabwawa ambayo si salama.
“Tunachota maji kwenye visima vya watu binafsi, lakini huwa vinakauka kwa hiyo tutakwenda kuchota mabondeni. Hayo ya mabondeni ni machafu na wanatumia wanyama wengine pia,” amesema Zainab Kanyale mkazi wa Madaba.
Rais Samia alisema kwa kuwa wananchi wameona jiwe la msingi zimewekwa, wamepata matumaini, hivyo kufikia Desemba Aweso ahakikishe mradi huo unatoa maji.
“Hakikisheni kufikia Desemba mwaka huu maji yanatoka hapa wananchi wale krismas huku wanaoga, kwa sababu tumeweka Jiwe la Msingi tumewapa matumaini,” amesema.
Agizo lingine ni kwa Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe aliyemtaka ahakikishe kufikia mwakani malipo ya wakulima katika zao la kahawa yanafanywa kupitia Chama Kikuu cha Ushirika kisha mkulima moja kwa moja.
Sambamba na hilo, agizo lingine lilimlenga Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Pindi Chana aliyetakiwa kuongeza ndegenyuki, vituo na askari wa kudhibiti wanyama waharibifu kwenye mazao ya wakulima wilayani Tunduru.
Akerwa wanaonyamazia uzushi
Katika ziara yake hiyo, alipotembelea Wilaya ya Tunduru, kuliibuka taarifa katika mitandao ya kijamii zinazomwonyesha mgonjwa akibebwa katika tenga kupelekwa hospitali kutoka Kituo cha Afya cha Mchoteka.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hatua ya wagonjwa kubebwa kwenye matenga, inatokana na kushindwa kumudu gharama za kukodi gari la kubebea wagonjwa ambazo ni Sh80,000 hadi Sh100,000.
Taarifa hizo zilianza kujibiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mchengerwa aliyasema ni uzushi.
Ameijenga hoja yake hiyo kwa kufafanua, Tunduru ni moja ya wanufaika wa magari ya kubebea wagonjwa manne kati ya zaidi ya 500 yaliyonunuliwa hivi karibuni.
Si hivyo tu, alisema Wilaya hiyo pia, ni mnufaika wa programu ya M-mama inayowaaniri madereva wa magari binafsi kubeba wagonjwa pale inapotokea gari la kubebea wagonjwa halipo.
Alisema takriban madereva 20 wamesajiliwa na kulipwa fedha kuifanya kazi hiyo, hivyo hakuna uhaba wa gari za kubebea wagonjwa kama ilivyozushwa.
Alipozungumza Rais Samia alionyesha kukerwa na hatua ya viongozi katika eneo hilo, kunyamazia uzushi huo na kusubiri viongozi wa kitaifa wakanushe.
“Kama kunarushwa picha ya uongo katika mitandao, katika maeneo yetu kuna wakuu mbalimbali wapo, lakini hakuna anayekanusha, kwamba hiyo picha sio ya leo.
“Kwamba hii hospitali au hilo eneo sasa hivi ipo katika hali hii na ikapigwa picha ikiwa katika hali hii kuondoa ule upotofu uliofanywa, sijui tunaelekea wapi,” alisema.
Alisema sio sawa kusubiri Rais au Waziri aende katika eneo husika akanushe uzushi, ilhali kuna viongozi ambao uzushi huo unawahusu moja kwa moja.
“Hii ni sawa mwanaume kaingia nyoka nyumbani kwako, unakwenda kumwita mwanaume mwenzio njoo nitolee nyoka nyumbani kwangu,” alisisitiza.
Alieleza kama wanazushiwa kwenye maeneo yao, ilhali maendeleo yanafanyika na fedha zinapelekwa, hiyo sio sawa.
“Kama kwenye nyuma yako unazushiwa, maendeleo yanakuja, fedha zinatoka, alafu anatokea mpuuzi mmoja anaweka picha za ajabu ajabu, lakini viongozi mmenyamaza kimya, mpaka Waziri aje awakanushie, mnatutia wasiwasi ndugu zangu,” alisema.
Hakikisho la kulipwa fidia
Hata hivyo, Rais Samia katika ziara yake hiyo, aliwahakikishia wananchi wanaopisha miradi ya maendeleo, kulipwa fidia zao.
Ingawa inaweza kuchelewa, amesema Serikali itahakikisha inampa kila mwananchi haki yake anayoistahiki.
Aliitoa kauli hiyo, akijibu ombi la Mbunge wa Madaba, Dk Joseph Mhagama aliyeomba wananchi watakaopitiwa na ujenzi wa barabara ya Makambako walipwe fidia.
“Hakuna mradi utakaopita kwa wananchi, Serikali ichukue ardhi bila kulipa fidia za watu. Inaweza ikachekewa lakini sio kwamba Serikali itaacha kabisa kulipa fidia,” alisema Rais Samia.
Ni ziara ya fursa Songea
Siku sita za ziara hiyo, zilitosha kujaza vyumba vya nyumba za kulala wageni hasa wilayani Songea, baada ya watu mbalimbali kufurika mkoani humo na hivyo kuibua fursa kwa wananchi.
Sakina Issihaka ni mmoja wa wahudumu katika nyumba ya kulala wageni Songea, alisema wateja walizuia vyumba tangu Septemba 20 na wengi wanahisi kuviachia Septemba 29, mwaka huu.
“Hapa vyumba vimejaa, hata nyumba nyingine ya jirani hapo nako vyumba vimejaa, huwezi kupata chumba kwa ugeni huu walivizuia mapema,” amesema Sakina.
Hali ilivyo kwa Sakina ndivyo ilivyo kwa Modesta Zullu aliyasema tayari vyumba vilizuiwa na karibu kila siku wanakwenda wateja kuulizia nafasi lakini zimejaa.
“Tofauti na ugeni huu, huwa vyumba vinakuwepo. Mimi napata wastani wa wateja watano Kati ya vyumba 10 vilivyopo, lakini kwa sasa vyote vimejaa,” amesema.
Hata hivyo, pamoja na ziara hiyo ya Rais Samia, katika Mji wa Songea kulifanywa Tamasha la tatu la Taifa la Utamaduni, ambalo pia lilichochea ongezeko la watu.
Kufungwa kwa tamasha hilo, ndiyo iliyokuwa shughuli ya kwanza ya Rais Samia katika ziara yake hiyo.
Mtazamo wa jumla
Akizungumzia ziara hiyo, Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk Revocatus Kabobe alisema mbali na uzinduzi na ukaguzi wa miradi, kilichofanyika ni muhimu kwa wananchi na Serikali kwa ujumla.
Umuhimu kwa wananchi unatokana na kile alichoeleza, watanufaika na huduma kutoka katika miradi husika, lakini kwa Serikali imejionea na kujipima nguvu inazotumia katika kuleta maendeleo.
Lakini kwa mtazamo mwingine, Dk Kabobe alisema ziara hiyo imekuwa muhimu hata kwa CCM kujiimarisha kwa kuwavutia wananchi.
“Ziara hii ni muhimu sana kwa CCM pia, sababu imekuwa ni sehemu ya kuendelea kuonesha yale yaliyoyafanywa kwa wananchi na kuhamaisha kuungwa mkono kupitia uchaguzi wa serikali za mitaa,” alieleza.
|
Rais Samia Suluhu Hassan ameonyesha kukerwa na tabia ya baadhi ya viongozi wanaoacha taarifa za uzus
|
Rais Samia Suluhu Hassan ameonyesha kukerwa na tabia ya baadhi ya viongozi wanaoacha taarifa za uzushi zisambae bila kuzikanusha.
Kinachomkera zaidi ni kile alichofafanua, pamoja na uzushi huo aghalabu hutokea na kuyahusu maeneo yenye wawakilishi wa Serikali, lakini wanasubiri viongozi wa kitaifa waje kukanusha.
Kauli hiyo ya Rais Samia inakuja kufuatia taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii, zikionyesha picha ya mtu anayedaiwa kuwa mgonjwa aliyebebwa kwenye tenga kupelekwa hospitali.
Taarifa hiyo inadai, mgonjwa huyo mkazi wa Mchoteka wilayani Tunduru amebebwa katika tenga hilo, baada ya kushindwa kulipa gharama za kukodi gari la kubebea wagonjwa.
Kutokana na taarifa hizo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mchengerwa alieleza kinachosambazwa ni uzushi.
Ameeleza kwa sasa hakuna changamoto ya gari za kubebea wagonjwa kwa kuwa Serikali ilinunua magari ya kubebea wagonjwa 530 yaliyosambazwa kwenye halmashauri mbalimbali.
Katika mgawo huo, amesema halmashauri ya Tunduru imepokea magari manne kwa ajili ya kusambazwa kwenye vituo mbalimbali vya afya.
Mchengerwa alisema magari hayo yaliyoenda
katika vituo vya afya vya Nakapanya, Matemanga, Tunduru Kusini na Nalasi.
Si hivyo tu, amesema Tamisemi ina programu ya M-MAMA inayolipa fedha kwa madereva wa kijamii kuwabeba wagonjwa pale inapotokea gari la wagonjwa halipo.
Ameeleza kwa Tunduru, Sh19 milioni imetolewa kwa ajili ya kuwapa madereva 20 kwa ajili ya kutekeleza kazi hiyo.
“Picha hizi zinazosambaa zinalenga kuwachanganya Watanzania, kazi unayoifanya (Rais Samia) ni kubwa. Picha hizo za zamani,” amesema.
Ufafanuzi wa Mchengerwa, ndiyo uliomuibua Rais Samia akionyesha kukerwa na hatua ya kusubiriwa viongozi wa kitaifa wakanushe uzushi unaoyahusu maeneo yenye viongozi wa ngazi husika.
Kauli ya Rais Samia
Rais Samia aliyasema hayo jana, alipozungumza na wananchi wa Tunduru, ikiwa ni siku ya nne ya ziara yake ya siku sita katika Mkoa wa Ruvuma.
“Kama kunarushwa picha ya uongo katika mitandao, katika maeneo yetu kuna wakuu mbalimbali wapo, lakini hakuna anayekanusha, kwamba hiyo picha sio ya leo.
“Kwamba hii hospitali au hilo eneo sasa hivi ipo katika hali hii na ikapigwa picha ikiwa katika hali hii kuondoa ule upotofu uliofanywa, sijui tunaelekea wapi,” alisema.
Alisema sio sawa kusubiri Rais au Waziri aende katika eneo husika akanushe uzushi, ilhali kuna viongozi ambao uzushi huo unawahusu moja kwa moja.
“Hii ni sawa mwanaume kaingia nyoka nyumbani kwako, unakwenda kumwita mwanaume mwenzio njoo nitolee nyoka nyumbani kwangu,” alisisitiza.
Alieleza kama wanazushiwa kwenye maeneo yao, ilhali maendeleo yanafanyika na fedha zinapelekwa, hiyo sio sawa.
“Kama kwenye nyuma yako unazushiwa, maendeleo yanakuja, fedha zinatoka, alafu anatokea mpuuzi mmoja anaweka picha za ajabu ajabu, lakini viongozi mmenyamaza kimya, mpaka Waziri aje awakanushie, mnatutia wasiwasi ndugu zangu,” alisema.
Alieleza kitendo hicho kinaonyesha tafsiri kuwa, katika eneo husika hakuna viongozi.
Mbali na hilo, Rais Samia alitumia mkutano huo kueleza uwepo wa soko la madini na ushindani unawahakikisha wachimbaji na wauzaji bei na mapato zaidi.
Kauli hiyo ni baada ya kuzindua soko la madini katika Wilaya ya Tunduru.
Alieleza kati ya Julai na Agosti mwaka huu, Serikali ilipokea Sh6.3 bilioni kama maduhuri ya Serikali kutokana na madini katika Mkoani Ruvuma.
“Ni mapato hayo ambayo yanatuwezesha kuja kufanya shughuli za maendeleo kama walivyosema wabunge wenu,” alisema.
Kadhalika, alieleza katika eneo hilo kuna masoko mawili ya zamani, akimtaka Waziri wa Madini, Anthon Mavunde kukaa na wachimbaji wadogo na sekta binafsi wazungumze kuona wanashirikianaje kufanikisha ujenzi.
Hata hivyo, aliahidi kufufua kiwanda cha Korosho katika eneo hilo, kwa kuwaagiza Waziri wa Viwanda na Biashara (Seleman Jaffo) kwa kushirikiana na Msajili wa Hazina (Nehemiah Mchechu) kukifufua kiwanda hicho kwa kumtafuta mwekezaji mwingine mwenye uwezo stahiki.
Kuhusu ndovu, alisema Serikali imeanza kuchukua hatua kwa kuongeza askari hadi ngazi za vijiji wanaoshirikiana na wengine.
Alisema magari ya doria yapo katika Wilaya husika na sasa kuna ndege nyuki zinazokimbiza tembo.
“Tunajua kuna tatizo la tembo lakini tumeanza kuchukua jitihada hizo, lengo letu ni kuongeza ndege nyuki na askari,” alisema.
Mapato madini kwa siku 84
Awali, akizungumza katika uzinduzi wa soko la madini Tunduru, Waziri Mavunde alisema katika siku 84 za mwanzo wa mwaka huu wa fedha, mauzo ya madini yameingiza Sh225 bilioni katika Mfuko Mkuu wa Serikali.
Kiwango hicho cha fedha kilichoingizwa, alisema ni matokeo ya uwepo wa masoko 43 ya madini na vituo 102 vya ununuzi wa rasilimali hiyo.
Kwa mujibu wa Mavunde, kiasi hicho cha fedha kilichoingizwa kinaonyesha matumaini katika kulifikia lengo la mwaka huu wa fedha, ambalo ni kuingiza Sh1 trilioni katika mfuko mkuu wa Serikali.
“Miradi ni ile ile, tumeongeza ufanisi, ufuatiliaji wa utoroshaji madini na kusimamia sheria,” alisema.
Hata hivyo, Mavunde alisema katika mwaka wa fedha uliopita, kiasi cha Sh1.7 trilioni kilizunguka kama sehemu ya biashara katika masoko yote 43 ya madini.
Hatua hiyo kwa mujibu wa waziri huyo, ilisaidia kuongeza wastani wa mapato yaliyoingia katika mfuko huo kufikia Sh753 bilioni kwa mwaka wa fedha 2023/24.
Alisema kiasi hicho ni kikubwa zaidi ya kile kilichoingizwa katika mwaka wa fedha 2015/16 ambacho ni Sh151 bilioni.
“Kabla ya mabadiliko ya Sheria ya Madini ya mwaka 2017, Tanzania haikunufaika na sekta hii na baada ya sheria, masoko na vituo vya ununuzi wa madini vilianzishwa,” amesema.
Akizungumzia mradi wa soko la madini Tunduru, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Chizya Marando amesema ujenzi wake umetekelezwa kwa ushirikiano na wafanyabiashara.
Ujenzi huo ulioanza Desemba mwaka jana, amesema umegharimu Sh1.4 bilioni na kati ya hizo, Sh1.37 bilioni zimetokewa na wafanyabiashara na Sh300 milioni ni halmashauri.
‘Mradi wa Uranium uharakishwe’
Mbunge wa Namtumbo, Vita Kawawa aliiomba Serikali kuharakisha utekelezaji wa mradi wa uchimbaji wa madini ya uranium ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika eneo hilo.
Hoja hiyo aliibua mbele ya Rais Samia aliyesimama katika eneo hilo kuzungumza na wananchi, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake mkoani Ruvuma.
Kawawa aliijenga hoja hiyo kwa kueleza uwepo wa hofu kwa wananchi wa Namtumbo, juu ya ucheleweshwaji wa mradi huo.
Hata hivyo, kinachoelezwa na Mbunge huyo kinashinikiza kuharakishwa kwa tathmini ya kimkakati ya mazingira (SEA) inayoendelea ili kuchunguza uwezekano wa uchimbaji na masharti kabla ya shughuli hizo katika eneo hilo.
Mapema mwezi huu, Naibu Waziri wa Madini, Dk Stephen Kiruswa alisema mchakato wa kuchagua kampuni itakayofanya SEA uko ukingoni na tayari zabuni imetangazwa.
Inakadiriwa Tanzania ina tani 55,000 za akiba ya madini ya uranium iliyothibitishwa hadi mwaka 2022, ingawa uchimbaji wa kibiashara bado haujaanza rasmi.
Eneo la Mto Mkuju wilayani Namtumbo linaaminika kuwa na akiba kubwa zaidi ya uranium nchini, ikiwa na tani milioni 182.1 za mabaki ya madini hayo na kiwango cha uranium kinachofikia asilimia 0.025.
Mbunge Kawawa alisisitiza umuhimu wa kuharakishwa mradi huo, “Mradi huu wa muda mrefu umewaacha wananchi wakiwa na maswali kuhusu lini utaanza.
“Tunaomba mara tu matokeo ya awali ya utafiti yanapopatikana, ruhusa ya uchimbaji itolewe haraka,” amesema Kawawa.
Alibainisha kuwa wilaya hiyo haina viwanda vya kutosha, huku akitaja faida za kiuchumi zilizopatikana wakati wa utafiti, ikiwemo ajira kwa vijana na kuongezeka kwa mzunguko wa fedha.
Katika hatua nyingine, alitumia jukwaa hilo kueleza uwepo wa changamoto ya uvamizi wa tembo, akisema zaidi ya kaya 400 zimeathirika.
Akijibu malalamiko hayo, Rais Samia aliwahakikishia wakazi kuwa Serikali inashughulikia kila ombi la Mbunge na wananchi kwa ujumla kwa njia zinazostahili.
|
Rais Samia Suluhu Hassan amesema sambamba na Serikali kuanza ujenzi wa bandari ya Mbambabay, pia ina
|
Rais Samia Suluhu Hassan amesema sambamba na Serikali kuanza ujenzi wa bandari ya Mbambabay, pia inatarajia kuzungumza na Serikali ya Malawi juu ya ushirikiano katika huduma za bandari hiyo.
Hatua hiyo kwa mujibu wa Rais Samia, inalenga kufungua milango ya ushirikiano wa kibiashara kupitia bandari hiyo kwa mataifa hayo, kwa kuwa bandari ya Mbambabay itahudumia mizigo inayotoka Malawi.
Mkuu huyo wa nchi anaeleza hayo baada ya kuweka Jiwe la Msingi la ujenzi wa bandari hiyo unaotarajiwa kufanyika kwa kipindi cha miezi 24, ukigharimu Sh70 bilioni.
Kujengwa kwa bandari hiyo, pamoja na mambo mengine, kunalenga kuimarisha ushoroba wa maendeleo ya Mtwara na kurahisisha uhudumiaji wa mzigo kutoka nchini Malawi kwa kuwa ndiyo njia fupi kutoka bandari ya Mtwara.
Rais Samia ameyasema hayo leo, Septemba 25, 2024 katika mkutano wake na wananchi uliofanyika Viwanja vya Maegesho ya Bandari ya Mbambabay, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya siku sita mkoani Ruvuma.
Amesema uwepo wa bandari hiyo pekee hautatosha kuleta mafanikio yanayotarajiwa, isipokuwa kunahitajika kuwepo huduma nzuri za usafirishaji wa mizigo.
Katika hilo, ameitaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kupitia kamati za pamoja, kuzungumza na Serikali ya Malawi.
Mazungumzo hayo, amesema yajikite katika kuisihi Serikali ya Taifa hilo, ijengwe miundombinu ya kupokea na kusafirisha mizigo kupitia bandari ya Mbambabay.
“Hii ndiyo diplomasia ya uchumi, nchi moja inaanza lakini mnazungumza na nchi ya pili ili muungane muelewane na wao waweke miundombinu inayofaa kupokea mizigo itakayotokea Tanzania na hivi ndivyo biashara inavyofanyika,” amesema.
Ushirikiano wa namna hiyo, amesema haufanyiki kwenye bandari hiyo pekee, tayari unafanyika katika miradi mbalimbali ukiwemo wa Reli ya Kisasa itakayounganisha Tanzania na Burundi.
Amesema hata barabara kubwa zinazoiunganisha Tanzania Kenya, Msumbiji na Uganda ni sehemu ya miradi inayotekeleza diplomasia ya uchumi na itifaki za biashara huru katika eneo la Afrika.
Hata hivyo, amesema tangu mwaka 2019 akiwa bungeni, amekuwa akimsikia Mbunge wa Nyasa, Stella Manyanya aliomba kujengwa Kwa bandari hiyo.
Amesema hatimaye miaka 10 baadaye, ujenzi wa bandari hiyo umeanza kwa kuwekwa Jiwe la Msingi na kwamba adhma inatimia.
Amesisitiza bandari hiyo itarahisisha usafiri na usafirishaji wa bidhaa kutoka na kwenda Malawi na inatarajiwa kuongeza fursa hasa kwa wananchi.
Ameitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kukamilisha mradi huo kwa wakati, viwango na ubora kama uliokubaliwa katika mikataba.
Aidha, akiwa wilayani Nyasa, Rais Samia amezindua barabara ya Mbinga-Mbambabay yenye urefu wa kilomita 66.
Kuhusu barabara hiyo, amesema ujenzi wake umetokana na ufadhili wa Sh630 bilioni kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).
Mbali na mradi huo, amesema kwa mara ya kwanza benki hiyo itasaidia mkopo wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) eneo la Kigoma inayounganisha na nchi ya Burundi.
Amewataka madereva wanaotumia barabara hiyo wahakikishe haileti masikitiko kwa ajali, badala yake inawapa furaha.
Uvuvi wa vizimba
Katika mkutano huo, Rais Samia amewataka wavuvi wilayani humo kuhakikisha wanakuwa na vizimba, huku akiisisitiza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenda kutoa elimu ya uvuvi huo.
Sababu ya hilo ni kile alichoeleza, uvuvi wa vizimba unawapa wavuvi fursa ya kufnya shughuli zao hata Serikali inapofungia maziwa.
“Pale tunapobaini kwamba rasilimali zilizomo ndani ya maziwa zinapungua, huwa tunafunga kwa miezi kadhaa ili rasilimali hizo zijizalishe tena. Kwa hiyo uvuvi wa vizimba unasaidia msikose kuvua nyakati hizo,” amesema.
Kuhusu zao la kahawa, amesema pamoja na mambo mzuri yaliyofanywa na Serikali, kuna changamoto ya makato ya malipo ya wakulima ambayo kwa sasa yanashughulikiwa.
Sambamba na hilo, amewataka wakulima wote, waendelee kuzingatia kanuni za kilimo bora na wavune pale inapokuwa imeiva na hata uzalishaji usiathiri soko la Kimataifa.
Kwa kuwa katika eneo hilo wanachimba madini, amesema Serikali itahakikisha inawasaidia wachimbaji hasa wadogo ili wanufaike huku nchi nayo ikinufaika.
Amewataka wachimbaji hao kutouza nje ya nchi madini bila kufuata njia halali, kwani kufanya hivyo kunaathiri mapato ya Serikali.
Ametumia fursa hiyo kueleza kuwa, anatambua uwepo wa baadhi ya vijiji visivyopata umeme, lakini kupitia mradi wa ujazilizi vyote vitapata nishati hiyo.
Uchaguzi Serikali za Mitaa
Amesema hana mashaka kwamba Wilaya hiyo ni ya kijani na njano ingawa ameona rangi nyingine.
Amesema kila mwenye sifa ya kuchaguliwa ahakikishe anaomba nafasi na kwamba mwenye haki ya kupiga kura ajitokeze kufanya hivyo.
Kuanza Oktoba 11, mwaka huu, amesema wananchi wajitokeze kujiandikisha katika daftari la uboreshaji wa taarifa za mpigakura.
Ametaka wananchi wote wanaotaka kuleta fujo kuelekea uchaguzi wanapaswa wakemewe.
“Tusikubali kurudisha nyuma kwa siasa zisizojami maslahi ya nchi wala sisi wananchi,” amesema.
Awali, akimkaribisha Mkuu wa Nchi, Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema hatua ya kukamilika kwa miundombinu hasa ya barabara ya Mbinga-Mbambabay inaufungua Mkoa wa Ruvuma ambao awali ulijifunga kwa kushindwa kuingiliana na mikoa mingine.
Amesema Tanroads imejenga mtandao wa barabara za kiwango cha lami kilomita 12,209, kati hizo, kilomita 2,384 sawa na asilimia 20 ya mtandao wote zimejengwa kwa ufadhili wa Benki ya AfDB.
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Patricia Laverley amesema kujengwa kwa barabara hiyo ni sehemu ya mchango na ushirikiano wa benki hiyo na Serikali ya Tanzania.
Ameeleza kukamilika kwake, hakutaishia kupunguza gharama za safari bali hata matengenezo ya magari yanayopita katika barabara hiyo.
“Mwaka jana zaidi ya magari 4,000 yanafanya safari katika barabara hii na kusafirisha abiria na mizigo, lakini mwaka 2015 tulivyokuja ni chini ya magari 150 ndiyo yaliyokuwa yanapita,” amesema.
Kwa upande wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Mohamed Besta amesema barabara hiyo inaunganisha Mikoa ya Ruvuma na Mtwara.
“Ujenzi wa barabara hii umefadhiliwa na benki ya AfDB kupitia mradi wa uboreshaji wa miundombinu ya barabara kwa Sh670 bilioni na kati ya hizo Serikali imetoa Sh70 bilioni,” amesema.
Kwa mujibu wa Besta, ujenzi wake umefanywa na kampuni ya uhandisi ya Chico kutoka nchini China na ulikamilika mwaka 2021.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Miundombinu, Suleiman Kakoso amesema bandari hiyo inaunganisha ukanda wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kupitia nchi ya Malawi na itaifanya Bandari ya Dar es Salaam ifanyie kazi vizuri.
Amesema zaidi ya kilomita 3,000 za barabara zimejengwa kwa kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Rais Samia.
“Tunashukuru na tunakuahidi tutaendelea kuiunga mkono Serikali yako,” amesema.
|
Kama ulidhani kuzaliwa kwako na baba na mama kunakupa uhalali usio na shaka wa kurithi mali walizona
|
Kama ulidhani kuzaliwa kwako na baba na mama kunakupa uhalali usio na shaka wa kurithi mali walizonazo unakosea, lipo takwa la kisheria linalokuondolea haki hiyo, ingawa mwenye mali ni baba au mama yako wa damu.
Pengine huu unaweza kuwa ukweli mchungu kwa baadhi ya warithi, kutokana na uhalisia wa matukio kadhaa ya ugomvi wa mali za urithi yanayozikabili familia mbalimbali na wengine wanafikia hatua ya kukatizana uhai.
Mfano wa hayo ni familia ya Bwire Mathayo wa Kibaha mkoani Pwani, iliyoingia kwenye mzozo wa miradi baada ya mama yao kufariki na kuacha mali.
Mzozo huo umetokana na wakubwa kugoma kuwaingiza wadogo zao kwenye mirathi, wakidai hawastahili kwa kuwa mali hizo zilichumwa na baba yao.
Kaka katika familia hiyo, Justine Zuberi alidai baba aliyefariki, ndiye mmiliki wa mali hizo na si baba yao wa kambo (Bwire Mathayo) aliyemuoa mama yao na kumkuta na mali alizoachiwa na baba yao.
Mama yao huyo alifariki dunia Desemba mwaka jana na kuacha watoto wanne lakini kwa baba wawili tofauti.
Binti mdogo, Sabrina Mathayo anasema mgogoro huo umeigawa kwenye familia, haina maelewano, baadhi ya wanandugu wanaamini watoto wote wana haki ya kupata urithi kwa mama yao kwani wote ni watoto wa marehemu na wengine wanapinga.
Mkasa mwingine unaikabili familia mjini Morogoro, baada ya baba kufariki mmoja wa watoto wake aliingia kwenye mgogoro na wenzake akipinga kuenguliwa kwenye mirathi.
Kijana huyo Deniss Joachim (sio jina lake halisi) anataka kuwa mmoja wa warithi, ndugu zake wanagoma wakisisitiza baba yao akiwa hai alimuengua kwenye warithi wake na wosia aliouacha umebainisha hilo.
Kama hiyo haitoshi, Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka alieleza mgogoro wa mirathi wa watoto wa familia moja mkoani humo ambao walikwenda ofisini kwake kutaka usuluhishi.
Katika mgogoro huo, watoto wadogo watatu walipinga wakubwa zao wawili kuwa wasimamizi wa mirathi, wakitoa hoja kwamba ndugu zao hawakutaka baba yao apelekwe hospitali alipokuwa anaumwa, iweje afariki ndiyo wawe wasiwamizi wa mirathi yake.
Katika simulizi hiyo, Mtaka alisema wale wadogo walipoulizwa kwanini hawataki, kaka zao wasimamie mirathi, wakasema baba yao alipata kiharusi, waliposhauri apelekwe Muhimbili (Hospital ya rufaa ya Taifa, Dar es Salaam), wale wakubwa walikataa wakidai mzazi wao huyo anaweza kufa muda wowote.
“Alikaa kwenye ari ya ugonjwa mwaka mmoja na miezi minne na kufariki, mvutano ulikuwa wadogo hawataki kaka zao kuwa wasimamizi wa mirathi, wakitoa hoja kwamba ndugu zao walikataa baba yao asipelekwe Muhimbili kwa matibabu zaidi wakati pesa ambazo zingetumika zilikuwa na zake, wakidai walitaka afe ili wagawane fedha za baba yao zikiwa nyingi.
“Wakubwa nilipowauliza wakasema mzee wao alikuwa amefikia kwenye koma, hivyo huenda angefia njiani, lakini swali la kujiuliza hata kama wangechukua ambulance wakalipa milioni 80, hela ni ya mgonjwa mwenyewe,” alisema Mtaka.
Ufafanuzi wa kisheria
Akizungumzia sintofahamu hiyo, Ofisa Usajili wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita) Joseph Mwakatobe anasema kuna vigezo vinavyomuondoa mtoto kwenye mirathi iwe baba/mama yake aliacha wosia au la.
“Kwa aliyeacha wosia, mwenye mali anaweza asimrithishe mtoto wake, lakini ni lazima amtaje kuwa ni miongoni mwa watoto wake na sababu za kutomuweka kwenye orodha ya warithi wake na ziwe na ushahidi,” anasema.
Kwa ambaye hakuacha wosia, anasema lazima kuwepo na mashahidi wasiopungua wanne kuthibitisha hilo kuwa mtoto husika hastahili kurithi na Mahakama itaviangalia kama vya msingi.
Kinachomuondolea mtoto uhalali wa kurithi
Pamoja na sababu nyingine, hatua ya kuzini na mke au mume na muandika wosia ni moja ya vigezo vinavyomwondolea mtoto haki ya kurithi.
“Hilo likithibitika, linamuondoa mtoto huyo katika haki hiyo kwa kuwa ni mkosefu wa maadili,” anasema.
Kama wewe ni mtoto na unaharibu mali za mzazi wako, hesabu hiyo ni moja ya sababu zinazokuondolea sifa ya kurithi kwa mujibu wa Mwakatobe.
“Mali aliyoharibu ndiyo itahesabika kuwa ni urithi wake, mzazi akiandika au hata kutamka na ndugu jamaa wakawa wanafahamu, hiyo ni moja ya vigezo vinavyomuondoa huyo mtoto katika mirathi,” anasema.
Lakini, ukishindwa kutoa huduma kwa mzazi wao angali hai, anasema ni sababu nyingine inayokuondolea sifa ya kumrithi.
“Ni kweli huyo mwanao ni mrithi wako, lakini hakukujali labda wakati unaumwa, hiyo inapelekea dhana kwamba pengine anataka ufe ili arithi, na baadhi ya mifano ipo watoto wengine huwaombea mabaya wazazi wao ili tu warithi mali, kigezo hicho kikiwa na ushahidi kinakuondoa kwenye mirithi,” anasema.
Lakini, anasema mtoto anaweza kupinga Mahakamani kama mzazi ameacha wosia na Mahakama itaangalia kama vigezo vilizingatiwa.
Mama mwenye watoto wa baba tofauti
Akifafanua mirathi ya watoto waliochangia mama, Mwakatobe anasema kama mume wa kwanza wa mama huyo alipofariki ulifanyika mgao na kila mmoja (mke na watoto), mama huyo akifariki watoto na mume wake mpya atakuwa na haki ya kumrithi.
“Kama mgao ulifanyika mume wake wa kwanza alipofariki, inamaanisha watoto wakubwa tayari walishapata mgao wao, na kama haukufanyika mali zote zikaenda kwa mama hiyo ni utaratibu anapaswa kufanya mgao bila kuangalia alizaa na nani.
“Mwakatobe anasema kuna migogoro watoto wakubwa wanadai mali alichuma baba yao, lakini kama mali hizo ziligawanywa baba wa kwanza alipofariki, kisha baadae mama akaolewa na kuzaa, ikitokea huyo mama amefariki wote ni uzao wa tumbo lake na kila mtoto anastahili kurithi na hata huyo mume aliyekuwa amemuoa naye anastahili,” anasema.
Anasema huyo mama akiwa na hekima atawaweka wazi mapema kuhusu mali zake na kueleza hizo mali alichuma na baba gani na warithi wake ni watoto wake na wale wa baba mwingine ataangalia baba yao na mali zao.
“Kama hakufanya hivyo, hakuacha wosia na hakuna maandishi na nyaraka, basi vyote vinakwenda kwa wale warithi wake hata mume aliyekuwa amemuoa anaweza kurithi, kwani anapofariki mwenye mali zake, mali zitangukia kwa warithi wake,” anasema.
Wajukuu wanaweza kurithi?
Mwakatobe anasema katika sheria wanaopaswa kurithi ni wale walioachwa na marehemu, mke, mume, wazazi au watoto.
"Kama watoto wa huyo marehemu walitangulia kabla ya baba yao, lakini nao wameacha watoto (wajukuu wa marehemu) hao hawana nafasi labda kama awe aliacha wosia na kuwaandika kwenye mirathi.
"Kinyume na hapo, hao wajukuu tunasema baba au mama yao alikimbia urithi, kwa sababu walifariki kabla ya mwenye mali, na ikitokea wamepata basi ni busara tu inatumika kwenye familia,” anasema.
Unavyoweza kuandika Wosia
Mwakatobe anasema, ili kuandika wosia unakwenda Rita kwanza ukiwa peke yako.
"Haihitaji kitu kingine zaidi ya kuja wewe kama wewe, tutakuelekeza, utaandika mali zako na sisu tutakupangia tarehe ambayo utakuja na mashahidi wawili ili kuandika wosia," anasema.
Hata hivyo, Mwakatobe anasema kitu cha muhimu ambacho watu wanapaswa kukifahamu ni kwamba kuandika wosia inaweza isiwe kigezo cha usimamizi wa mirathi yako pale unapokuwa umefariki endapo wosia utakosa vigezo.
"Hii imekua ikileta shida, unaweza kujiuliza inakuwaje Mahakama imekataa wosia na marehemu aliuandika akiwa hai? ndiyo anaweza kuwa ameandika lakini haujakidhi vigezo, sisi Rita kabla ya kuandika tunakupa elimu kwanza," anasema.
Anasema kwenye wosia mbali na mali, unaandika pia madeni na lazima uwaorodheshe watoto wako na kama miongoni mwao yupo ambaye humpi urithi na ueleze sababu na umtaje msimamizi wa mirathi.
"Unapokuja kuandika wosia uthibitisho wa mali zako unao mwenyewe, Rita tunachohitaji ni taarifa na taarifa yako anakua nayo kichwani, kama una vitu vingi, tunakwambia kaa tulia andika summary ya vitu vyako.
"Wosia unaweza kukosa vigezo, kama muandikaji ameandika si kwa hiari yake, kwani kuna watoto huwa wanazimisha baba aandike kisa labda kaoa mke mwingine halafu wanaona hizo mali zilichumwa na mama yao," alieleza.
Anasema kigezo cha kwanza katika kuandika wosia lazima uwe na hiari nao, pili ni utimilifu wa akili ukijua kile unachoandika na unakikumbuka.
"Pia uwe na mashahidi wasiopungua wawili na lazima uchapwe, usifutwe futwe na kilichoandikwa kisilete utata na usainiwe na muandikaji na mashahidi siku moja na uthibitishwe,” anasema.
Anasema kwenye wosia shahidi anaweza kufariki kabla ya mwenye mali, hivyo wosia unaweza kubadilika mara kwa mara kulingana na uhitaji uliopo.
Kwa mujibu wa Mwakatobe, gharama za kuandika wosia zinaanzia Sh30,000 na kuuhifadhi ni Sh30,000 kwa mali isiyozidi Sh50 milioni.
Kuanzia mali za Sh50 milioni hadi Sh500 milioni kuandika ni Sh100,000 na kuuhifadhi ni Sh100,000.
Na kwa mali ya kuanzia Sh500 milioni na zaidi kuandika ni Sh150,000 na kuuhifadhi ni Sh150,000.
"Mali hizo huwa tunazifanyia makadirio na kutathimini kulingana na mazingira," anasema.
|
Baada ya kusuasua kiuendeshaji, hatimaye Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (Temesa), imebadili mfum
|
Baada ya kusuasua kiuendeshaji, hatimaye Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (Temesa), imebadili mfumo wa utendaji wake, ikitangaza kubadili mfumo wa utekelezaji wa majukumu yake, kwa kushirikiana na sekta binafsi kupitia ubia (PPP).
Kutokana na mabadiliko hayo, Temesa imewaita wawekezaji wa sekta binafsi kutoka ndani na nje ya nchi kuwasilisha mapendekezo ya ushirikiano nayo katika huduma za vivuko, karakana za ufundi magari na ufundi umeme.
Temesa inakuja na mpango huu ikiwa ni miezi mitatu tangu gazeti hili lichapishe mfululizo wa ripoti maalumu zinazoonyesha wakala huo kuhelemewa na majukumu, kuathiriwa na mifumo na hata kujikuta ikiangukia katika madeni.
Ripoti hiyo iliyotokana na uchunguzi uliofanywa kwa takriban miezi mitatu, iliweka wazi juu ya Temesa kukiuka mpango wa matengenezo ya vivuko na kudaiwa zaidi ya Sh30 bilioni na wasambazaji wa vipuli kwenye karakana zake za ufundi magari.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, ubia wa sekta ya umma na binafsi ndiyo ulioonekana kama suluhu ya changamoto zote zinazoukabili wakala huo na sasa hatimaye umeanza kulitekeleza hilo kwa kushirikiana na Kamishna wa Ubia wa Sekta ya Umma na Binafsi, David Kafulila.
Hata hivyo, pamoja na ubia huo kuwa fursa kwa sekta binafsi, wadau hao wanasema kunahitajika uhuru wa kuamua baadhi ya mambo ili kuzalisha faida kwa pande mbili.
Ushirikiano katika vivuko
Katika taarifa hiyo, Temesa imewaalika wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya kuwekeza kwenye uendeshaji wa vivuko kupitia mpango wa PPP.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mwekezaji ana fursa ya kuwekeza kwa njia ya kukodisha vivuko vyote, kuunda ubia wa pamoja au kuendesha vivuko vyake sambamba na vile vya Temesa.
Mwekezaji huyo anayeonyesha nia, anapaswa kuwasilisha nakala zilizothibitishwa za hati za kisheria za taasisi husika na muhtasari wa maelezo ya awali ya uwekezaji.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mwekezaji huyo pia anapaswa kuwasilisha maelezo ya awali ya uwekezaji, kutoa muhtasari wa mradi uliopendekezwa na uwezo wake wa kufikia ufanisi, unafuu wa kifedha na thamani.
Katika pendekezo hilo, mwekezaji anatakiwa kutuma idadi ya vivuko atakavyoendesha na idadi ya abiria na magari yatakayohudumiwa kwa mwaka.
Kwa mujibu wa Temesa katika tangazo hilo, mradi uliopitishwa utapaswa kuanza ndani ya miezi 24 kwa kusaini mkataba wa utendaji na kuwasilisha dhamana ya benki, kiasi kitakachokubaliwa kati ya Temesa na mwekezaji mtarajiwa.
Pia, taarifa hiyo inataka ulinganifu na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Tanzania 2025 na mipango ya kitaifa ya maendele.
“Thamani ya fedha kwa manufaa kwa Serikali, ikihusisha kuchochea maendeleo ya kiuchumi, kuongeza huduma, ajira na ukuaji wa uchumi, mageuzi ya teknolojia na kuongeza mapato ya taifa,” imeeleza.
Ushahidi wa uwezo wa kifedha wa wawekezaji kwa kuwasilisha ripoti za fedha zilizokaguliwa kwa miaka mitatu, uzoefu wa mwekezaji katika kutekeleza miradi kama hiyo ni vigezo vingine vilivyobainishwa.
Kadhalika, uwezo wa kuboresha na kuendesha vivuko kwa kutumia teknolojia ya kisasa, makadirio ya gharama za mitaji ya uwekezaji, faida zinazopendekezwa kulipwa kwa Temesa na faida za kijamii zinazopendekezwa kwa jamii inayozunguka mradi huo.
Karakana
Kwa upande wa karakana, Temesa imetawatangazia wawekezaji kushirikiana nayo katika uendeshaji wa karakana 13 kupitia mpango wa PPP
Limesema baada ya hatua hiyo, Temesa itachagua wawekezaji watakaokidhi vigezo vya tathmini na baadaye kuwaalika waombaji waliofanikiwa.
Tangazo hilo hilo pia limetolewa kwa sekta binafsi itakayoshirikiana nayo katika ufundi wa umeme.
Alichosema Kamishna wa PPP
Kamishna wa Ubia wa Sekta ya Umma na Binafsi, David Kafulila alisema ushirikiano huo unalenga kufanywa katika uendeshaji wa karakana 13 kati ya 30 za wakala huo, sambamba na majukumu mengine kama vivuko na ufundi.
Kwa upande wa magari Kamishna huyo alisema karakana hizo 13 zipo katika mikoa ya Katavi, Rukwa, Shinyanga, Kagera, Singida, Iringa, Mara, Manyara, Pwani, Lindi, Ruvuma, Njombe na Simiyu.
Hata hivyo, Kafulila alisema hatua hiyo ya Temesa inaakisi matakwa ya Kanuni ya 36 (b) na (d) ya Ubia kati ya sekta ya umma na binafsi ya mwaka 2020 na marekebisho yake ya mwaka 2023.
Kanuni hiyo, kwa mujibu wa Kamishna huyo, inairuhusu Temesa kuwaalika wawekezaji katika utekelezaji wa miradi yake kwa njia ya ubia.
“Mpango wa Temesa kuboresha karakana zake na kutoa huduma kwa njia ya ubia unatoa matumaini ya kukidhi mahitaji ya huduma za matengenezo kwa aina mbalimbali za magari na mitambo,” alisema.
Kwa mtazamo wa Kafulila, hatua hiyo itawezesha kuvutia teknolojia za kisasa, kuchochea ufanisi wa uendeshaji na kuboresha ubora wa huduma.
“Mageuzi makubwa yatazidi kutokea katika miradi ya ubia baada ya Kituo cha Ubia wa Sekta ya Umma na Binafsi kufikia adhma yake ya kutoa huduma zote za ubia ndani ya kituo (one-stop centre),” alieleza Kafulila.
Maoni ya wadau
Akizungumza kuhusu ushirikiano katika uendeshaji wa vivuko, mmoja wa maofisa wa ngazi ya juu kutoka moja ya kampuni binafsi zinazoendesha huduma za vivuko nchini (jina lake limehifadhiwa), alisema hiyo ni fursa kwa upande mmoja lakini inahitaji maelewano kwa upande mwingine.
Kwa upande wa fursa, alieleza kwa sababu kuna mahitaji makubwa ya abiria kutumia usafiri huo, bila shaka ni biashara nzuri na yenye faida.
Lakini, fursa hiyo alisema haitakuwa kama inavyotarajiwa iwapo Temesa haitatoa uhuru kwa mwekezaji huyo kutoka sekta binafsi wa kupanga baadhi ya mambo kwa maslahi ya pande zote.
Miongoni mwa mambo hayo, alitaja ni nauli kwa abiria, utaratibu wa uendeshaji, mbinu za ukusanyaji nauli na hata mageuzi ya huduma kwa ujumla wake.
“Kiufupi isiwe huduma iwe biashara, sekta binafsi inatafuta faida, wenzetu serikali wanahudumia. Kama wanataka ubia wakubali kukaa pembeni washuhudie biashara ikifanyika wabaki kusimamia ili wachungulie mapato,” alisisitiza.
Mkuu wa Idara ya Usafirishaji na Biashara wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji, Dk Prosper Nyaki alieleza ushirikiano huo utawezekana iwapo Serikali itaendelea kukusanya nauli na kumlipa mwekezaji kulingana na gharama zake za uendeshaji.
Ikitoa ruhusa kwa mwekezaji kukusanya, alisema itakuwa vigumu kuilipa Serikali kwa kuwa inaonekana gharama za uendeshaji wa vivuko ni kubwa ukilinganisha na nauli inayotozwa.
“Kwa nauli sekta binafsi haitaweza kulipa labda Serikali ije na mbinu ya mwekezaji atoe huduma na Serikali iwe inawalipa,” alieleza.
Hata hivyo, mwanazuoni huyo alisema kwa kawaida usafiri wa umma huwa ni huduma na sio biashara na unapoishirikisha sekta binafsi unalenga kupata faida.
“Napata shida kujua itawezekanaje ukizingatia nauli wanayolipa abiria hailingani na gharama halisi za uendeshaji wa vivuko, sijui mwekezaji atapataje faida,” alisema.
Lakini, alisema ushirikiano utakuwa na tija iwapo mwekezaji huyo ataamua kuja na vivuko vyake.
Kuhusu karakana, Mtaalamu wa Ufundi, Salim Msami alisema itakuwa vema kwa sekta binafsi kuunda ubia na Temesa kwa kuwa wadau hao binafsi watajihakikishia upatikanaji wa soko.
“Serikali ina magari mengi kwa hiyo ukishirikiana nao moja kwa moja unakuwa na uhakika wa wateja,” alisema Msami ambaye pia ni ofisa katika kampuni binafsi ya Hyundai.
Ili ushirikiano huo uwezekane, alisema kunahitajika kuwepo na sharti la wadau wote wawili kuwa sehemu ya uongozi na mgawanyo wa majukumu na mapato ueleweke vema.
Alisisitiza sekta binafsi imejikita katika faida zaidi na sio kutoa huduma, ili Temesa ishirikiane nayo vema inahitaji kubadili mfumo wa utendaji wake na kuweka wazi makubaliano ya uendeshaji wa karakana hizo.
Kwa mujibu wa Msami, kunahitajika uhuru wa uendeshaji wa karakana hizo kwa sekta binafsi iwapo itapewa kazi hiyo.
|
Katika jitihada za kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya tabianchi na gharama za uzalishaji wa
|
Katika jitihada za kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya tabianchi na gharama za uzalishaji wa kilimo, matumizi ya nishati ya umeme jua hasa kwenye umwagiliaji yanatazamwa kama suluhisho.
Teknolojia hiyo sio tu inapunguza gharama za kilimo, bali inachangia kuongeza uzalishaji wa mazao, hasa katika maeneo yenye ukame na upatikanaji mdogo wa maji.
Pamoja na uhalisia huo, matumizi ya nishati ya umeme jua katika kilimo cha umwagiliaji nchini, bado hayaridhishi kama inavyoonyeshwa katika utafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Maendeleo ya Kilimo Tanzania (Tari) mwaka 2020.
Kwa mujibu wa Tari, kwa mwaka huo takriban asilimia 85 ya wakulima wanaotumia mifumo ya umwagiliaji wanategemea pampu zinazotumia dizeli.
Takwimu za Tari, zinaakisi matokeo ya ripoti ya Benki ya Dunia ya mwaka 2021, iliyoonyesha wakulima wengi wadogo nchini wanaendelea kutumia pampu za dizeli kutokana na gharama ndogo za awali za ununuzi wake, ingawa gharama za uendeshaji kwa muda mrefu huwa kubwa zaidi.
Mwaka mmoja baadaye 2022, Benki ya Dunia ilitoa ripoti yake ikionyesha wakulima wanaotumia nishati ya umeme jua katika umwagiliaji ni asilimia 15 pekee nchini.
Ingawa hali iko hivyo, matokeo ya tafiti na ushuhuda wa wakulima unaonyesha matumizi ya nishati ya umeme jua katika kilimo cha umwagiliaji yana tija zaidi kuliko nishati nyingine.
Tija ya umeme jua kwenye umwagiliaji
Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) mwaka 2021, liliweka wazi kuwa kwa kutumia pampu za umeme jua, wakulima wanaweza kupunguza gharama za nishati kwa asilimia 70 hadi 90.
Shirika hilo, kupitia mradi wake wa kilimo cha umwagiliaji wa pampu za umeme jua kwa kilimo endelevu, uliofanywa mkoani Dodoma, ulionyesha wakulima walipunguza gharama za nishati kwa asilimia 80 baada ya kubadili matumizi ya dizeli kwenda kwenye umeme wa jua.
Katika hatua nyingine, Ripoti ya Benki ya Dunia kuhusu nishati mbadala ya mwaka 2022, inakadiria matumizi ya umeme jua kwenye kilimo cha umwagiliaji yanaweza kuongeza uzalishaji wa mazao kwa wastani wa asilimia 30 hadi 50.
Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) nalo linaonyesha matumizi ya nishati ya jua katika kilimo cha umwagiliaji yameongeza uwezo wa wakulima kukabiliana na majanga ya hali ya hewa kwa kuboresha upatikanaji wa maji.
Unafuu wa gharama
Kwa mujibu wa Chama cha Nishati Jadidifu Tanzania (Tarea), mkulima atagharimika Sh3.81 milioni kwa mwaka, kumiliki jenereta linalotumia mafuta kwa ajili ya umwagiliaji katika shughuli za kilimo na litadumu kwa miaka mitatu.
Lakini kwa mtambo wa umeme jua kwa ajili ya umwagiliaji, unagharimu Sh10 milioni, ambao kiuhalisia unadumu kwa miaka 20.
Tarea inaeleza licha ya gharama kubwa za mwanzo katika usimikaji wa mtambo wa nishati ya umeme jua katika kilimo cha umwagiliaji, kuna unafuu mkubwa baadaye.
Unafuu huo kwa mujibu wa Tarea, unatokana na muda mrefu ambao mtambo wa nishati ya umeme jua unadumu, kadhalika hauhusishi gharama yoyote ya uendeshaji, wakati jenereta linahitaji mafuta kila siku.
Chama hicho kimekwenda mbali zaidi na kueleza, jenereta linalotumia mafuta katika shughuli za kilimo cha umwagiliaji linazalisha kilo 487 za hewa ya ukaa, ambayo ni hatari kwa mazingira kila siku.
Ushuhuda wa mkulima
Mbali na tathmini ya Tarea, Anthony Machai mkulima anayetumia nishati hiyo mkoani Dodoma, anasisitiza unafuu wa nishati hiyo katika kilimo, ukilinganisha na mtambo unaotumia mafuta.
Kwa mujibu wa Machai, katika shamba la ekari tatu kwa jenereta utalazimika kununua mafuta ya Sh50,000 kila siku kuwezesha kuvuta maji kutoka kisimani hadi kwenye mazao kwa ajili ya umwagiliaji.
Gharama hizo, anasema kwa mwezi ni sawa na kutumia Sh1.5 milioni, kiasi ambacho ni maumivu kwa mkulima.
Lakini unapotumia mitambo ya umeme jua, anasema gharama ni kuifunga tu, baada ya hapo mkulima hatagharimika na chochote.
“Pamoja na mazingira hayo, ni wakulima wachache ndiyo tunaotumia nishati ya umeme jua kwenye kilimo, wengi wanaona afadhali watumie majenereta na mafuta,” anaeleza.
Kinachochochea wakulima wengi wachague majenereta licha ya faida ndogo wanayopata ni kile kilichoelezwa na Machai kuwa, hawana uwezo wa kufunga mitambo ya umeme jua.
Machai anasema mtambo wa umeme jua unaomudu huduma za shamba la ekari nne hadi tano, unagharimu Sh9 hadi 15 milioni.
Anasema ni wakulima wachache wenye uwezo wa kuwa na viwango hicho cha fedha kwa mara moja, ndiyo maana wanachagua kuingia gharama kidogokidogo kwenye mafuta.
“Ni kweli ukifunga mtambo kwa gharama hizo hautahitajika kutoa gharama nyingine yoyote, lakini ni wakulima wachache wenye uwezo wa kupata kiasi hicho cha fedha kwa mkupuo wafunge nishati hiyo,” anasema.
Kinachopaswa kufanywa, anasema ni Serikali iangalie utaratibu wa kuwawezesha wakulima kukopeshwa mitambo hiyo ili wawe wanalipa kidogo kidogo hadi watakapomaliza
Kwa sababu anasema gharama za mitambo huo, zinarudishwa kwa awamu moja ya kilimo.
“Mimi mwaka huu nimelima ekari moja ya nyanya kwa kutumia solar nimeingiza Sh12 milioni, kwa hiyo ni msimu mmoja unakuwezesha kurudisha gharama za mtambo lakini si kila mkulima ana uwezo wa kupata fedha ya kununua mtambo kwa mara moja, wakopeshwe,” anaeleza.
Gharama kubwa za mtambo anasema zinasababishwa na kodi zilizopo katika uingizaji wa bidhaa hizo nchini.
Anapendekeza kuwepo msamaha wa kikodi katika uingizaji wa bidhaa za sola nchini ili kuwarahisishia wakulima na kuendana na mpango wa Serikali wa matumizi ya nishati safi.
Mikakati ya Serikali
Akizungumzia hilo, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa anasema kinachofanywa na mamlaka hiyo ni kutoa elimu kwa wakulima kutumia nishati ya umeme jua katika shughuli za umwagiliaji.
Sambamba na hilo, anasema mamlaka hiyo imeshaanza mkakati wa matumizi ya nishati hiyo kwa kupendekeza nishati ya umeme jua.
Kwa hatua za awali, anaeleza wameanza kuingiza visima 60 kati ya 1,000 mwaka huu vitakavyotumia nishati ya umeme jua katika umwagiliaji.
“Tumeanza na visima 60 kati ya 1,000 mwaka huu. Tumeyabainisha maeneo tutakayoanza nayo lakini kuna uwezekano wa visima hivyo kuongezeka zaidi,” anasema.
Anasema tayari kazi hiyo imeshaanza na kwamba anaamini itakwenda kukamilika.
|
Rais Samia Suluhu Hassan ameyajibu matamko ya balozi zinazoyawakilisha mataifa mbalimbali nchini, ya
|
Rais Samia Suluhu Hassan ameyajibu matamko ya balozi zinazoyawakilisha mataifa mbalimbali nchini, yaliyotaka uchunguzi wa haraka wa matukio ya utekaji na mauaji ya watu, akisema Tanzania ni nchi huru haipaswi kuelekezwa cha kufanya kwenye mambo yake.
Katika majibu yake hayo, amewashutumu mabalozi hao akisema walichokitamka haamini kama ni maelekezo ya wakuu wa nchi zao, huku akiahidi kuwachongea kwa marais wa mataifa husika kwa kuiingilia Tanzania.
Chimbuko la majibu ya mkuu huyo wa nchi ni tamko la pamoja la balozi za mataifa 15 yanayowakilisha Umoja wa Ulaya (EU) nchini, yakilaani na kutaka uchunguzi wa haraka na huru wa matukio ya mauaji.
Balozi zilizotoa tamko hilo la pamoja ni Ubelgiji, Uingereza, Canada, Denmark, Ufaransa, Finland, Ujerumani, Ireland, Italia, Uholanzi, Norway, Poland, Hispania, Sweeden na Uswisi.
Katika tamko hilo, balozi hizo zilisema; “Tunakaribisha wito wa Rais wa kuanzisha uchunguzi wa haraka ili kubaini wahalifu waliohusika na kuhakikisha kuna uwajibikaji.”
Kadhalika wametaka ulinzi wa upinzani, ili kuakisi falsafa ya R4 ya Rais Samia na kusisitiza; “Tunatambua kwa wasiwasi mkubwa kwamba matukio haya ya hivi karibuni yanatishia misingi ya kidemokrasia na haki za wananchi wa Tanzania.
Hata hivyo, mabalozi hao walitoa tamko hilo, muda mchache baada ya taarifa ya kifo cha kada wa Chadema, Ali Kibao aliyechukuliwa akiwa katika usafiri wa umma Septemba 6, mwaka huu na siku moja baadaye amekutwa ameuawa.
Rais Samia aliyasema hayo mkoani Moshi jana, alipohutubia hafla ya kufunga mafunzo ya Maofisa wa Jeshi la Polisi yaliyofanyika kuadhimisha miaka 60 ya jeshi hilo katika Chuo cha Polisi.
“Hatupo hapa kuelekezwa nini cha kufanya ndani ya nchi yetu, tuna Katiba sheria, miongozo, mila na desturi zetu zinazotuongoza nini cha kufanya kwenye nchi zetu,” alisema.
Rais Samia alisema ameapa kuilinda na kuitetea nchi na kwamba atafanya kila linalowezekana kuimarisha ulinzi wa maisha na uhai wa watanzania kwa kuwa ni jukumu lake.
Katika wajibu huo, alisema hahitaji kuelekezwa na mtu yeyote cha kufanya kwa sababu Katiba ya Tanzania ina maelekezo ya jinsi ya kuendesha Serikali.
“Wengine wanapotaka kuonyesha huruma yao basi tunawasihi wafanye hivyo kwa kufuata makubaliano ya mahusiano kidiplomasia ya kimataifa kama ilivyoelezwa kwenye Vienna Convention on Diplomatic Relation la 1961.
“Lile tamko lililotoka na kuambiwa tufanye moja mbili tatu, sisi tunajua cha kufanya kama Tanzania kama nchi yetu. Na ni imani yangu kwamba tamko lile lililotolewa si maelekezo ya wakuu wa nchi huko walikotoka,” alisema.
Kwa sababu ana namna ya kujua, mkuu huyo wa nchi alisema atawasiliana na wakuu wenzake wa nchi za balozi hizo kujua iwapo tamko hilo ni maelekezo yao na kama sivyo atawasilisha malalamiko yake.
Katika maelekezo yake hayo, alisema mauaji yanatokea katika kila nchi, lakini Tanzania haikuwahi kuwatuma mabalozi wake wakaelekeze nchi hizo cha kufanya.
Atoa onyo
Katika hotuba yake hiyo, alisema ingawa Serikali yake inaongozwa kwa falsafa ya R4, haimaanishi kuruhusu uvunjwaji wa sheria, mila, desturi na kuruhusu utovu wa nidhamu.
“Hatutavumilia vitendo vyovyote vya kuleta machafuko na mifarakano nchini. Sasa ni vizuri tusisahau au wale wanaojiandaa na machafuko wasisahau mapito waliyopita. Ni falsafa hii hii ndiyo imewapa ruhusa ya kurudi nchini, tukafumbia macho mengine yote, sasa kama wameshaota mikia sasa sheria zile zile bado zipo.
Alieleza Serikali imefanya juhudi za kurudisha uhuru wa vyama vya siasa, vyombo vya habari, waliokuwa jela walitolewa na waliokuwa na jinai zilifumbiwa macho kwa lengo la kuwa pamoja kujenga nchi.
Alieleza inakuwa mbaya watu hao hao wanasimama kutoa kauli zinazoirudisha nyuma nchi, akisisitiza atailinda amani ya nchi kwa gharama yoyote.
“Ukimya wangu sio ujinga na wala kuzungumza sana sio werevu hata kidogo, kuzungumza sana ni udebetupu tu haliachi kuvuma lazima litavuma.
“Na anayenyamaza kimya si mjinga ni mtu anayetafakari mambo si mjinga. Kwa hiyo ukimya wangu sio ujinga na kuropoka kwao sio werevu,” alieleza.
Kwa kuwa aliapa kuilinda na kutetea Katiba, alisema hatakuwa na muhali kwa atakayetaka kuivuruga amani.
“Tumevumiliana sana kwa mambo mengi, lakini kwenye kulinda tunu ya amani na utulivu nieleze, sitakuwa na muhari kwa yeyote atakayejikaribisha katika mambo haya, anayeratibui, anayeshiriki na hata anayetekeleza mipango hiyo miovu,” alisema.
Mauaji ya Kibao
Mkuu huyo wa nchi, pamoja na kueleza kuhuzunishwa na kulaani tukio la kifo cha Kibao, lakini ameshangazwa namna wananchi walivyoponyesha hisia kali ilhali kwenye mauaji ambayo aghalabu hutokea yakiwemo ya albino hawaonyeshi hali hiyo.
“Katika hali ya kushangaza kifo hicho kimeleta hisia kali pia kwa wawakilishi wa baadhi ya mataifa ya nje wanaoiwakilisha nchi zao hapa kwetu. Nataka niungane nao na niseme kwamba kwa sababu yoyote ile mauaji haya hayakubaliki,” alisema.
Kutokana na hali hiyo, alisema ndiyo maana Serikali ililaani na kutaka vyombo vya uchunguzi vifanye uchunguzi kama inavyofanyika katika mataifa yote duniani.
“Lakini kuna vifo vinasemwa muda baada ya muda, watoto maalbino wanakatwa mikono, watoto wadogo wanauliwa wanakatwa sehemu nyeti wanatupwa sijui huyu kamuua huyu.
“Hadi leo asubuhi IGP (Camilius Wambura) kanipa ripoti huko Dodoma watu watatu wameuliwa lakini yanapotokea haya yanatokea kwenye maeneo yetu lakini kimya mpaka polisi iibuke iseme wengine hawasemi.
“Lakini inashangaza kifo cha ndugu yetu Kibao kimeibua wimbi kubwa kulaani, kusikitika, kulaumu, kuita Serikali ya wauaji hii si sawa, kifo ni kifo. Tunachopaswa kufanya Watanzajia wote tukemmeane tusimame imara kukemea mambo haya,” alisema.
Wavunjifu wa amani
Katika hotuba yake hiyo, alisema alisikiliza sauti za wanasiasa mbalimbali wote wakitoa taswira ya mipango ya uvunjifu wa amani inayopangwa na baadhi ya vyama vya siasa.
“Nayaunganisha haya na kikao cha Septemba 11, mwaka huu kilichofanywa na chama kimoja cha siasa kule Nguleli mkoani Arusha. Kikao ambacho kimeazimia kuwatumia na kuwachochea vijana kwa kuzusha tuhuma dhidi ya jeshi la polisi, kufanya siasa chonganishi kwenye misiba na kushusha molari kwa jeshi la polisi ili washindwe kufanya kazi yao ya kulinda usalama wa raia na mali zao,” alisema.
Alieleza kwa sababu ya ukubwa wa intelejensia ya nchi, ndiyo maana imewezekana kupata taarifa za kikao hicho, akisisitiza naye anayo.
“Kwa hiyo nataka niwaambie vikao vyote vinavyokwenda kupanga uovu huu, uovu tutaupata. Kumepangwa sijui kushusha moto mpaka Samia aseme sijui basi nime-surrender naondoka, hiyo Serikali Serikali ya samaki?” alihoji.
Matukio mengine aliyoyazungumzia, ni mauaji yanayohusisha upigaji ramli na vuguvugu la uchaguzi, akisema yanapaswa yakome.
“Wananchi wanakata tamaa kuona matukio haya yanahusishwa sio tu na waganga wa kienyeji bali hata watu mashuhuri kama viongozi wa dini na hata wazazi na watoto.
“Lakini yanapotokea kule chini jamii ipo kimya kama Tanzania haitokei kitu, lakini vyombo vya ulinzi wakiibua ndiyo sasa watu wanaibuka eeeyeye yeye… lakini kabla ya kuibuka hakuna anayelaani,” alisema.
Mafunzo kwa askari
Alisema askari wanatakiwa kupatiwa mafunzo kazini, ndani na nje ya nchi, huku akisisitiza nchi nyingine ziongezwe ili wakajifunze wenzao wanavyofanya.
Sambamba na hayo alitaka mafunzo ya ndani pia yaendelee, akisisitiza mabadiliko ya fikra yanategemea mafunzo ya mara kwa mara.
Hata hivyo, alieleza bado kuna changamoto katika utendaji wa jeshi hilo na kwamba Tume ya Haki Jinai imeshapendekeza namna ya kufanyia kazi.
Mambo mengine aliyozungumzia ni ajali za barabarani akisema zinasababisha vifo vya wananchi wengi na kwamba zinapaswa kudhibitiwa.
Kadhalika, alilitaka jeshi hilo kuendana na teknolojia za sasa ili kudhibiti uhalifu wa mtandaoni hasa kuelekea chaguzi na wizi kwa njia ya mtandao.
“Miongoni mwa uhalifu unaongezeka kwa kasi ni kutoa taarifa za uzushi na uongo na kutuma picha za utupu na unyanyasaji. Kutokana na kukua kwa teknolojia ya akili bandia taarifa za uzushi zinatarajiwa kuongezeka,” alisema.
“Hatusemi tufungie mitandao ya kijamii au tuwafunge midomo wananchi kuto maoni yao, lakini haijuzu kufumbia macho uhalifu unaofanywa kwenye mitandao ya kijamii. Uhalifu ni uhalifu.
“Kama ambavyo mhalifu angekamatwa kufanya uhalifu nje ya mitandao ya kijamii, vivyo hivyo afanywe yule atakayefanya hivyo kupitia mitandao ya kijamii,” alisema.
Kadhalika, mkuu huyo wa nchi alisisitiza kuongezwa uwezo na ujuzi wa kuwabaini wahalifu wanaotumia majina bandia au anga la nje ya Tanzania.
Kuhusu utapeli, alitaka liangaziwe kwa karibu zaidi kwani kwa kadri wananchi wanavyohamasika kufanya miamala kwa njia ya mtandao na ndivyo wahalifu nao wanavyobuni mbinu za kuiba.
Kwa kuwa mwelekeo wa Serikali ni kuongeza matumizi ya fedha kidigitali, alisema ni vema jeshi hilo kuhakikisha linaimarisha mbinu za kudhibiti uhalifui huo.
Alilitaka jeshi hilo, liwasilishe mkakati na bajeti ya kukabili uhalifu wa mtandao ili Serikali ione namna itakavyowezesha kukomesha hilo.
Kuelekea uchaguzi, alisema ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha nchi inabaki kuwa moja na salama kwa kuwa uchaguzi utapita na taifa litabaki.
“Jeshi la polisi liwe macho katika kipindi chote cha kabla, wakati na baada ya uchaguzi. Jeshi la Polisi lihakikishe yeyote anayejaribu kuhatarisha amani ya nchi yetu kwa kisingizio cha chaguzi hizo anachukuliwa hatua haraka na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria,” alisema.
Rais Samia alisema jeshi la polisi halipaswi kuhusishwa au kuhisiwa kuhusika na ukiukwaji wa sheria na haki inazozisimamia.
“Nilikuwa naona leo kuna clip kule Mwanza, kuna mhalifu kakamatwa polisi wanataka kuondoka naye, raia wamezuia gari wanasema haliondoki mpaka OCS aje ndiyo aondoke na huyu mtuhumiwa sasa hiyo ifanyieni kazi vizuri,” alisema.
Alilitaka lisimamie maadili ya askari ili jeshi litoe huduma stahiki na kuongeza imani ya wananchi kwa chombo hicho.
Alitaka kasi ya kuikumbatia Tehama katika jeshi hilo iwe kubwa na anasubiri bajeti ilia one namna atakavyosaidia.
Alisisitiza askari kujengewa uwezo stahiki ili wasipitwe na teknolojia, huku akidokeza juu ya umuhimu wa mifumo kusomana.
|
Tofauti na ilivyo katika maeneo mengi, kila jina la mtaa unaounda Kata ya Kimara ni simulizi yenye h
|
Tofauti na ilivyo katika maeneo mengi, kila jina la mtaa unaounda Kata ya Kimara ni simulizi yenye historia maridhawa.
Uwepo wa viwanda, shughuli za kiuchumi na miradi mbalimbali, ndiyo msingi wa ubatizo wa majina hayo, yanayoendelea kutumika hadi sasa.
Unapotokea mjini kati Dar es Salaam, Mtaa wa Kibo ndilo lango la kuingia Kimara. Ingawa Kibo inahusishwa na Kata ya Ubungo, kwa sehemu fulani imeigusa Kimara.
Kwanini Kibo
Historia ya jina Kibo inahusishwa na Mlima wenye jina hilo, mkoani Kilimanjaro, kama inavyosimuliwa na Meya mstaafu wa Ubungo, Boniface Jacob kupitia mtandao wake wa X.
Mzee Naumu ndiye mwasisi wa jina hilo, aliyeamua kuipa jina baa yake aliyoijenga katika eneo hilo, Kibo Bar na umaarufu wake ukazaa jina la mtaa hadi sasa panaitwa Kibo kwa mujibu wa Jacob.
Kwa mujibu wa Jacob, Mazee Naumu aliamua kuiita baa yake kwa jina hilo kwa kuwa eneo hilo lilikuwa na mlima na hivyo aliufananisha na ule wa Kibo, Kilimanjaro.
Kabla ya jina hilo, Jacob anasema eneo hilo liliitwa kilima cha kwanza kwa anayetoka mjini kati na kilima cha mwisho kwa anayetokea Mbezi. Hivyo hakukuwa na jina rasmi.
Kwa bahati nzuri Kibo Bar ipo hadi sasa, lakini si kwa umaarufu kama ilivyokuwa zamani. Hata hivyo ni vigumu kuiona unapopita barabarani kwa kuwa mbele yake kuna flemu za maduka na mti ambao ni kijiwe cha madalali.
Kimara Baruti
Ukistaajabu ya Kibo, ya Kimara Baruti yatakusangaza. Asili ya jina hilo ni shughuli za uhifadhi baruti zilizokuwa zinafanywa katika eneo la kiwacha cha Saruji cha Twiga Chemical.
Baruti hizo, zilitumika kupasulia mawe yanayotumika katika kutengenezea saruji.
Katika eneo hilo pia, Jacob anasema kulikuwa na maghala ya kuhifadhi baruti na kambi kubwa ya wafanyakazi wa kiwanda cha saruji.
Haikuwawia vigumu waswahili, kushabihisha shughuli maarufu katika eneo hilo na jina la mtaa na ndilo chimbuko la Kimara Baruti.
Mwanasiasa huyo anasema kwa sasa eneo hilo imejengwa Hospitali ya Wilaya ya Ubungo na shughuli za uhifadhi baruti zilihamishwa tangu miaka ya 1990.
Kimara Bucha
Kama lilivyo jina lake, asili ya jina la mtaa huu ni bucha la nyama ya kitimoto, lililojengwa kwa nakshi za aina yake kulingana na nyakati hizo, inadaiwa miaka ya 1980, kwa mujibu wa Jacob.
Bucha hilo lililokuwa mali ya Thomas Lyimo ambaye pia alimiliki kiwanda cha maziwa cha Thom Dairy, yaliyokuwa yakigawiwa bure katika shule za msingi.
Jamaa alianza kwa kujenga banda la chuma tupu, kwa namna lilivyopambwa kila mmoja alikuwa na shauku ya kujua nini kinalengwa kuwekwa ndani yake. Hatimaye likawa duka la nyama ya nguruwe na ndiyo asili ya jina la Kimara Bucha.
Kimara Korogwe
Hili sio la muda mrefu kama yalivyo majina mengine. Liliibuka mwanzoni mwa miaka ya 1990 kama inavyosimuliwa na Jacob kupitia mtandao huo.
Kabla ya Korogwe, eneo hilo liliitwa Kimara Resort kutokana na uwepo wa kiwanja cha starehe, mithiri ya vile maarufu hapa mjini kwa sasa.
Watu wa nyakati hizo, kabla ya kwenda kwenye kumbi hiyo, walivalia suti ya kitambaa cha Asante Urafiki, lililokuwa vazi maarufu kipindi hicho.
Mbwembwe na umaarufu wa jina hilo, ulivurugwa na Msambaa aliyetoka Korogwe mkoani Tanga na kuanzia banda la chipsi, msosi pendwa kwa mabinti.
Haikuwa kawaida, kwa kuwa banda hilo lilipanga magari ya Serikali na msululu wa wananchi wakisubiri chipsi za msambaa, pengine kwa sababu ya ladha yake.
Hakuwa peke yake, kama ulivyo utamaduni wa wasambaa, alikuwa na vijana zaidi ya 100 wanaotumikia ofisi hiyo kwa kumenya viazi kukidhi mahitaji ya wateja.
Kwa mujibu wa simulizi ya Jacob, isingekuwa rahisi upite eneo hilo na una fedha mfukoni, usinunue chipi kwa namna zilivyonukia na kuvutia.
Basi bwana, jamaa akapata aidia ‘idea’ akaandika bonge la bango kwa mkono ‘KOROGWE’ kuanzia hapo jina la Resort likajifia na Korogwe likaibuka.
|
Licha ya mtazamo kuwa, kuimarika kwa usafiri wa reli ya kisasa (SGR) kutaathiri usafiri wa anga kwa
|
Licha ya mtazamo kuwa, kuimarika kwa usafiri wa reli ya kisasa (SGR) kutaathiri usafiri wa anga kwa upande mmoja, wadau wa usafiri huo, wamesema reli hiyo ya kisasa inaweza kuimarisha sekta ya anga pia.
Matumaini ya wadau hao yanatokana na mtazamo kuwa, kuna uwezekano wa vyanzo hivyo vya usafiri kushirikiana na kuwapa fursa wananchi kuchagua aina gani wanayopenda kulingana na mahitaji yao.
Hoja hizo za wadau zinakuja katika kipindi ambacho, treni za SGR zimeteka soko la sekta ya usafiri kutokana na gharama nafuu, ufanisi na ratiba za kuaminika, jambo linalovutia abiria wengi.
Katika siku za karibuni, Shirika la Reli Tanzania (TRC) liliripoti kuhudumia abiria 366,000 tangu treni hiyo ilipoanza kutoa huduma kwa njia za Dar es Salaam, Morogoro na Dodoma.
Idadi hii imezidi matarajio ya awali na makadirio yanaonesha idadi ya abiria inaweza kufikia au kuzidi milioni moja katika miezi ijayo.
Uimara na ushawishi huo wa usafiri wa njia ya reli ya kisasa, haujawa tishio kwa wadau wa usafiri wa anga, wanaoonyesha matumaini ya kuimarika pia na kuwapa abiria fursa ya kuwa na machaguo ya aina ya usafiri.
Tishio la athari katika usafiri wa anga kama matokeo ya uimara wa SGR, linathibitishwa na mmoja wa abiria aliyeomba hifadhi ya jina lake, anayesema ndege aliyopanda Jumamosi usiku kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam, kulikuwa na abiria 10 pekee.
Hilo lilimpa wasiwasi kwa kile alichoeleza, kuna uwezekano safari hizo zikapotea, kwa kuwa, kwa kawaida ni hasara kwa ndege kupakia abiria chini ya 50.
“Ingawa SGR inaweza kutoa changamoto, hasa kwa abiria wa daraja la juu ambao kwa kawaida hushika nafasi zao mapema, haipaswi kuonekana kama mbadala wa moja kwa moja wa safari za anga,” alisema.
Aliongeza kuwa mashirika ya ndege yanayohudumia maeneo kama Dodoma yanapaswa kufikiria kuratibu ratiba zao na huduma za treni ili kudumisha faida.
Wasiwasi wake unaakisi suala pana zaidi, hasa mabadiliko yanayoweza kutokea ya abiria wa daraja la juu kutoka kwenye ndege kwenda kwenye treni.
Mabadiliko haya yanaweza kuwa changamoto kwa mashirika ya ndege, hasa katika njia maarufu kama ya Dodoma-Dar es Salaam, ambapo ndege huwa zimejaa lakini sasa zinakabiliwa na ushindani kutoka kwa huduma ya treni.
“Iwapo SGR itaendelea kuwa na ufanisi wa hali ya juu, huenda kukawa na kupungua kwa safari za ndege kwenda Dodoma kwani abiria wengi watapendelea kutumia treni. Tofauti kati ya kusafiri kwa treni na ndege ni ndogo, na urahisi unaotolewa na treni za umeme unaweza kuathiri usafiri wa anga,” aliongeza.
Ingawa kwa abiria huyo ni wasiwasi, mtaalamu wa usafiri wa anga, John Njawa kwake ni matumaini, akipendekeza SGR inapaswa kuangaliwa kama nyongeza ya safari za anga badala ya kuwa mshindani wa moja kwa moja.
Hata hivyo, anasema kuanzishwa kwa SGR kunaweza kubadilisha mwamko wa abiria kwa muda, lakini haiwezekani kuathiri moja kwa moja usafiri wa anga, akisisitiza njia zote za usafiri zinaweza kuishi pamoja.
“Watu wana ladha tofauti na inahusu tabia ya wateja. Kitu kipya kinapotokea, watu wanataka kukijaribu,” alisema.
Njawa alikubali kuwa sekta ya usafiri wa anga hatimaye itaweza kuendana na kuwepo kwa SGR.
“Patakuwa na athari, hasa kwa muda mfupi, lakini hazitakuwa endelevu kwa muda mrefu. Ninaona huduma ya SGR kama nyongeza ya sekta ya usafiri wa anga badala ya mshindani wa moja kwa moja,” alisema.
Mtaalamu mwingine wa usafiri wa anga na mkufunzi, Juma Fimbo anaamini SGR ambayo bado iko katika hatua za mwanzo, haijawa changamoto kwa mashirika ya ndege.
Anaeleza huduma za reli hazina sera kamili za kushughulikia ucheleweshaji na usumbufu mwingine mdogo, maeneo ambayo mashirika ya ndege yameanzisha mikakati thabiti ya huduma kwa wateja.
“Kwa sasa hakuna ushindani halisi kati ya SGR na ndege; wako kama marafiki. Kuna uwezekano wa abiria kuchanganya safari za ndege na safari za SGR kwa usafiri wa ndani. Sekta zote mbili zinaweza kushirikiana kuboresha uzoefu wa usafiri,” alisema Fimbo.
Anaona uwezekano wa ushirikiano wa baadaye mashirika ya ndege na SGR yanaweza kuwa na huduma za pamoja za tiketi na kugawana mapato, hivyo kuzinufaisha sekta zote mbili.
Mtazamo huo, unaungwa mkono na Nahodha wa ndege, Philemon Kisamo anayesema abiria wengi kwa sasa wanapendelea SGR kwa sababu ya bei nafuu ukilinganisha na tiketi za ndege.
Mara kwa mara za safari za SGR kila siku zinatoa urahisi kwa wasafiri wa muda mfupi, kama wale wanaosafiri kibiashara.
“Ingawa mabasi yaendayo mikoani yanaweza kutoa nauli za chini zaidi, SGR ni ya kasi zaidi na abiria wanathamini uratibu wake wa muda. Ningeshauri SGR kudumisha kiwango hiki cha huduma,” alisema.
Meneja wa masoko na mawasiliano ya ushirika wa Precision Air Tanzania, Hilary Mremi anasema badala ya kuiona SGR kama tishio vema itazamwe kuwa fursa.
Anasema itazamwe kama fursa itakayoyafanya mashirika ya ndege kuboresha huduma zao; “Kwa kuboresha ubora wa usafiri wa anga, mashirika ya ndege yanaweza kuendelea kutoa sababu zinazovutia kwa abiria kuchagua ndege badala ya treni.”
“Tunaona SGR kama changamoto chanya ambayo itatusukuma kuboresha huduma zetu, na kuzifanya kuvutia zaidi kwa abiria, hasa ukizingatia muda mfupi wa safari za ndege ukilinganisha na treni,” alisema Mremi.
Aliongeza athari za SGR ni ndogo kwa sasa na idadi ya abiria bado inabadilika akitoa mfano; “Safari za ndege kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam huwa zimejaa siku za Ijumaa, na kupungua kwa abiria siku za Jumamosi si jambo geni.”
Kama sehemu ya kukabiliana na athari za SGR, Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa) kimetangaza mipango ya kuendeleza mikakati ili kuendelea kushindana, ikihusisha kuhamisha mitaji yao katika maeneo mengine ya uwekezaji.
Katibu Mkuu wa Taboa, Joseph Prisicus alibainisha chama hicho kinaangalia namna ya kukabiliana na changamoto hiyo, ikiwemo kuomba msamaha wa kikodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutokana na kupungua kwa shughuli za mabasi.
“Hatuwezi kupinga maendeleo ya reli. Kuna faida nyingi kama abiria wataishia Dodoma na kuna mabasi ambayo yatawachukua kwenda maeneo mengine. Kwa kuwa sisi sote ni walipakodi, Serikali inapaswa kuangalia jinsi ya kuwasaidia wamiliki ili wote wanufaike,” alisema.
Prisicus aliongeza Taboa inachunguza athari kwenye ajira na mitaji ya wawekezaji na inaweza kurekebisha shughuli zao kulingana na matokeo ya uchunguzi.
Kuanzishwa kwa SGR kumesababisha baadhi ya wamiliki wa mabasi kupunguza safari zao.
Kwa mfano, kampuni iliyokuwa ikifanya safari 20 kwa siku kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro sasa imepunguza hadi safari tisa au 10 kwa siku. Kupungua huku kwa huduma kuna athari kwa malipo ya kodi na uendelevu wa uendeshaji.
Kadiri SGR inavyoendelea kuimarika na kupanuka, uhusiano wake na sekta ya usafiri wa anga unaweza kubadilika.
Ingawa kuna wasiwasi kuhusu ushindani, wataalamu wanakubaliana kwamba kuna fursa ndani yake.
|
Wakati Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) na wadau wengine wakisisitiza uchunguzi huru dhidi ya m
|
Wakati Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata) na wadau wengine wakisisitiza uchunguzi huru dhidi ya matukio ya utekaji na mauaji, Serikali imesema kwanza jamii inapaswa kujiuliza kwanini matukio hayo yanatokea kila unapokaribia uchaguzi.
Katika hoja yake hiyo, Serikali imesema ni rahisi kutupa lawama kwa Jeshi la Polisi juu ya matukio hayo, huku ikieleza badala ya kufanya hivyo ni vema wananchi waanze kutafuta jawabu la kwanini yanatokea kila unapokaribia uchaguzi.
Wito wa uchunguzi ndiyo unaoonekana kubeba matamanio ya wadau wengi juu ya matukio hayo, wengine wakitaka ufanywe na tume ya kijaji, wapo wanaopendekeza mamlaka za nje ya Tanzania, kadhalika kuna lile kundi linalotaka polisi waifanye kazi hiyo.
Kila aina ya uchunguzi unaopendekezwa na wadau, unajengwa kwa msingi wa hoja, wanaotaka uchunguzi kutoka mamlaka ya nje wanadai hawana imani na vyombo vya ndani kuifanya kazi hiyo.
Lakini wale wanaotaka tume ya kijaji, wanaijengea hoja kuwa, ina uhuru zaidi wa kutekeleza jukumu hilo, hivyo watakaobainika watakuwa wahusika halisi, huku wale wanaotaka Polisi wakisema bado jeshi hilo halina udhaifu katika kuifanya kazi hiyo hivyo lipewe uhuru wa kuifanya.
Chumbuko la yote hayo ni mfululizo wa matukio ya kupotea, kutekwa na kuuawa kwa raia kulikotokea katika siku za karibuni na hivyo kuibua taharuki.
Tukio la mwisho lililoamsha hisia za wengi ni la kada wa Chadema, Ali Kibao aliyekamatwa Septemba 6, mwaka huu akiwa katika usafiri wa umma na siku moja baadaye mwili wake ukaokotwa Ununio jijini Dar es Salaam akiwa amefariki.
Hatua hiyo ilisababisha Chadema itake Serikali kuwatoa watu wote waliopotea kufikia Septemba 21 na isipofanya hivyo wataandamana kuanzia Septemba 23, katika Jiji la Dar es Salaam.
Hata hivyo, tayati Jeshi la Polisi limeshapiga marufuku juu ya maandamano hayo.
Kauli hizo za Bakwata na Serikali zimetolewa leo, Septemba 16, 2024 na Katibu Mkuu wa Baraza hilo, Nuhu Mruma na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa walipohutubia Baraza la Maulidi ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (SAW) mkoani Geita.
Msimamo wa Bakwata
Katika hotuba yake, Katibu Mkuu wa Bakwata, Nuhu Mruma amesema baraza hilo linaungana na Rais Samia Suluhu Hassan kulaani vitendo hivyo na wanavitaka vyombo vya ulinzi na usalama vifanye uchunguzi huru kubaini wale wote waliojitokeza kufanya uhalifu huo.
“Viende mbali zaidi (vyombo vya ulinzi na usalama) na kujua dhamira yao ni nini ili kutafuta ufumbuzi na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria,” amesema.
Amewasihi wanaofanya uchunguzi huo kutofanya upendeleo au kumkandamiza yeyote bali haki itendeke bila kujali itikadi za wanaofanya unyama huo.
“Tunaomba wananchi kuwa mabalozi wazuri wa kulinda na kutunza amani yetu na kutokubali kutumika na yeyote kwa maslahi binafsi katika kuvuruga amani yetu,” ameeleza.
Waziri Mkuu
Kwa upande wa Majaliwa amesema badala ya kutupa lawama kwa jeshi la polisi ni vema kujiuliza kwanini matukio hayo yanatokea kila inapokaribia uchaguzi.
Kwa mujibu wa mtendaji mkuu huyo wa Serikali, tangu awamu ya tatu hadi ya sasa ya serikali matukio kama hayo hutokea, lakini swali linabaki kuwa kwanini kila unapokaribia uchaguzi.
“Rais alitoa karipio juu ya yanayotokea matukio haya ambayo yanatokea kila kipindi fulani lazima tujiulize kwanini yanajitokeza hasa inapokaribia chaguzi nani anafanaya ni rahisi kusema polisi, lakini muhimu tukatafakari kwanini wakati huu na nani anafanya,” amesema Majaliwa.
Katika mazingira hayo, amesema mafanikio ya ulinzi wa taifa hayatfanikiwa kwa kuwategemea polisi pekee, badala yake kila mwananchi awajibike kuifanya kazi hiyo.
Ameijenga hoja yake hiyo kwa kurejea mwaka 2021, akisema kulikithiri matukio hayo mkoani Mtwara na Rais Samia aliunda tume ambayo matokeo yake ikawa ni kuundwa kwa Tume ya Haki Jinai.
Kwa sababu mkuu wa nchi ameshaelekeza, Majaliwa amesema Watanzania wanapaswa kuiamini Serikali kwa kuwa iko macho na imara.
Amesisitiza Serikali haitafumbia macho wanaochokoza taifa kwa matukio ya utekaji na mauaji, hatua kali zitachukuliwa dhidi yao, huku akiwataka wananchi waendelee kuwa na imani.
Katika nyakati hizo, amesema yeyote atakayeona viashiria vya uvunjifu wa amani katika maeneo awe mstari wa mbele kutoa taarifa, kwani kinachohitajika sasa ni ushirikiano kati ya wananchi na vyombo vya ulinzi na usalama.
Katika hatua nyingine Waziri Mkuu, amewataka wazazi na viongozi wa dini kutimiza wajibu wao katika malezi ya watoto ili taifa liwe sehemu salama.
“kila mmoja anao wajibu iwe taasisi za elimu au dini moja kati ya ajenda muhimu ni kuhamasisha Watanznaia kulea jamii katika maadili mema ili kuepuka maovu yote,” amesema Majaliwa.
Amesema viongozi wa dini wana jukumu la kuhamasisha maadili kwa jamii, huku wazazi wakiwa na wajibu wa kulea watoto kuanzia ngazi ya familia ili wawe na maadili.
Mufti wa Tanzania, Abubakar Zuber amewataka Waislamu kujenga uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa, huku wakiweka elimu mbele na kuilinda amani.
Katika hotuba yake hiyo, amesisitiza umuhimu wa maadili kwa mtu mmoja mmoja, akisema mwonekano wako unatosha kutafsiri wewe ni muadilifu kiasi gani.
“Unakut mtu mzima mwanaume anavaa bukta anazurura huku na kule anashangaa tunamcheka. Tunamcheka kwa sababu amevaa vazi lisilopaswa kuvaliwa naye,” amesema.
Sambamba na hayo, amesisitiza tabia za kujidhuru na kudhuru wengine ni kinyume na matakwa ya dini ya Kiislamu na maelekezo ya Mtume Muhammad.
Amesema yeyote anayefanya hivyo kwa mujibu wa vitabu vitakatifu anakuwa amekiuka maelekezo ya Mungu na Uislamu unamkataa.
Baadhi ya waumini wakizungumzia matukio ya utekaji nchini wamesema yanayotokea sasa ni ishara ya kuwa watu wameacha kumwamini Mungu na kuamini ushirikina.
Wamesema ni jukumu la viongozi wa dini kuendelea kutoa elimu ya dini ili watu wamrudie Mungu.
Jumapili Hussein amesema watu wamehamisha imani zao kutoka kwenye imani ya dini na kuamini ushirikina, ndio chanzo cha mauji na matukio mabaya yanayoshamiri nchini kwa sasa.
|
Hisia na mitazamo tofauti imeibuka juu ya sheria inayomtaka mama kuacha wazi eneo linalopaswa kuandi
|
Hisia na mitazamo tofauti imeibuka juu ya sheria inayomtaka mama kuacha wazi eneo linalopaswa kuandikwa jina la baba wa mtoto katika cheti cha kuzaliwa, iwapo mzazi huyo wa kiume hajulikani au kuna sababu za kutoandikwa.
Mitazamo hiyo inakuja ikiwa ni siku moja tangu Mwananchi Digital iliporipoti kuhusu takwa la mama kuacha eneo la jina la baba huyo au aandike ‘hajulikani’ badala ya kutumia ubini wa mzazi asiye asilia wa mtoto.
Msingi wa habari iliyoripotiwa na Mwananchi Digital ni maneno ya Ofisa Usajili wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita), Joseph Mwakatobe aliyesema ni vema kuacha wazi kuliko kuandika jina la baba bandia, akisisitiza ni kosa kisheria.
Wakili Kiongozi wa kampuni ya Uwakili ya Haki kwanza, Alloyce Komba ni miongoni mwa walioibukia kwenye mjadala huo, akiunga mkono kauli ya Rita kwa kueleza aliyetoa jina bandia na mwenye jina hilo wanaweza kuingia matatani kama baba asilia wa mtoto ataamua kufuata sheria.
Kwa mujibu wa Komba, sheria pia itamlinda mama, endapo ataamua kudai matunzo ya mtoto kwa baba asilia ambayo aliyatoa kwa mtoto katika kipindi chote ambacho alimlea peke yake.
"Itaandikwa baba hajulikani hadi pale wazazi watakapomaliza tofauti zao watakwenda kubadilisha au mama atumie busara kuandika ubini asilia wa baba mzazi wa mtoto tangu mwanzo hata kama hamtunzi, kisha akamshatiki kwa kutomtunza mtoto wake lakini akibainika ameandika jina tofauti na la baba mzazi ni kosa kisheria na ataingia matatani yeye (mama) na huyo baba bandia," anasema wakili Komba.
Anasema wapo watoto wengine pia anapokuwa mkubwa na kufahamu ubini anaotumia si wa baba yake asilia, anakwenda kubadilisha kwa kiapo ili kuwa na utambulisho wake sahihi.
"Hivi vitu vinafanyika sema watu huwa hawavizingatii tu, mama anapoandika ubini tofauti na wa baba mzazi, baba halisi asijue au asifuatile hilo si tatizo, lakini akijua na kwenda kushtaki Mahakama akijiridhisha ni kweli, anashinda hata kama hakuwa akimhudumia mtoto wake," anasema.
Hata ukimbadilishia mtoto ubini, Wakili Komba anasema haimuondolei baba halali uhalali wa kumchukua mwanawe atakapohitaji, sheria inamlinda.
"Suala sio huduma, baba mzazi ni yupi? mama anatakiwa amshtaki baba ambaye hatunzi mtoto mapema, sio kuamua kubadili ubini wa mtoto, hilo ni kosa kisheria,” anasema.
Anasema baba kumtunza mtoto wake ni suala la kisheria na sheria ya mtoto ya mwaka 2019 imeeleza wazi kuwa baba mzazi ana wajibu wa kutoa matunzo.
"Ikitokea hamtunzi na wewe mama umekaa kimya na ukampa ubini wa baba wa kufikia, fanya hivyo baba mzazi asijue, ikitokea amejua wewe mama na huyo baba wa kufikia wote mtakuwa matatani.
"Hata ukimpa ubini wa ujombani, bado utakuwa matatani kwani huwezi kuzaa na ndugu yako, hiyo sio sawa, kisheria baba mzazi ndiyo baba asilia anayetambulika bila kujali hamtunzi mtoto na akienda Mahakamani akamdai mtoto wake, Mahakama ikithibitisha atamchukua mtoto wake,” anasema.
Anasema baba huyo anaweza kunyimwa mtoto huyo kulingana na mazingira, Mahakama itaangalia yupo katika mazingira mazuri ya kumlea huyo mtoto au la?.
"Ikionekana mazingira ya mama yako vizuri zaidi, Mahakama ndiyo itasema kweli mtoto ni wako, lakini mazingira yako ya kumlea si rafiki hivyo ataendelea kulelewa na mama," anasema.
Wakili Komba anasema kinachozingatiwa ni maslahi ya mtoto, ambaye atapewa haki ya kuzungumza iwapo hamfahamu yule baba (mzazi) alilelewa na mama pekee au vinginevyo.
“Mashauri yoyote kuhusu mtoto kipimo kikubwa ambacho Mahakama huwa inakizingatia ni maslahi ya mtoto, kama mwisho wa siku baba mzazi atapewa mtoto, mama ana uwezo wa kudai gharama zote ambazo amezitumia kwenye matunzo na baba atazilipa ili achukue mtoto wake. lakini yote hayo hayamuondolei haki ya ubini kwa mtoto, kama ndiye baba mzazi ana haki bila kujali malezi," anasema wakili Komba.
Viongozi wa dini
Matumizi ya majina bandia ya baba si Rita pekee, hata katika Kitabu cha Quran inakataza hilo, kama inavyoelezwa na Kadhi wa mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Ramadhan Kitogo.
"Haitakiwi kumpa jina la ujombani, babu au baba wa kufikia mtoto, ikitokea baba na mama mmetengana. Quran inasema mwanamke akaichana na mumewe na ndani ya tumbo lake ana ujauzito wa mwezi mtu hawezi mjua, asifiche kile kilichomo ndani tumbo lake hata kama yule aliyekuwa amemuoa hampendi na anamchukia,” anasema.
Anasema haipaswi kumuunganisha mtoto na nasaba isiyo yake, na Mtume ametamka Mwenyezi Mungu umlaani afanyaye hivyo, Uisilamu ukielekeza watoto waitwe kwa majina ya wazazi wao.
"Kufanya kinyume ni jambo baya na tunalikemea na mwenye maadili mazuri hawezi fanya kitu kama hicho," anasema Sheikh Kitogo.
Mchungaji Daniel Sendoro wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Daniel Sendoro anasema suala la majina japo halina nguvu katika dini, lakini kuna athari pale mtu anapopewa jina tofauti na la baba yake.
"Kwa mtoto atakapokuwa mkubwa inaweza kumharibu kisaikolojia, jina ndilo limebeba utambulisho wake, kama ni Sendoro wewe ukamuita Makongoro akiwa mkubwa utamletea shida huyu mtoto na ataanza kutafuta utambulisho wake," anasema mchungaji Sendoro ambaye pia ni mwanasaikolojia.
Anasema huyo mtoto ipo siku ataambiwa baba yako sio yule, hao waliokupa hilo jina ni wajinga tu na mambo kama hayo, moja kwa moja ataanza kujiona asiyemkamilifu kwani moja ya vituvinafanya mtu kuwa mkamilifu ni utambulisho wake.
"Akijua jina alilonalo sio la utambulisho wake, ataanza kujioa sio wa huku ni wa kule, itamvuruga kisaikolojia na kutaka kumjua baba yake.
"Hivyo tuwaombe wazazi kina mama wawape majina ya utambulisho halisi watoto wao, labda kuwe na sababu za kiusalama uenda umezaa na askofu au padri, uliamua kuutoa mwili wako sadaka ukabeba mimba ndipo utandika ubini tofauti, lakini huko mbele ya safari mtoto aambiwe ukweli," anasema.
Mitazamo ya wengine
Katika mtandao wa kijamii wa Instagram ya Mwananchi, suala hilo liliibua mjadala mkali huku baadhi ya watu wakipinga na wengine wakitaka watoto wasiingizwe kwenye ugomvi wa wazazi.
Segito Mgonanzi alisema maumivu ya mtoto kukataliwa na baba yake ni makali mno na mama mzazi ndiye anayafahamu.
"Watuache tu tuandike tunavyojua, lakini hamjui maumivu ya kuandika un known yapoje kwa mtoto,” aliandika.
Shayo Luicensi yeye alisema kuandika jina la babu wa mtoto haisaidii akisema ni bora kuandika jina la baba halisi hata kama hamhudumii.
sibuma_binadamu anaona ni vema ugomvi wa wazazi ubaki baina yao, lakini usiathiri jina na ubini wa mtoto kwa namna yoyote.
Kwa mtazamo wa mgendison, Rita iishirikiane na madawati ya jinsia kutoa elimu na kuwakumbusha wazazi wajibu.
Ingawa Rita imeweka wazi kuhusu hilo, lakini ilikuwa vigumu kwa nely_qeuty yeye kukubali kuweka ubini wa baba asiyehudumia mimba.
|
Kutokana na kuongezeka kwa mwamko wa abiria kutumia usafiri wa treni ya umeme (SGR), wamiliki wa mab
|
Kutokana na kuongezeka kwa mwamko wa abiria kutumia usafiri wa treni ya umeme (SGR), wamiliki wa mabasi nchini wamekuja na mikakati mipya kuhakikisha wanaendelea kuwa sokoni bila biashara zao kuathirika.
Tangu kuanza kwa usafiri huo, wamiliki wa mabasi wamekuwa wakilalamikia changamoto katika soko na tayari wengine wameanzisha safari mpya katika njia zisizo na reli ya kisasa.
Makampuni kama Kimbinyiko, BM Coach, Abood na Shabiby tayari zimeanza kupanua huduma katika maeneo mapya, ikiwemo Sumbawanga, Bukoba, Musoma na hata nchi jirani ya Kenya.
Hatua hizi zinalenga kurejesha sehemu ya soko na kudumisha shughuli zao za usafirishaji licha ya mabadiliko makubwa katika sekta ya usafiri.
SGR, ambayo ilianza kutoa huduma hivi karibuni, imevutia wananchi zaidi, ikiwa na zaidi ya abiria 7,000 wanaosafiri kwa siku kati ya Dar es Salaam, Morogoro na Dodoma.
Ufanisi na mvuto wa mtandao huo wa reli umesababisha kupungua kwa idadi ya abiria wanaotumia usafiri wa mabasi kwa njia ya barabara.
Hata hivyo, wamiliki wa mabasi wamesema, licha ya treni kuchukua soko katika njia zilizozoeleka, haitakuwa shida kwao, kwa kuwa Tanzania ni kubwa.
Tanzania ina eneo la kilomita za mraba 945,087, ikiwa ni kubwa zaidi kuliko Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda kwa pamoja.
Eneo la nchi hizo nne lina ukubwa wa kilomita za mraba 877,852, huku Kenya na Uganda zikichukua sehemu kubwa zaidi ya kilomita za mraba 582,646 na 241,038, mtawalia.
Kuwepo kwa mipaka na nchi saba, ambapo nchi mbili kati ya hizo hazina bahari na zinategemea bandari za Tanzania kwa biashara za kimataifa, kunatoa fursa kwa wamiliki wa mabasi kutumia fursa hiyo.
Akizungumza na gazeti hilo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Mabasi ya Kimbinyiko, Ferdinand Mabumo alisema tayari kampuni yake ilishaanzisha njia nne mpya ili kuendana na soko linalobadilika.
"Tumepunguza safari kati ya Dar es Salaam na Dodoma kutoka safari 10 hadi nne kwa siku," alisema.
Njia mpya sasa ni Dodoma-Arusha, Arusha-Mbeya, Dodoma-Njombe na Moshi-Mbeya. Mipango ya baadaye ya kampuni hiyo ni kupanua huduma hadi Nairobi, Kenya.
Meneja wa Kampuni ya Mabasi ya Shabiby, Edward Magawa alisisitiza umuhimu wa kupanua maeneo ya huduma.
“Tanzania ni kubwa ingawa bado kuna mahitaji ya safari kati ya Dar es Salaam na Dodoma, tumejikita katika njia mpya kama vile Dodoma-Sumbawanga, Dodoma-Bukoba na Dodoma-Musoma,” alisema.
Shabiby pia imeagiza mabasi mapya yanayotarajiwa kufika katikati ya Oktoba ili kutumika katika njia hizo mpya.
BM Coach imeanzisha huduma za kuvuka mipaka, ikizindua njia mpya kati ya Dar es Salaam na Nairobi tangu Septemba 4, mwaka huu.
"Kwa sasa tupo kwenye majaribio na tuna mipango ya kupanua hadi Kampala na Rwanda," alisema Meneja wa Operesheni wa BM Coach, Gabriel Makundi.
Kampuni hiyo itaendesha safari nne kwa siku kwenye njia hiyo na inafikiria kuongeza njia ya Dar es Salaam-Tunduma hivi karibuni.
Kabla ya kuanza kwa SGR, BM Coach ilikuwa ikiendesha hadi mabasi 22 kwa siku kwenye njia ya Dar es Salaam-Morogoro na mabasi 10 kati ya Dar es Salaam na Dodoma.
Hata hivyo, kutokana na kuongezeka kwa usafiri wa reli, sasa ni mabasi sita tu yanayofanya safari kati ya Dar es Salaam na Morogoro na manne kati ya Dar es Salaam na Dodoma.
Licha ya changamoto zinazotokana na SGR, wamiliki wa mabasi nchini wanatumia uwezo wao wa kubadilika na kupanua njia zao ili kuhakikisha wanaendelea kuwa sehemu muhimu ya mtandao wa usafiri nchini.
BRT kama mbadala
Wamiliki wa mabasi wamesema wako tayari kuwekeza kwenye mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) endapo maboresho yatafanywa katika ukusanyaji wa nauli na mikataba ya uendeshaji.
Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa) kinahimiza ushiriki zaidi katika mfumo wa BRT ili kuendeleza biashara zao huku mtandao wa reli ukiendelea kubadilisha sekta ya usafiri.
Katibu Mkuu wa Taboa, Priscus Joseph aliliambia gazeti hili kuwa, mazungumzo na Wakala wa Usafiri wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (Dart) yalifanyika mwaka 2022.
Katika mazungumzo hayo, wamiliki wa mabasi walipendekeza kununua mabasi ya kuendesha ndani ya mfumo wa BRT lakini bado hawajapata mrejesho.
“Tulipendekeza turuhusiwe kuwekeza kwenye mabasi huku serikali ikibaki na miundombinu, lakini bado hatujapata majibu,” alisema.
Mradi wa BRT, unaotekelezwa kwa awamu sita, umekumbwa na changamoto za kimuundo.
Awamu ya Kwanza ya BRT, iliyoanza mwaka 2016, ilikusudiwa kuendeshwa kwa mabasi 305 lakini kwa sasa yanafanya kazi mabasi 210 tu, huku mengi yakiwa yameharibika.
Awamu ya Pili ya BRT, iliyokamilika Oktoba mwaka jana, inasubiri kuwasili kwa mabasi mapya.
Mapema mwezi huu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mchengerwa aliitaka Dart na Udart kushirikiana kuwaingiza waendeshaji wa mabasi ya mikoani kwenye mfumo wa BRT ili kuboresha huduma za abiria badala ya kusubiri wawekezaji kutoka nje.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kadi na mageti ya kisasa kwenye vituo vya BRT Dar es Salaam, Mchengerwa alisema kuanza kwa huduma za treni za umeme kwenye SGR kumeathiri baadhi ya waendeshaji wa mabasi ya mikoani.
Kwa hivyo, ingefaa kuangalia uwezekano wa mabasi hayo kufanya kazi ndani ya mfumo wa BRT.
“Kumekuwa na mjadala wa muda mrefu kuhusu suala la mabasi. Awamu ya Kwanza ya BRT bado inahitaji mabasi 170 ili ifanye kazi kwa ufanisi, na mabasi 500 yanahitajika ili kuanza kazi kwa Awamu ya Pili ya BRT kwenye njia ya Mbagala. Hakikisheni mabasi yananunuliwa kufikia Desemba mwaka huu,” alisema.
Mchengerwa alisema; “Wamiliki wa mabasi ya mikoani, ambao wamekuwa wakisafirisha abiria kwa miaka mingi, wanaweza kufanya kazi kwa ufanisi katika njia za BRT. Kwa hivyo, wito unatolewa kwa waendeshaji wa ndani kuwekeza kwenye BRT badala ya kusubiri wawekezaji wa kigeni.”
Kwa upande wake, Makundi alisema ingawa wamiliki wa mabasi wako tayari na wanataka kutumia fursa hiyo, kuna haja ya uwazi zaidi kwenye mchakato wa zabuni kwa ajili ya uendeshaji wa mabasi ya BRT.
“Tangazo rasmi la zabuni linapaswa kutolewa ili kuainisha vigezo vinavyohitajika kwa mabasi ya mikoani kushiriki kwenye mfumo wa BRT,” alisisitiza.
Magawa wa Shabiby alisema kampuni yake iko tayari kuwekeza kwenye BRT lakini akatoa wito wa kufanyika mapitio ya nauli na mazingira bora ya uwekezaji.
Mkurugenzi Mtendaji wa Dart, Athumani Kihamia alikiri mazungumzo ya mwaka 2022 na wamiliki wa mabasi lakini alieleza kuwa hawakuafikiana.
“Tuna mpango wa kushirikisha waendeshaji zaidi ili kuelezea maendeleo yetu na kushughulikia masuala yanayowakabili,” alisema.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Taboa, Mustapha Mwalango alibainisha kupungua kwa idadi ya abiria na kuongezeka kwa mabasi yasiyo na kazi.
“SGR imeathiri shughuli zetu kuliko tulivyotarajia awali,” alisema.
Mkuu wa Mawasiliano wa Latra, Salum Pazzy alishauri wamiliki wa mabasi kuiona SGR kama fursa badala ya tishio.
Alibainisha SGR ikitumika vema, kutakuwa na ongezeko la mahitaji ya mabasi kusafirisha abiria kutoka Dodoma kwenda mikoa mingine.
Mkurugenzi wa Usafiri wa Barabara wa Latra, Johansen Kahatano alithibitisha kupungua kwa huduma za mabasi.
“Tafiti zetu zinaonyesha kupungua kwa safari za mabasi na idadi ya abiria tangu SGR ilipoanza. Tunafanyia kazi kutatua athari hizi,” alisema.
Kutokana na hali hiyo, Latra inapanga kuandaa mkutano wa wadau wa usafiri, waendeshaji wa mabasi na Shirika la Reli Tanzania (TRC) ili kuchunguza njia za kuboresha muunganiko wa usafiri na kupunguza gharama za nauli kwa abiria.
Mkutano huo utalenga kutafuta suluhisho na kuboresha ushirikiano kati ya huduma za mabasi na treni, hususan karibu na vituo vya SGR.
Kadri sekta ya usafiri inavyoendelea kubadilika, wamiliki wa mabasi wana matumaini kwamba ushirikiano zaidi na mipango madhubuti itawezesha kuendelea kutoa huduma muhimu za usafiri nchini.
|
Licha ya Jeshi la Polisi kupiga marufuku maandamano ya Chadema, chama hicho kimesema kitu pekee kita
|
Licha ya Jeshi la Polisi kupiga marufuku maandamano ya Chadema, chama hicho kimesema kitu pekee kitakachositisha mpango huo ni jeshi hilo kuwarejesha viongozi wote waliotekwa wakiwa hai au wafu.
Mpango wa maandamano ulitangazwa Septemba 12 na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kushinikiza kurudishwa kwa viongozi wake waliotekwa.
Kabla ya maandamano hayo, Mbowe alitoa hadi Septemba 21, mwaka huu, Serikali iwe imeshawarejesha viongozi hao na kinyume na kulitekeleza hilo, Septemba 23, wataandamana jijini Dar es Salaam.
Siku moja baada ya tangazo hilo la Chadema, jeshi la polisi kupitia msemaji wake, David Misime lilipiga marufuku maandamano hayo, likizuia wanachama na wafuasi kusafiri kutoka maeneo mbalimbali kwenda kushiriki tukio hilo.
Kutokana na hali inayoendelea, wadau wameikosoa marufuku ya polisi wakisema ni mapema sana kuzuia, walipaswa kuacha ili waone iwapo chama hicho kitafuata utaratibu au vinginevyo.
Lakini, wengine wameonyesha mashaka na marufuku hiyo, wakisema inawezekanaje Chadema hao hao waliruhusiwa kuandamana katika majiji makubwa nchini na sasa wanazuiwa.
Kauli ya wadau
Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Fulgence Massawe amesema kwa sasa jeshi la polisi linapaswa kusubiri hadi tarehe ya maandamano ndipo litoe kauli.
Sababu ya kusubiri huko, amesema ni kuona iwapo Chadema itafuata utaratibu kabla ya kufanya maandamano au hapana.
Lakini, ameeleza kilichofanywa na jeshi la polisi kupiga marufuku kabla hata ya kujua iwapo Chadema watafuata utaratibu wa kutoa taarifa kwa mamlaka husika, si sawa.
“Jeshi la polisi lilipaswa kusubiri hadi muda ufike ndipo waseme lolote, hawakupaswa kuingilia kati kabla hawajajua kama Chadema watakiuka utaratibu au hapana,” amesema.
Kwa sababu kuandamana na haki ya kikatiba kwa kila mtu, ameeleza hakukuwa na sababu ya kupiga marufuku hasa ukizingatia chama hicho kinazo hoja kinazozishinikiza kupitia maandamano hayo.
“Chadema wana haki ya kuandamana hasa kwa hoja waliyonayo na ukizingatia Katiba inaruhusu kuandamana. Chadema walifanya maandamano ya amani na yalikwenda vema haijulikani kwa sasa nini kimebadilika hadi polisi wanapiga marufuku,” amesema.
Wote wafuate sheria
Mkurugenzi wa Taasisi ya Haki Taarifa, John Kitoka amesema pande zote mbili kwa Chadema na Jeshi la Polisi wanapaswa kuheshimu sheria na Katiba ya nchi.
“Maamuzi ya Chadema yako ndani ya Katiba na maandamano yao yanatakiwa kulindwa na kuhakikishiwa usalama na kama kutakuwa na vihatarishi vya uvunjivu wa amani kama wanavyodai Polisi wanapaswa kushughulika navyo na si kuzuia haki ya watu kuandamana,” alisema
Kitoka katika maelezo yake amedai iwapo Polisi wataenda nje kwa kuzuia maandamano hayo watakuwa wanavunja haki ya watu ya kukusanyika na kupashana habari.
“Chadema wanahaki ya kufanya hivyo kutokana na matukio kadha wa kadha yaliyojitokeza ya watu kutekwa,utesaji na uaji wa raia wasiokuwa na hatia,”alisema
Alisema sababu walizotoa Polisi kuzuia maandamano ni kuibua hasira kwani bado hazina mashiko na kwa nyakati tofauti wamekuwa wakidai hali ni shwari.
“Ukirejea maamuzi ya Rais kupitia mtandao wake wa kijamii wa X ni kwamba hali ya usalama si shwari na akaagiza uchunguzi ufanyike ili apate ukweli kuhusu yanayotokea," alisema
Kitoka alisema hata Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Emmanuel Nchimbi alitoka hadharani hawakubaliani na matukio ya utekaji na mauaji yanayojitokeza.
“Polisi wanaonyesha hakuna shida lakini wakati huohuo wanaona kuandamana kama ni uvunjivu wa amani, chadema wanaandama kwakuwa matukio yanayojitokeza Polisi walipaswa kuzuia,” alisema.
Mwanaharakati, Gemma Akilimali alisema jeshi la Polisi linapaswa kujisahihisha.
“Katika kujisahisha wanapaswa kuangalia watendaji wao inawezekana walioingia ni majangili lakini wameingizwa kama walikuwa na hiyo tabia hawawezi kuacha ya kumtisha mwananchi," alisema
Alisema sheria inalitaka jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi na usalama wa mali za raia na maandamano wanayotaka kufanya Chadema yanapaswa kulindwa ili kuondoa dhana tofauti kwa wananchi.
“Jeshi la Polisi kupinga inaibua maswali mengi, kwanini unapinga inawezekana kuna ukweli ndiyo maana wanataka wasiandamane kama ndivyo kwanini wazuie basi wanajua makosa yao na wanaona kama yanalipuliwa,”alisema
Alisema maandamano ni haki ya wananchi huku akieleza kinachoendelea nchini Polisi hawataki hata kujenga utamaduni wa kujielimisha ni kiasi cha kusema kama wanataka kuandamana basi wataimarisha ulinzi.
“Polisi hawana haki ya kuzuia maandamano kwa sababu wenzao wanasababu na si shida za wanachadema pekee bali ni tatizo lilolifika Taifa nzima sasa wanataka wananchi wote wanyanyuke,” alisema
Alisema maandamano hayo hayapaswi kuzuiwa kwa sababu yanalenga kuwabeba wale wote walioumia na matatizo yanayolikumba taifa kwa waliotekwa,kuteswa na kuawa na ndugu au watu wao wa karibu.
Msimamo wa Chadema
Kitu pekee kitakachosimamisha maandamano ya Chadema ni Serikali kuwarudisha viongozi wao waliotekwa wakiwa hai au wafu na si kingine chochote, kama inavyoelezwa na Mkurugenzi wa Itifaki na Mambo ya Nje wa chama hicho, John Mrema.
Amesema kitakachofanywa nao ni kufuata utaratibu wa kisheria unaowataka kutoa taarifa ndani ya saa 48 juu ya maandamano hayo, eneo yatakapofanyika na njia watakazopita.
“Wataosababisha maafa ni polisi sio sisi. Sisi tutafuata sheria na ikifika Septemba 21 kama polisi hawajawarejesha viongozi wetu tutaanza kuchukua hatua,” amesema.
Anasisitiza hawataogopa kutekeleza hilo kwa sababu wakiendelea kufanya hivyo, vitendo hivyo havitafika mwisho.
Hata hivyo, ameeleza hadhani kuwa chama hicho kinahitaji meza ya mazungumzo na jeshi la polisi, isipokuwa kila upande unapaswa kufuata sheria.
“Sisi kama chama hatuhitaji kupatanishwa na jeshi la polisi wao wafuate sheria na sisi tutafuata sheria hapo ndipo tutaenda vema,” amesema.
|
Usisubiri hadi kumbukumbu yake ya kuzaliwa au kumbukizi ya siku ya ndoa ‘anniversary’ kumwonyesha mk
|
Usisubiri hadi kumbukumbu yake ya kuzaliwa au kumbukizi ya siku ya ndoa ‘anniversary’ kumwonyesha mkeo thamani yake maisha mwako, unajua ipo siku rasmi ya kuadhimisha kumuenzi mke. Kwa lugha ya kimombo inaitwa ‘Wife Appreciation Day’.
Siku hiyo inayoadhimishwa Septemba 15 (leo), kila mwaka imeteuliwa kuwa maalumu kwa ajili ya kuhakikisha unamshukuru, kumsifu na kumpongeza kwa kazi kubwa anayoifanya kama mke.
Andiko hili halihalalishi kumpitisha mkeo katika mitihani kwa siku zote usubiri Septemba 15 ndiyo umwonyeshe thamani yake hapana, muktadha ni kuitumia siku hii maalumu kama nyenzo ya kustawisha upendo, furaha na hali ya kuaminiana na mkeo.
Katika maisha ya ndoa ni muhimu kuonyesha thamani kwa mke wako. Hii si tu inadhihirisha kwamba unamwona na kumthamini, bali pia inaimarisha mahusiano yenu na kukuza upendo wa kweli. Haijalishi umekuwa na ndoa kwa mwaka mmoja, miaka 10 au hata 50, lazima uonyeshe mke wako jinsi alivyo na thamani kwako.
Umuhimu wa kulifanya hilo, unathibitishwa na takwimu za Taasisi ya Maendeleo ya Familia ya Afrika Mashariki za mwaka 2021, zinaoonyesha asilimia 65 ya familia zilizo na msingi wa uaminifu na kuthaminiana huwa na utulivu wa ndoa kwa kipindi kirefu zaidi kuliko zile zisizo na utaratibu huo.
Kama hiyo haitoshi, utafiti wa Chuo Kikuu cha Stanford mwaka 2018, ulibaini wanandoa walioonyesha kuthaminiana waliripoti kiwango cha juu cha furaha na kuridhika kwenye ndoa zao. Asilimia 80 ya wanandoa walioshiriki kwenye utafiti huo walisema kuthaminiana ni kiungo muhimu cha kudumisha uhusiano wa furaha.
Benki ya Dunia nayo mwaka 2020, iliweka wazi kuwa, familia zenye wanandoa wanaoheshimiana na kuthaminiana zina uwezo mkubwa wa kushirikiana kwenye maamuzi ya kifedha, jambo linalowasaidia kujenga uchumi imara.
Kwa baadhi ya wanaume, kuonyesha hisia za upendo inaweza kuwa jambo la kawaida. Lakini kwa wengine, inaweza kuwa changamoto. Si kwa sababu ya dosari ya tabia au makosa yako, bali kwa sababu baadhi ya wanaume hawapendi kuonyesha hisia zao au wanapata shida kuziwasilisha.
Tunajua hali hiyo, lakini siku ya kumuenzi mke wako inatoa nafasi bora ya kuhakikisha mke wako anajua jinsi anavyothaminiwa.
Unaweza kujifunza kuadhimisha siku hii
Kwanza kabisa mwanaume wa kweli na anayejali ndoa yake huhitaji kujua miaka ya ndoa. Badala yake anapaswa kufungua milango kwa mke wake, kumpongeza kwa busu la ghafla, kumletea maua au kutumia muda mzuri pamoja ili kumfanya ajue jinsi anavyothaminika kwake.
Siku hii inahusu kuonyesha upendo wako kwa mke wako na kuthibitisha thamani yake kwako. Mara nyingi hatutoi shukurani ya kutosha kwa wale tunaoishi nao kwa karibu, hususan wake.
Wakati umekaa na mtu kwa muda mrefu, inaweza kuwa rahisi kupuuza mambo yote wanayofanya kwa ajili yako. Iwe ni kupika chakula cha jioni au kukufanya uache tabasamu kila siku, ni muhimu kutafakari jinsi mke wako anavyochangia maisha yako na kumfanya ajue kuhusu hili.
Kununua pete kwa mke wako ni mila ya zamani sio kwa ndoa tu au uchumba, bali pia kwa maadhimisho ya miaka yenu ya ndoa. Unaweza kutumia siku hii kuhuisha ndoa yenu kwa kumnunulia pete nyingine.
Kitendo cha kutoa pete kama ishara ya upendo kilifanywa na mshairi wa Kirumi wa vichekesho aitwaye Plautus. Miaka michache baadaye, katika karne ya nne, kitendo hiki kilibadilishwa kuwa cha Kikristo.
Historia ya siku hii
Siku ya kumuenzi mke wako ni tukio la kupendeza linalowapa waume nafasi ya kuonyesha jinsi wanavyopenda na kuthamini wake zao. Tangu ilipoanzishwa, imeorodheshwa katika kalenda ya matukio ya kila mwaka ya Chase na imekuwa maarufu sana.
Kuna mambo mengi ambayo mke mwenye mapenzi na msaada hufanya kwa mume wake, na hii ni fursa kwa waume kutazama nyuma na kukumbuka mambo makubwa na madogo ambayo huongeza thamani kwenye maisha yao.
Jinsi ya kuadhimisha siku ya kumuenzi mkeo wako
Mbali ya kumununulia zawadi ya pete mwanaume anaweza kumuagizia mkeo shada la maua analolipenda, kumfanyia sapraizi ya kuandaa mahali mtakapopata chakula cha jioni pamoja au kumpeleka kwenye mapumziko mafupi ya kimapenzi. Pia unaweza kumnunulia manukato au kitu cha kipekee ambacho kitabaki kama kumbukumbu kwa siku nyingi zijazo.
Hii haimlazimishi anayeifanya kutumia fedha nyingi, anaweza kuiandaa kulingana na mazingira na kipato chake ilimradi muhusika ambaye ni mke afurahi na kuona namna anavyothaminiwa na mumewe.
|
Tanzania inaungana na mataifa mengine kuadhimisha demokrasia katika kipindi ambacho, wanazuoni na ri
|
Tanzania inaungana na mataifa mengine kuadhimisha demokrasia katika kipindi ambacho, wanazuoni na ripoti mbalimbali zinaonyesha dosari katika misingi ya demokrasia ya nchi.
Kwa mitazamo ya wanazuoni hao, Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, ndiyo uliokuwa ukomo wa safari njema ya demokrasia nchini, baada ya kushuhudiwa misingi kadhaa ikivunjwa.
Uchaguzi huo, ulimweka madarakani Hayati John Magufuli aliyemshinda mpinzani wake kutoka chama cha upinzani cha Chadema, Edward Lowassa.
Uongozi wa Hayati Magufuli, unatajwa kukiuka misingi lukuki ya kidemokrasia, ikiwemo kuzuia mikutano ya hadhara kwa vyama vya upinzani, lakini kukomesha uhuru wa vyombo vya habari.
Hali iliyoshuhudiwa mwaka huo, iliendelea na demokrasia haikuwahi kutengemaa hadi sasa, kwa mujibu wa wanazuoni hao waliozungumza na gazeti hili.
Historia ya Tanzania katika safari ya demokrasia, ilianza baada ya uhuru mwaka 1961, wakati huo nchi ikiendeshwa chini ya mfumo wa chama kimoja cha TANU na baadaye CCM baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964.
Mfumo huo wa chama kimoja uliendelea hadi mwaka 1992, wakati mfumo wa vyama vingi ulipoanzishwa rasmi.
Hii ilifungua milango kwa vyama vya siasa kushiriki katika uchaguzi na kutoa fursa kwa raia kushiriki katika maamuzi ya kisiasa.
Iliharibika tangu 2016
Akizungumza na Mwananchi Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Dk Conrad Masabo anasema demokrasia ya Tanzania ilishaharibiwa tangu mwaka 2016.
Kuharibika kwake, Dk Masabo anasema kulitokana na uamuzi uliofanywa na Watanzania kuamini mtu na sio utaratibu na hilo lilifanyika tena mwaka 2021 alipoaminiwa mtu na sio mifumo.
“Tunachokipitia ni matokeo ya hayo maamuzi yetu. Demokrasia kama haki nyingine hudaiwa na sio kuombwa, pia inapaswa kulindwa ili walioitoa wasiipokonye tena,” anasema.
Katika vipindi hivyo, Dk Masabo anasema Watanzania wote waliamini Hayati John Magufuli ni mkombozi na 2021 waliamini Rais Samia Suluhu Hassan atakomboa, hadi kupigiwa chapuo na vyama vya upinzani.
Kwa mtazamo wa mwanazuoni huyo, kwa hali ilivyo hadhani kama maboresho yanawezekana.
Lakini, anaeleza uwezekano upo katika mambo mawili ambayo ni kuja kwa kiongozi mwenye hisani aijenge, ingawa hilo ni gumu kwa mfumo wa demokrasia ya vyama uliopo.
Jambo la pili, anasema au wananchi wajiunge kuidai kitu ambacho ni kigumu kwa vile raia wameamua kuwaachia wanasiasa jukumu hilo.
“Kuna uwezekano mkubwa wa kulipa thamani kubwa ili kurejea tulipokuwa 2015, swali ni nani wa kulipa gharama hii?,” anahoji.
Dk Masabo anasema kinachoitesa Tanzania ni kwa sababu demokrasia yake ni ya vyama na sio ya raia, hivyo raia au wananchi wanaamini hawana wajibu wa kudai na kuilinda.
“Mafanikio ya Reject Financial Bill (kuondolewa kwa muswada wa fedha) ya Kenya ni kwa vile ilikuwa inaongozwa na kusimamiwa na raia na ndio maana baada ya vyama kuingia, malengo na mafanikio yamepotea,” anafafanua.
Mtazamo kama huo unatolewa pia na Mwanazuoni mwingine, Profesa Mohamed Bakary anayesema kuna anguko kubwa la demokrasia linaloendelea kushuhudiwa nchini, ukilinganisha na ilivyokuwa mwanzo.
Anasema Tanzania ilianza kuingia katika mfumo wa demokrasia kwa mguu wa kulia, lakini kwa kadri siku zinavyokwenda hali inakuwa mbaya zaidi.
Msingi wa hoja yake hiyo ni kile anachofafanua, Tanzania ilianza kuiishi demokrasia baada ya kuruhusu mfumo wa vyama vingi na katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995, ilishuhudiwa demokrasia ya hali ya juu.
Anasema hali ilikuwa hivyo hadi katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, vyama vya upinzani vilishuhudiwa vikipata nafasi ya kuongeza katika ngazi ya mitaa, vijiji, vitongoji na hata majimbo.
“Ile hali iliashiria kuimarika na kuendelea kukua kwa demokrasia tangu mfumo wa vyama vingi ulipoanza,” anaeleza.
Anguko, anasema lilianza kushuhudiwa mwaka 2015, ule uhuru wa uchaguzi na ambo mengine yanayoijenga misingi ya demokrasia ilianza kuyeyuka.
Badala ya kusonga mbele, Profesa Bakary anasema Tanzania ilianza kurudi nyuma kidemokrasia hadi ulifika wakati idadi ya washindi wa vyama vya upinzani katika nafasi mbalimbali ziliporomoka.
“Hata matukio ya watu kupotea yanayoripotiwa sasa ni ishara ya kuonyesha kwamba tumerudi nyuma. Tulitarajia kama tungekuwa tumepiga hatua haya matukio yangefanyiwa uchunguzi na watuhumiwa wangetangazwa hadharani na hatua zingechukuliwa,” anasema.
Lakini hali iliyopo sasa, mwanazuoni huyo anasema unakuta watu wanajichukuliwa sheria mkononi na uwajibikaji hauonekani.
“Kuna kurudi nyuma kwa kiwango cha kutisha na inaweza kuleta hatari ya demokrasia kusambaratika kabisa,” anasema.
Demokrasia kwa mtazamo wa tafiti mbalimbali
Hali mbaya ya demokrasia nchini, inapigiwa msumari na Ripoti ya Freedom House ya mwaka 2023, iliyoipa Tanzania alama 32 kati ya 100 katika kipimo cha uhuru.
Katika utafiti huo, nchi hupimwa kulingana na uhuru wa kisiasa na kiraia na kwa mujibu wa takwimu hizo Tanzania imetafsiriwa kuwa nchi isiyo huru.
Hali inaashiria changamoto katika maeneo kama uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa kujieleza na uwazi wa uchaguzi.
Mbali na Freedom House, Ripoti ya Democracy Index ya The Economist Intelligence Unit (EIU) mwaka 2022, iliiorodhesha Tanzania kuwa nchi yenye utawala wa mabavu, ikiwa na alama 3.44 kati ya 10.
Hii ni ishara kuwa bado kuna vikwazo vinavyoathiri demokrasia ya nchi, hasa katika ushirikishwaji wa kisiasa na utawala wa sheria.
Sambamba na ripoti hizo, mifano ya hivi kaibuni nayo in aonyesha changamoto katika demokrasia, mathalan Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.
Katika uchaguzi huo, kuliibuka madai ya ukiukwaji wa haki za upinzani, udanganyifu katika kuhesabu kura na kuzuiliwa kwa wagombea wa upinzani kufanya kampeni zao kwa uhuru.
Kwa mujibu wa ripoti ya Tume ya Uchaguzi ya Tanzania (NEC) wakati huo, aliyeshinda uchaguzi huo ni Hayati Magufuli akipata asilimia 84 ya kura zote.
Hata hivyo, vyama vya upinzani kama CHADEMA na ACT-Wazalendo vilipinga matokeo hayo, vikidai uchaguzi haukuwa huru na wa haki.
Kuna fursa ya kuboresha
Licha ya changamoto hizo, kuna fursa ya kuboresha hali ya demokrasia nchini. Mabadiliko yaliyofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan tangu alipoingia madarakani mwaka 2021 yanaonyesha matumaini.
Rais Samia ameonyesha utayari wa kufanya mageuzi katika maeneo kama uhuru wa vyombo vya habari na haki za kisiasa.
Serikali yake imeruhusu upya mikutano ya kisiasa ya vyama vya upinzani, hatua iliyopongezwa na viongozi wa kisiasa na wanaharakati wa haki za binadamu.
Pia, kumekuwa na jitihada za marekebisho ya katiba. Wanaharakati wa haki za binadamu na vyama vya siasa wameendelea kusisitiza haja ya katiba mpya, itakayoweka misingi imara ya haki za kiraia, usawa wa kisiasa, na uhuru wa vyombo vya habari. Rais Samia ameonyesha utayari wa kufufua mjadala wa katiba mpya, na hii ni ishara ya matumaini kwa maendeleo ya demokrasia nchini.
|
Baadhi ya wanazuoni na wadau wa haki jinai, wamesema hatua ya kuibua tuhuma zinazolichafua Jeshi la
|
Baadhi ya wanazuoni na wadau wa haki jinai, wamesema hatua ya kuibua tuhuma zinazolichafua Jeshi la Polisi, inawatengenezea sumu wananchi na hivyo wanajenga dharau kwa chombo hicho cha ulinzi na usalama.
Dharau hizo kwa mujibu wa wadau hao, matokeo yake ni vitendo vya uvamizi wa vituo vya polisi na hatimaye kulifanya jeshi hilo lishindwe kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
Wamekwenda mbali zaidi na kusisitiza, makosa ya askari wachache wasio waadilifu ndani ya jeshi hilo, yasitumike kulichafua jeshi zima, lililojitoa kulinda usalama wa raia na mali zao.
Ingawa wadau hao wameibuka na mtazamo huo, wanazuoni wengine wamepingana na hoja hizo, wakisema kinachoshuhudiwa ni wananchi kupoteza imani na vyombo vya ulinzi na usalama na sio kuvidharau.
Hata hivyo, wanazuoni hao wanasema kupotea kwa imani hizo ni matokeo ya utendaji wa jeshi la polisi na vyombo vingine, ikiwemo matumizi ya nguvu yaliyoondoa maana ya huduma kwa wananchi badala yake imekuwa kuwaonea.
Hatua mbaya
Akizungumza na Mwananchi Jaji mstaafu, Francis Mihayo, amesema miongoni mwa hatua mbaya kuwahi kutokea ni wananchi kulidharau jeshi la polisi kiwango cha kuvamia kituo.
Kwa mujibu wa mtaalamu huyo wa sheria aliyehudumu katika mahakama kwa miongo kadhaa, polisi ndiyo mamlaka yenye jukumu la kulinda watu na mali zao, inapotokea wanadharauliwa ni mwelekeo mbaya.
“Sisi tukiwa vijana isingewezekana mtu akimbilie kituo cha polisi alafu atokee mtu akalazimishe kumtoa, ni jambo gumu na lisingewezekana, najiuliza kwanini haya yanatokea sasa,” amesema.
Alikwenda mbali zaidi na kueleza tabia hiyo itasababisha taifa lifikie hatua hatari zaidi hasa ya wananchi kuona vituo vya polisi ni maeneo ya kawaida.
Lakini yote hayo kwa mujibu wa Jaji Mihayo, yanachochewa na kauli za baadhi ya viongozi kushusha lawama na tuhuma kwa jeshi hilo, zikiwemo za utekaji na mauaji ya watu.
“Naanza kuona kama vile baadhi ya viongozi wanawafanya wananchi wasiliamini jeshi kwa kulitupia lawama kila wakati,” amesema.
Kwa sababu polisi, amesema ni chombo chenye mamlaka ya ulinzi wa amani, si vema kulilaumu na kulituhumu hadharani kwa matendo ya wabaya wachache.
“Jeshi ni chombo kizuri isipokuwa wapo wabaya ndani yake, sasa wabaya hao wasitumike kuwachafua wengine au kulichafua jeshi la polisi kwa ujumla wake,” amesema.
Amesisitiza umuhimu wa viongozi kuepuka kauli zinazolilaumu jeshi hilo, kwa kuwa kufanya hivyo kunapandikiza sumu kwa wananchi na hatimaye wanaanza kuwadharau polisi.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari juzi, Katibu Mkuu wa CCM, Dk Emmanuel Nchimbi amesema kati ya mambo mabaya yanayofanywa nchini, ni kulifarakanisha jeshi la polisi na wananchi.
Amesema hilo linafanywa ilhali katika baadhi ya maeneo wananchi wanajenga vituo vya polisi kwa nguvu zao na wanaomba wapelekewe polisi.
“Tunazunguka mikoani, mnaona wananchi wanavyojenga vituo vya polisi wenyewe na wanaomba wapelekwe askari. Ina maana kwa wananchi wa kawaida polisi wanafanya kazi yao vizuri.
“Sasa haiwezekani kukitokea polisi wawili watatu wenye matatizo ninyi mnataka wananchi wawakasirikie polisi nchi nzima hili halikubaliki ni jambo la ovyo kuliko yote ninayoyafahamu,” amesema.
Wasichokijua baadhi ya watu, amesema polisi ni miongoni mwa watumishi wanaotoa maisha yao kwa ajili ya wananchi kuliko inavyodhaniwa.
Ameijenga hoja yake hiyo kwa kurejea takwimu za miaka mitano kuanzia 2017/2023, akisema jumla ya polisi 42 waliuawa katika mapambano na majambazi, huku 141 wakijeruhiwa.
“Tafakari kwa dakika moja tu, hivi polisi wote wakisema wamechukua likizo kwa saa 24 itkuwaje katika nchi hii,” amesema.
Tumefikaje, madhara na tunatokaje
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk Revocatus Kabobe amesema utamaduni wa baadhi ya wananchi wa kujichukulia sheria mkononi si sahihi ukirejea hasa kwenye kuvamia vituo vya polisi.
Amesema ni hatari zaidi wananchi kukosa imani na jeshi la polisi ambalo kimsingi lipo kuwalinda raia na mali zao.
“Turudi kwenye misingi ya utawala wa sheria ambapo ni mahakama tu yenye mamlaka ya kusema nani mwenye kosa na nani hana.
“Tukianza kuchukua sheria mkononi tutabomoa taifa letu wenyewe kitu ambacho sio sawa. Haya ndo madhara ya kulidharau jeshi la polisi,” amesema.
Amesema yawezekana wananchi wana hoja ya msingi juu ya hatua wanayochukua, lakini kuchukua sheria mkononi na kuvamia vituo vya polisi haiwezi kuwa njia bora ya kutatua tatizo.
“Polisi wana silaha na wanapozitumia kujihami dhidi ya raia walowavamia madhara ni makubwa zaidi,” amesema.
Hata hivyo, amesema vitendo hivyo ni ishara kwamba kuna mahali taifa limeteleza kwa kudharau utawala wa sheria na kutotimiza wajibu kama raia na upande wa polisi pia.
Pia, amesema kuna matukio mengi ambayo jeshi la polisi linatuhumiwa kutotenda haki, jambo linalowafanya wananchi wawe na hasira hadi kujichukulia sheria mkononi.
“Matukio mbalimbali yanayoashiria polisi kujihusisha na siasa kitu ambacho ni kinyume na sheria zetu. Haya yote yanawafanya wananchi wapate taswira tofauti ya jeshi la polisi,” amesema..
Ili kujiepusha hilo, amependekeza kurudi kwenye misingi ya ujenzi wa taifa na kuiishi, ikiwemo utawala wa sheria.
Amependekeza polisi wawajibike kwa mujibu wa sheria na kanuni zao zilizojengwa kuwahudumia wananchi kwa kuwalinda na mali zao.
Kwa upande wa wananchi, amesema wanapaswa kutii sheria bila shuruti, wawajibike kushirikiana na polisi katika kutimiza majukumu yao.
“Jeshi la polisi liendelee kutoa elimu kwa wananchi juu ya haki na wajibu wao katika kulinda usalama wa nchi na watu wake. Bila polisi hakuna usalama,” amesema.
Sio dharau, hawana imani
Kwa mtazamo wa Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Sabatho Nyamsenda, kilichopo sio wananchi kulidharau jeshi hilo, bali wamekosa imani nalo.
Kukosa kwao imani na jeshi hilo, amesema ndiko kunakowafanya waamue kujichukulia sheria mkononi.
Hatua ya wananchi kukosa imani na jeshi hilo, imetokana na kile alichoeleza, badala ya kutoa huduma, polisi wameonekana wakitumia nguvu zaidi kulinda usalama wa raia.
“Kwa ujumla mara nyingi linatumia nguvu na linaonekana lipo kwa ajili ya kuwanyanyasa na sio kuwatumikia. Wananchi wanaona halitoi huduma bali linawanyanyasa,” ameeleza.
Kwa mujibu wa Dk Nyamsenda, mazingira hayo yameondoa uhusiano mzuri kati ya jeshi la polisi na wananchi tangu muda mrefu.
“Kilichotokea Geita ni kwamba wananchi waliona jeshi la polisi halitoi majibu sahihi juu ya kupotea kwa watoto na hata walipoandamana jeshi ilitumia nguvu kiasi cha kupoteza uhai wa raia mmoja.
“Kuna uwezekano mkubwa kwamba chombo hicho pengine kinafumbia macho au baadhi ya maofisa wake wasio waaminifu pengine ni wahusika wakuu, huu ndiyo mtazamo wa wananchi,” amesema.
Katika mazingira hayo, amesema kuna haja ya kuliangalia upya jeshi hilo, kama linaonekana kwenda kinyume na misingi ya kuanzishwa kwake, lifumuliwe.
“Kwa bahati mbaya polisi wanapotuhumiwa, majibu yao ni kuonyesha vitisho zaidi. Kama nchi ni vema kuchukua hatua kubwa ikiwemo kulifumua jeshi moja kwa moja.
“Nadhani huu sio muda wa kutoa vitisho na kuwalazimisha watu wawe na utii na chombo ambacho wanaona kinawaonea, badala yake tufikiri namna mpya ya kukifanyia Mageuzi,” amesisitiza.
Amesema kwa sababu jeshi hilo limeundwa na Watanzania, halitakuwa jambo gumu kulibadili kuwa namna ambavyo jamii ingetamani liwe.
|
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere (MNF), Joseph Butiku amewataka viongozi wa vyombo vy
|
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere (MNF), Joseph Butiku amewataka viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama wasiseme hawawajui wahusika wa uhalifu, kufanya hivyo kunaondoa sababu za wao kuwa na nafasi walizonazo.
Ameisisitiza hoja yake hiyo kwa kuweka wazi kuwa, wahalifu wa utekaji, mauaji na ulawiti wanajulikana kwa kuwa wanaishi miongoni mwa wananchi, makanisani, misikitini na kwenye vyombo vya dola.
Sambamba na hilo, Butiku ametaka uwajibikaji wa viongozi inapotokea maeneo waliyopewa kuyaongoza yameingia doa kwa namna yoyote.
Kauli hiyo ya Butiku, inakuja katika kipindi ambacho kumekuwa na mfululizo wa taarifa za matukio ya utekaji na mauaji ya raia na Ripoti ya Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), ilioroshesha watu 83 waliokumbwa na kadhia hizo.
Hata hivyo, kauli ya kiongozi huyo wa zamani serikalini tangu awamu ya kwanza, inakoleza mwendo wa matamko ya wadau hasa baada ya tukio la kuuawa kwa kada wa Chadema, Ali Kibao, aliyekamatwa Septemba 6, mwaka huu na wasiojulikana wakiwa katika usafiri wa umma.
Butiku ametoa kauli hiyo leo, Septemba 10, 2024 alipozungumza na waandishi wa habari, katika Ofisi za taasisi hiyo, Posta jijini Dar es Salaam.
“Wasitwambie hawajui, IGP (Inspekta Jenerali wa Polisi) asitwambie hajui, Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa asitwambie hajui, lazima wajue laa sivyo hawana sababu ya kuwa pale,” amesema.
Butiku amesema lazima Serikali iwajue kwa sababu wanaishi miongoni mwa wananchi, katika kaya, wapo ndani ya vyombo vya dola, wapo makanisani na katika misikiti.
“Viongozi wa vyombo hivi wasitwambie kwamba hawajui kinachotokea wanajua, wasitwambie kwamba wanamwogopa Rais wasimsingizie,” amesema.
Kwa mtazamo wa Butiku kutokana na mwenendo wa matukio hayo, viongozi wa vyombo vya usalama wanapaswa kuwajibika, huku akiwasihi wananchi waendelee kuviamini vyombo hivyo.
"Huwezi kuwa Waziri, halafu watu wanatekwa na kuuwawa kisha unasema Rais ameagiza, Rais kazi yake ni kupewa taarifa ili aagize, wajibu wa kwanza kwenye matukio haya ni wako wewe kiongozi wa ulinzi na usalama.
“Ukipewa kundi uliongoze, mambo ya aibu yakitokea katika kundi lile, nani unamuuliza. Tunachosema kuhusu vyombo vya ulinzi na usalama sio wote, hatutaki kuwalaumu wote.
“Ndani mule kuna watu wa ovyo wamefundishwa vizuri lakini hawakuiva kiusalama tunatarajia viongozi wao wawe wanajua,” amesema.
Katika mkutano wake huo, Butiku amesema Watanzania wanapaswa kuelewa kuwa Tanzania sio taifa la wauaji wala wahuni ni la watu wanaoishi kwa kuzingatia Katiba na sheria.
“Hakuna nafasi wala ruhusa kwa raia yeyote wa nchi kuishi nje ya utaratibu huo na huo ndiyo msingi wa amani, umoja na maendeleo yanayoshirikisha wananchi wote kwa faida yao. Kwa maana hii sisi Watanzania ni wastaarabu,” amesema.
Amewataka wananchi kumsaidia Rais kuwapata wabaya ili wachukuliwe hatua kwa kuwa mkuu huyo wa nchi ana vyombo vya dola vyenye utaalamu.
“Tanzania ina Rais mmoja aliyekabidhiwa katiba aitumie kuiongoza nchi na kulinda taifa na mali zake, anapaswa kuungwa mkono bila kusita na katika hilo bila maswali,” amesema.
Kuhusu kuundwa kwa tume huru kwa ajili ya kuchunguza, Butiku amesema hilo linapaswa kufanyika iwapo itabainika kuna ombwe la ujuzi kwa vyombo vya uchunguzi vilivyopo,
Hata hivyo, ameeleza kwa miaka 60 tangu uhuru wa Tanganyika haamini kama vyombo vya ulinzi na usalama vilivyopo vimekosa utaalamu huo.
Kuhusu suala la utekaji kutojadiliwa bungeni, amesema muhimili huo una utaratibu hasa katika mambo magumu yanapotokea.
Amesema kuna kamati na mambo yanapokuwa magumu, mnakwenda kwenye kamati hizo na Waziri Mkuu ndiye mwenyekiti huko kila mtu anayehusika atanyooshewa kidole.
“Mnayaamua alafu mnarudi bungeni bila kuwaletea wananchi mambo ya ovyo ovyo,” ameeleza.
|
Mataifa mbalimbali duniani yameeleza kusikitishwa na taarifa za vitendo vya ukatili, kupotea na vifo
|
Mataifa mbalimbali duniani yameeleza kusikitishwa na taarifa za vitendo vya ukatili, kupotea na vifo dhidi ya wanaharakati wa haki za binadamu na kisiasa nchini, huku yakisisitiza uchunguzi wa haraka kubaini wanaohusika.
Masikitizo ya mataifa hayo 15 yanayounda Umoja wa Ulaya (EU) yalitolewa na balozi zao zilizopo nchini, yakiisihi Serikali kuhakikisha ulinzi wa upinzani, ili kuendana na falsafa ya R4 kama alivyoahidiwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Falsafa hiyo yenye tafsiri ya Maridhiano, Ustahimilivu, Mageuzi na Kujenga upya, ilitambulishwa na Rais Samia mapema baada ya kuapishwa kuwa Rais Machi mwaka 2021, kama msingi wa utendaji wake.
Mataifa hayo 15 ni Ubelgiji, Uingereza, Canada, Denmark, Ufaransa, Finland, Ujerumani, Ireland, Italia, Uholanzi, Norway, Poland, Hispania, Sweeden na Uswisi.
Hata hivyo, tamko la mataifa hayo linakuja muda mchache tangu alipozikwa kada wa Chadema, Ali Kibao aliyekutwa ameuawa Ununio jijini Dar es Salaam, siku moja baada ya kukamatwa na wasiojulikana akiwa kwenye usafiri wa umma.
Kuuawa kwake kulimuibua Rais Samia kupitia mitandao ya kijamii, akiandika kusikitishwa na tukio hilo, huku akiviagiza vyombo vya uchunguzi kufanya uchunguzi wa kina na kuwasilisha taarifa kwake.
Katika taarifa yake hiyo, mkuu huyo wa nchi, alisisitiza Serikali chini yake haitavumilia vitendo vya namna hiyo.
Katika tamko la pamoja na mataifa hayo, lililotolewa leo, Septemba 10, 2024, nchi hizo zimeisihi Tanzania kulinda haki za msingi wa wananchi ukiwemo uhuru wa kujieleza.
“Jumuiya ya Umoja wa Ulaya unasikitishwa na taarifa za hivi karibuni za vitendo vya ukatili, kupotea kwa watu na vifo vya wanaharakati wa kisiasa na haki za binadamu,” limeeleza tamko hilo.
Umoja wa nchi hizo, umetaka uchunguzi wa kina wa matukio hayo, huku ukiwapa pole wanafamilia wote walioathiriwa na vitendo hivyo.
“Tunakaribisha wito wa Rais wa kuanzisha uchunguzi wa haraka ili kubaini wahalifu waliohusika na kuhakikisha kuna uwajibikaji,” imeelezwa katika tamko hilo.
Tamko hilo limetoa wito wa ulinzi wa upinzani, ili kuakisi falsafa ya R4 ya Rais Samia.
“Tunatambua kwa wasiwasi mkubwa kwamba matukio haya ya hivi karibuni yanatishia misingi ya kidemokrasia na haki za wananchi wa Tanzania.
“Katika nchi inayoheshimika kimataifa kwa amani na utulivu, na tunaungana na wito wa kulinda amani na utulivu wa nchi,” limeeleza tamko hilo.
|
Licha ya Rais Samia Suluhu Hassan kuelekeza mamlaka za uchunguzi zichunguze matukio ya mauaji, wadau
|
Licha ya Rais Samia Suluhu Hassan kuelekeza mamlaka za uchunguzi zichunguze matukio ya mauaji, wadau wamependekeza njia mbadala ya uchunguzi huo, wakitaka vyombo vya dola visihusike kutekeleza jukumu hilo.
Kwa mujibu wa wadau hao, kamisheni maalumu inapaswa kuundwa na mkuu huyo wa nchi itakayohusisha vyombo mbalimbali vya kijamii na kwamba pamoja na matukio hayo ilichunguze pia na Jeshi la Polisi.
Rais Samia alielekeza kufanywa kwa uchunguzi huo, juzi kupitia mitandao yake ya kijamii alipoandika kusikitishwa na tukio la kuuawa kwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Chadema, Ally Kibao.
“Nimeagiza vyombo vya uchunguzi kuniletea taarifa ya kina kuhusu tukio hili baya kabisa na mengine ya namna hii haraka. Nchi yetu ni ya kidemokrasia na kila raia ana Haki ya kuishi.
"Serikali ninayoiongoza haivumilii vitendo vya kikatili vya namna hii,” aliandika Rais Samia katika mitandao yake hiyo.
Mzizi wa maelekezo hayo ya mkuu huyo wa nchi ni tukio la kukamatwa kwa Kibao na baadaye kukutwa ameuawa Ununio jijini Dar es Salaam.
Taarifa za uchunguzi kutoka Hospitali ya Mwananyamala zilibaini kifo chake kimetokana na kipigo na kumwagiwa tindikani usoni.
Mbali na tukio la Kibao, uchunguzi unaozungumzwa na Rais Samia unatarajiwa kuhusisha matukio lukuki, likiwemo la kupotea, kutoweka na kutekwa kwa waandishi wa habari, wanasiasa na wanaharakati nchini.
Mwaka 2017, kada wa Chadema, Ben Saanane alitoweka katika mazingira ya kutatanisha na hadi sasa hajawahi kupatikana.
Tukio kama hilo, lilitokea kwa Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Mwananchi, Azory Gwanda aliyetoweka baada ya kufuatwa na watu nyumbani kwake mwaka 2017 hadi sasa hajulikani alipo.
Mwaka huo huo, aliyekuwa Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu ambaye sasa ni Makamu Mwenyekiti bara wa chama hicho, alishambuliwa kwa risasi na hadi sasa wahusika wa shambulio hilo hawajapatikana wala uchunguzi kufanyika.
Lakini, Agosti mwaka huu, wanasiasa kadhaa akiwemo Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Deusdedith Soka na wenzake wawili walitoweka baada ya kuitwa na watu wanaodaiwa kuwa na askari wa jeshi la polisi, hadi sasa haijulikani walipo.
Kada wa Chadema, Kombo Mbwana pia alitoweka nyumbani kwake katika mazingira ya kutatanisha, lakini baadaye jeshi la polisi lilikiri kumsikilia, licha ya siku za nyuma kukataa kuwa naye.
Hiyo ni mifano michache kati ya matukio mengi yanayohusisha utekaji, kutoweka na kuuawa kwa watu katika mazingira ya kutatanisha.
Hata hivyo, Agosti mwaka huu, Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) ilitoa orodha ya watu 83 waliotekwa, kutoweka na hata kuuawa, jambo lililoiibua Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kufanyia uchunguzi (THBUB).
Uchunguzi utakaofanywa na chombo huru ndiyo wito ulioonekana kutolewa na wadau wengi kama njia ya kupata jawabu la matukio hayo na Ubalozi wa Marekani ni miongoni mwa wadau hao.
Uchunguzi uwe hivi
Akizungumzia na Mwananchi jana, Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi alisema uchunguzi huo haupaswi kufanya na jeshi la polisi kwa kuwa lenyewe ndilo linalotuhumiwa.
Badala yake, alitaka viongozi wa juu wa jeshi hilo wawekwe chini ya uchunguzi, utakaofanywa na Kamisheni maalumu itakayoundwa na Rais Samia.
“Tunasema polisi wasichunguze kwa sababu wenyewe ndiyo watuhumiwa namba moja. Mara zote waathirika wametoa ushuhuda wakilitaja jeshi hilo au mazingira yanayolihusisha na matukio hayo,” alisema.
Kwa mtazamo wa Mwabukusi, kamisheni hiyo itakayoundwa na mkuu wa nchi, inapaswa kuwa na mwakilishi kutoka TLS, Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).
Wawakilishi wengine kwa mujibu wa Mwabukusi ni Wanasheria kutoka sekta ya umma, Usalama wa Taifa na Mwenyekiti wa Kamisheni hiyo anapaswa kuwa Jaji mstaafu wa Mahakama.
“Kamisheni hiyo ipewe kazi ya kulichunguza jeshi la polisi na vikosi kazi vyote. Hao watu watakaoteuliwa wasiteuliwe kwa majina, bali kila taasisi ielekezwe kupeleka jina la mwakilishi wake,” alieleza.
Katika pendekezo lake hilo, Mwabukusi alitaka kamisheni hiyo ipewe siku 60 kutekeleza jukumu hilo la uchunguzi kisha ikabidhi ripoti yake.
Wakati uchunguzi unaendelea, Rais huyo wa wanasheria Tanganyika alisema Serikali itoe tamko la dharura la kutoruhusiwa askari yeyote au kikundi chochote kwenda kukamata mtu bila hati ya mahakama au kiongozi wa Serikali za Mitaa.
“Kama mtu yupo kwenye chombo cha usafiri, abiria na dereva waruhusiwe kumpeleka mtu huyo kwa pamoja hadi katika Kituo cha Polisi kilichopo karibu naye,” alisema.
Hayo, alitaka yaende sambamba na hatua ya Rais Samia kutoka hadharani alaani, kukemea na aelekeze kuachiwa mara moja kwa wananchi wote waliotekwa au kukamatwa kwa uonevu, akiwemo Deusdedith Soka na Haji Kombo.
“Kwa sababu hawa ndiyo waathirika watakaoleza ukweli wa nini kipo nyuma ya pazia,” alisema.
Mtazamo wa Mwabukusi, haukutofautiana na Mwanazuoni wa Sheria wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Emeritus Fimbo aliyetaka kuundwa kwa tume ya kijaji itakayofanya uchunguzi wa jumla.
“Inawezekana wakati polisi wanafanya uchunguzi kuhusu tukio la Kibao, kukawa na chombo kingine cha uchunguzi kwa sababu kuna wanaohisi kwamba watendaji wa mambo haya ni polisi,” alisema Profesa Fimbo.
Hata hivyo, alisema mwenye mamlaka ya uundaji wa tume hiyo ni mkuu wa nchi na kwa utashi wake ndiyo anateuwa wajumbe na viongozi wa tume husika.
Alisema pamoja na kuundwa kwa tume hiyo, anachotilia shaka ni kuwekwa hadharani kwa ripoti itakayobainika kwa kuwa historia inaonyesha ripoti nyingi zilifichwa.
Kuhusu tukio la Kibao, alitaka uchunguzi utakaofanywa na Polisi uhusishe kuangalia kuangalia ilikuwaje, hizo gari zilizotumika ni za aina gani.
“Wale walioingia kwenye basi wachunguzwe wote waliokuwepo waliona nini. Alikaa siti gani na nani na waliokuwepo walisikia nini kutoka kwa aliyekuja na pingu,” alisema.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda naye alipendekeza kuundwa kwa tume hiyo ya kijaji kwa ajili ya kuchunguza matukio ya utekaji na mauaji.
“Mheshimiwa Rais taifa linahitaji tume ya kjaji kuchunguza matukio yote ya utekaji na mauaji,” aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa Twitter.
Jaji Werema awapa jukumu wanahabari
Alipotafutwa kuzungumzia hilo, Jaji mstaafu Frederick Werema alisema kabla ya uchunguzi mwingine, vyombo vya habari vinapaswa kuhakikisha vinafanya habari za uchunguzi kubaini mzizi wa tatizo.
“Wanahabari wanapaswa kufanya habari za uchunguzi kubaini sababu za tatizo, kama huyu niliyesikia kwamba amechukuliwa akiwa kwenye basi, uchunguzi wa wanahabari uje na jawabu la kwanini basi lilimwachia abiria wake kwa watu wasiojitambulisha,” alieleza.
Jaji Werema ambaye amewahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, alisema zaidi ya hivyo ni vema wananchi wasubiri uchunguzi ufanyike kama ilivyoelekezwa na Rais Samia kisha itajulikana kinachofuata.
Wito wa kuundwa kwa tume ya kijaji, ulitolewa pia na Makamu Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo bara, Issihaka Mchinjita alisema ni muhimu Rais Samia aunde tume ya kijaji kuchunguza matukio hayo.
Akiwa katika mazishi ya Kibao mkoani Tanga, Mchinjita alisema sababu ya kuundwa kwa tume hiyo ni kukosekana imani kwa vyombo vya ulinzi na usalama kama vinaweza kuwa sahihi kuchunguza matukio hayo.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe naye aliungana na wadau wengine kutaka tume ya kijaji ichunguze matukio hayo na vyombo vya dola kwa ujumla.
“Wote tumesikia kauli ya Rais jana, lakini kauli ya Rais ambayo inaelekeza vyombo vile vile ambavyo ni watuhumiwa namba moja wakajichunguze wenyewe tunaona hiyo haiwezekani hii nchi haitarekebika.
“Rai ya waombolezaji katika msiba huu, kamwambie Rais yeye pekee ndiye mwenye mamlaka ya kuunda tume ya kijaji ya kimahakama ambayo inaweza ikachunguza matukio yote haya na mengine mengi yaliyojificha,” alisema.
Alieleza ni imani yake kuwa, hiyo ndiyo njia pekee itakayowezesha kukomesha vitendo hivyo.
“Sisi ambao tuna ushahidi tutakuwa tayari kueleza mbele ya tume hii,” alisema.
Ubalozi wa Marekani
Katika hatua nyingine, Ubalozi wa Marekani umesisitiza uchunguzi huru na wa uwazi dhidi ya tukio hilo na mengine ya utekaji.
“Mauaji na kupotea kwa watu, kukamatwa, kupigwa na juhudi nyingine za kuwaengua raia katika uchaguzi zilizotokea mwezi ulipita, havipaswi kuwa na nafasi katika demokrasia,” imeelezwa katika tamko hilo.
Kwa mujibu wa tamko hilo, vitendo hivyo vinadhoofisha haki, za kikatiba.
TEF
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), liliongeza nguvu katika wito wa kuundwa kwa Tume ya Majaji kuchunguza wimbi la utekaji na mauaji.
“Tunaomba uongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani katika ngazi zote, ujitafakari iwapo unastahili kuendelea kuwapo wakati tuhuma hizi nzito za watu kutekwa zikiendelea kusikika sehemu mbalimbali nchini.
“Tunao mfano hai wa alichofanya Mzee Ali Hassan Mwinyi mwaka 1976 kwa nia ya kuleta uwajibikaji wafungwa walipouawa kwa kuteswa wakiwa gerezani mkoani Shinyanga,” imeeleza taarifa hiyo.
|
Gari mbili zilizokuwa na namba za usajili nyeupe zilizoandikwa kwenye vibao vyeusi, ndizo zilizotajw
|
Gari mbili zilizokuwa na namba za usajili nyeupe zilizoandikwa kwenye vibao vyeusi, ndizo zilizotajwa na mashuhuda kuhusika katika tukio la ukamatwaji wa Mjumbe wa Sekretarieti ya Chadema, Ally Kibao Septemba 6, mwaka huu.
Kwa mujibu wa mashuhuda hao, tukio hilo lilitokea saa 1 jioni, muda ambao tayari giza lilishaanza kuingia na hakukuwa na aliyekuwa na wasiwasi kwa kuwa walidhani wakamataji ni askari wa Jeshi la Polisi.
Kibao alikamatwa Septemba 6 Tegeta mbele ya Jengo la Kibo Complex na siku moja baadaye mwili wake uliripotiwa kupatikana Ununio jijini Dar es Salaam, akiwa amefariki, huku uso wake umeharibika kiasi cha kutotambulika.
Hata hivyo, taarifa ya uchunguzi wa kitaalamu kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala, imebaini kifo chake kimetokana na kipigo na kwamba alimwagiwa tindikali usoni.
Alivyokamatwa
Mwananchi imefika Tegeta alikokamatwa Kibao, ni umbali wa takriban mita 20 kutoka Jengo la Kibo Complex ni eneo ambalo aghalabu mabasi yanayoelekea Tanga, Moshi na Arusha husimama kupakia abiria.
Kama ulivyo utaratibu wa kawaida, basi hilo la TASHRIF alilokuwa amepanda Kibao lilisimama kupakia abiria kwa mujibu wa mashuhuda, gari mbili moja Land Cruiser na lingine ni V8 zenye namba za usajili nyeupe zilifika.
Shuhuda huyo amesema Land Cruiser iliegeshwa mbele ya basi hilo na V8 iliegeshwa nyuma ya basi hilo na kisha watu wanne walishuka kwenye gari hizo.
“Wanne wote walikuwa na risasi (akimaanisha bunduki) alienda kwenye mlango wa basi na wawili wakaingia ndani, wawili walibaki mlangoni,” amesema.
Alichokisikia shuhuda huyo ni kauli kutoka kwa mmoja wa watu hao kuwa, ‘tumemfuata mtu wetu’ na kwa namna walivyokuwa kila mmoja alidhani ni polisi.
Amesema walioingia ndani ya basi walitoka na Kibao wakiwa wamemfunga pingu na hata aliyekamatwa naye hakuwa na wasiwasi, hali iliyofanya mashuhuda waondoe wasiwasi zaidi.
“Walivyotoka naye wakamuongoza hadi kwenye Land Cruiser wakamwingiza humo na wengine wakaenda kupanda V8 wakaondoka naye,” ameeleza.
Uelekeo wa safari hiyo, shuhuda mwingine amesema ni Bagamoyo, lakini gari hizo awali zilifika hapo zikitokea uelekeo wa Mwenge.
“Kila mmoja akawa anasema jamaa amekamatwa na polisi atakua mhalifu, hakuna aliyekuwa na mashaka. Mimi niliangalia namba za usajili wa gari wakati zinaondoka lakini sikuzizingatia, nilichoona ni rangi nyeupe na zimeandikwa kwenye kibao cheusi, sio za kawaida,” ameeleza.
Alichoshuhudia mwandishi
Eneo kilipo kituo hicho ni mita 20 kutoka Jengo la Kibo Compex lenye Kamera za CCTV.
Kwa namna ilivyo, isingekuwa rahisi kwa Kamera za Kibo Compex kuona kinachofanyika katika kituo hicho.
Mbali na mazingira hayo, woga na hofu zimekita mizizi katika mioyo ya mashuhuda wa tukio hilo, wengi walioulizwa walidai hawafahamu kilichotokea.
Wachache waliosimulia, waliomba hifadhi ya majina yao kwa kile walichodai wana familia zinazowategemea na mazingira yaliyomtokea Kibao yasije kuwatokea wao pia.
“Kama mtu amekuja kumchukua mtu hapa mbele yetu na baadaye akamuua, anashindwa vipi kunifuata mimi hohehahe akanimaliza,” ameeleza shuhuda mmoja.
Mwingine amesema ameshafuatwa na watu zaidi ya watatu kuulizwa kuhusu alichoshuhudia wakati wa tukio hilo, lakini hakutoa ushirikiano kwa hofu ya kuhusishwa katika kesi hiyo.
|
Saa chache baada ya kuripotiwa kwa mauaji ya Mjumbe wa Sekretarieti ya Chadema Ally Kibao, Jeshi la
|
Saa chache baada ya kuripotiwa kwa mauaji ya Mjumbe wa Sekretarieti ya Chadema Ally Kibao, Jeshi la Polisi limesema limeanza uchunguzi mkali kubaini wahusika wa mauaji hayo ili wachukuliwe hatua za kisheria.
Taarifa za kuuawa kwa Kibao zilisambaa leo, Septemba 8, 2024 katika mitandao ya kijamii, baada ya mwili wake kukutwa Ununio jijini Dar es Salaam, ikiwa ni siku mbili baada ya kukamatwa.
Kibao alikamatwa na watu waliodhaniwa ni askari wakiwa na silaha za moto, Septemba 6, mwaka huu akiwa ndani ya basi la Kampuni ya TASHRIF lenye namba za usajili T 343 EES, alipokuwa safarini kwenda nyumbani kwao, mkoani Tanga.
Hata hivyo, tayari mwili wake ulishafanyiwa uchunguzi katika Hospitali ya Mwananyamala na kubainika aliuawa baada ya kipigo kikali kisha kumwagiwa tindikali usoni.
Taarifa kuhusu uchunguzi wa polisi, imetolewa na Msemaji wa jeshi hilo, David Misime baada ya kuulizwa na Mwananchi Digital kuhusu kinachoendelea kutokana na tukio hilo.
Katika majibu yake, Misime amesema sambamba na uchunguzi huo, timu kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (Ramadhan Kingai) imetumwa kuongeza nguvu ili kuhakikisha waliofanya mauaji hayo wanapatikana na kifikishwa mahakamani.
“Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi mkali na timu kutokà Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai imetumwa kuongeza nguvu ili kuhakikisha waliofanya mauaji hayo wanapatikana na kifikishwa mahakamani,” alisema.
|
‘Ni utata mtupu’ ndiyo maneno yanayoakisi tukio la kuuawa kwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Chadema, All
|
‘Ni utata mtupu’ ndiyo maneno yanayoakisi tukio la kuuawa kwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Chadema, Ally Kibao lililotokea siku moja baada ya kukamatwa akiwa katika usafiri wa umma kwenda nyumbani kwao mkoni Tanga.
Kinachojenga msingi wa utata ni mazingira ya kukamatwa kwake kulikofanyika Tegeta, mbele ya Jengo la Kibo Complex, jijini Dar es Salaam na watu waliokuwa na gari mbili zilizozuia safari ya usafiri huo wa umma aliokuwa amepanda Kibao.
Hatua hiyo ilisababisha usafiri huo ambao ni basi la kampuni ya TASHRIF lenye namba T 343 EES kusimama na watu waliobeba silaha za moto waliingia ndani hadi alikokaa Kibao na kumfunga pingu kisha kuondoka naye.
Baada ya kuripotiwa kwa tukio hilo, utata zaidi uliibuka siku moja baadaye, ziliposambaa taarifa katika mitandao ya kijamii, zikieleza kada huyo amekutwa Ununio jijini Dar es Salaam, akiwa tayari ameshafariki na usoni alijeruhiwa kiasi cha kutoonekana vema.
Mwili wake ulipelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala jijini hapa, kwa taratibu za uchunguzi, uliobaini kifo chake kilisababishwa na kipigo kikali, kadhalika alimwagiwa tindikali usoni, kama ilivyoelezwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alipotoa taarifa za uchunguzi wa hospitali hiyo.
Bado mazingira tata yanaendelea kugubika mauaji hayo, kwa kile kinachohojiwa na wadau, ni nani anayeweza kumkamata mtu akiwa na mtutu wa bunduki na pingu, silaha ambazo aghalabu hutumiwa na Jeshi la Polisi, hivyo wapo wanaohusisha tukio la Kibao na askari wa jeshi hilo.
Maswali zaidi yanaibuka hasa kutokana na ukweli kwamba, yaliyomtokea Kibao yanaongeza idadi kati ya raia wengine zaidi ya 80 waliotekwa, kutoweka na baadhi yao kuuawa na wasiojulikana, kama ilivyoripotiwa Agosti mwaka huu na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).
Wito wa uchunguzi ili kuwabaini wahusika na kuundwa tume ya kijaji itakayochunguza matukio yote kwa ujumla, ndiyo sauti inayoonekana kuwa moja kutoka kwa wadau wa haki za binadamu, wanasiasa na wanaharakati nchini.
Hata hivyo, wadau wanatoa wito huo wakati tayari Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), ilishaanza uchunguzi wa matukio ya namna hiyo yanayohusisha zaidi ya watu 80.
Kutokana na tukio hilo la Kibao, kuhusishwa na askari wa jeshi la Polisi, Mwananchi ilimtafuta Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro alitaka atumiwe ujumbe na alipotumiwa hakujibu.
Jibu kama hilo lilitolewa pia na Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime ambaye pia alipotumiwa ujumbe hakujibu.
Hata simu ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni nayo iliita bila majibu na alipotumiwa ujumbe mfupi hakuujibu.
Heka heka za uchunguzi ‘Postmortem’
Awali, uliibuka mzozo katika hospitali ya rufaa ya Mwananyamala ulikopelekwa mwili huo, baada ya uchunguzi wa kitaalamu kubaini sababu ya kifo cha kada huyo kuonekana kuchelewa.
Ndugu wa marehemu, wafuasi na makada wa Chadema waliofurika katika hospitali hiyo, walitaka mchakato wa haraka kujua kiini cha kifo cha Kibao na shinikizo lao ilikuwa uchunguzi huo ufanywe mbele ya Wakili wa chama hicho, Hekima Mwisapu.
Ilionekana hali ya kutoelewana kati ya walinzi wa chumba cha kuhifadhia maiti ulikokuwa unafanyikia uchunguzi huo na makada na wafuasi wa Chadema, kwa kuwa wakili huyo alizuiwa kuingia chumbani humo.
Hoja ya walinzi hao kuhusu sababu ya kumzuia Mwisapu ilijengwa na kile walichoeleza, itifaki zinaruhusu ndugu pekee kushuhudia uchunguzi huo na si mwingine yeyote.
Lakini wafuasi wa Chadema, walishinikiza Mwisapu awepo ndani, kwa kile walichodai, itawezesha kusikia uhalisia wa sababu za mauaji hao na baadaye aliruhusiwa kuingia.
Subira ilionekana kuwashinda wafuasi wengi wa Chadema waliokuwepo nje ya hospitali hiyo, kwa kuwa ilichukua muda mrefu kabla ya majibu ya uchunguzi huo kutolewa.
Kutoka saa 12:07 uchunguzi ulipoanza hadi 2:50, ndipo Mbowe na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika walipoitwa ndani kusikia majibu ya uchunguzi huo.
Akitoa taarifa ya awali ya uchunguzi huo mbele ya vyombo vya habari, Mbowe amesema sambamba na kipigo kikali, uso wa Kibao ulimwagiwa tindikali.
“Ni dhahiri ameuawa baada ya kupigwa sana na hata kumwagiwa tindikali katika uso wake," amesema.
Mbowe amesema wameshauriana na familia ya marehemu na kukubaliana kuwa, washeria wa Chadema washiriki katika kikao cha uchunguzi, kujua Kibao ameuawa kwa namna gani.
Amesema mwili unaandaliwa ili taratibu nyingine za kifamilia zifanyike, huku mashauriano yakiendelea kuona hatua za kisheria zinazoweza kuchukuliwa.
Ameeleza hawataruhusu hali hiyo iendelee, huku akivituhumu vyombo vya dola kama mtuhumiwa namba moja kutokana na mazingira ya tukio.
Kwa kuwa imeshindikana suala la utekaji kuzungumzwa bungeni, amependekeza Rais Samia Suluhu Hassan aunde tume ya kijaji ya kimahakama kuchunguza matukio yote.
"Polisi hawana weledi wa kuchunguza jambo hili hata kidogo kwa sababu wao wenyewe ni sehemu ya watuhumiwa," amesema.
Ndugu wa marehemu
Mdogo wa marehemu huyo, Sharif Ally amesema wameshtushwa na taarifa za kifo cha ndugu yao na kwamba tayari mwili huo umepelekwa nyumbani Morocco jijini Dar es Salaam kwa ajili ya taratibu za kuusafirisha kwenda Tanga kwa ajili ya maziko.
Maziko amesema yatafanyika kesho, saa 7 mchana maeneo ya Sahale nyumbani kwa marehemu, njia ya kuelekea Pangani.
Wadau walaani
Tukio hilo, lilikiibua Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kilichoisihi Serikali ifnye uchunguzi wa kina na haraka kubaini wahusika na wachukuliwe hatua.
Kituo hicho kimesisitiza uchunguzi huo unapaswa kuwa wa wazi ili kuondoa sintofahamu na kurudisha imani ya wananchi kwa vyombo vya ulinzi na usalama.
Kadhalika, kimezitaka mamlaka husika zielekeze juhudi kudhibiti matukio ya namna hiyo ili kupunguza taharuki kwa jamii.
“Jeshi la Polisi lithamini na lidhibiti mianya ya uhalifu ndani ya vyombo vya dola, kuhakikisha watu wasiokuwa dhamana hawapati nafasi ya kujipenyeza na kufanya uhalifu wakijifanya sehemu ya vyombo vya ulinzi,” kimeeleza katika taarifa yake kwa umma.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyosainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wake, Anna Henga imemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi (Hamad Masauni), ajitathmini na kuwajibika kwa madhila yanayowakumba wananchi.
Kituo hicho, kilitoa wito kwa Rais Samia Suluhu Hassan atoe tamko la kukemea matukio hayo ya utekaji na mauaji yanayoendelea nchini.
Chama cha ACT-Wazalendo nacho, kimelaani tukio hilo, kikisema kunaongeza hofu juu ya usalama na amani na kuchafua imani iliyopo kwa wananchi.
“Maswali tunayojiuliza hivi ni nani anayeweza kufanya matukio haya siku zote hizo bila kukamatwa? Je, vyombo vyetu vinazidiwa uwezo na watekaji? Majibu ya wananchi ni kuwa vyombo vyetu ndiyo vinahusika ndio maana haviwezi kujiwajibisha vyenyewe.
“Tunajiuliza utekaji unafanyika kwa maslahi ya nani? Na kwa lengo lipi?” kilihoji.
Sambamba na hoja zake hizo, kilimtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi, Camiliu Wambura awaeleze wananchi wanaohusika na vitendo hivyo, huku bunge likitakiwa kuunda kamati maalumu kuchunguza mauaji yote ya raia yanayohusisha vyombo hivyo.
CCM yataka uchunguzi
Katika hatua nyingine, Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla amelitaka jeshi la polisi kutimiza wajibu wake katika uchunguzi wa tukio hilo.
"Nimekuwa nikifuatilia toka asubuhi, sisi ni vyama vya siasa linapokuja suala la ubinadamu, siasa unaweka pembeni. Niliombe jeshi la polisi likatimize wajibu wake wa kuendelea na uchunguzi ili tupate taarifa baada ya uchunguzi,” amesema Makalla.
|
Wimbi la vitendo vya mauaji katika siku za hivi karibuni, limehusishwa na kukithiri kwa matatizo ya
|
Wimbi la vitendo vya mauaji katika siku za hivi karibuni, limehusishwa na kukithiri kwa matatizo ya afya ya akili, kumomonyoka kwa maadili, uelewa duni wa namna ya kuishi, huku umasikini uliopitiliza nao ukitajwa kama moja ya sababu.
Kwa mtazamo wa kisaikolojia, wanazuoni wanasema vitendo hivyo ni dalili ya jamii kupunguza uwezo wa kufikiri vema na kufanya maamuzi sahihi, kunakosababishwa na shida katika afya ya akili.
Lakini, viongozi wa dini wamekwenda mbali zaidi na kuhusisha vitendo hivyo na dalili za mwisho wa ulimwengu kama ilivyotabiriwa katika vitabu vitakatifu, huku mmomonyoko wa maadili ikiwa ni sababu nyingine iliyotajwa nao.
Msingi wa hoja za wanazuoni na viongozi hao wa dini ni mwenendo wa matukio ya mauaji ya watu, yaliyotokea katika miezi miwili kuanzia Julai hadi Agosti mwaka huu.
Matukio ya mauaji
Miongoni mwa matukio hayo ni lile la Julai 8, mwaka huu, uhai wa mwanafunzi wa kidao cha pili katika Shule ya Sekondari Kalunde mkoani Tabora, Salma Mussa (15) ulipokatishwa alipokuwa akielekea shuleni.
Siku hiyo hiyo katika Mkoa wa Dodoma, Stephen Mabula (44), aliingia mikononi mwa polisi baada ya kumnyonga mwanawe wa kambo hadi kufa, baada ya ugomvi uliohusisha wivu na mapenzi na mwenza wake.
Kama hiyo haitoshi, Mkazi wa Mgongola ‘A’ mkoani Tanga, alipoteza maisha baada ya kukatwa kichwa na watu wasiojulikana akiwa anachuma mboga shambani, Julai 27, mwaka huu.
Tukio hilo lilifuatiwa na lililotokea usiku wa kuamkia Julai 31, mwaka huu, wivu wa mapenzi ulikatisha uhai wa Mary Mushi, mkazi wa Moshi, mkoani Kilimanjaro, aliyeuawa kwa kukatwa mapanga. Baada ya kuuawa, mwili wake ulitupwa shambani kwao.
Agosti 9, mwaka huu katika Mkoa wa Dodoma, maisha ya Angela Joseph yalikatishwa baada ya kuuawa na mpenzi wake kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa mapenzi.
Angela aliuawa kikatili na mwili wake kufungwa kwenye mfuko wa nailoni kisha kuingizwa kwenye kiroba na baadaye kutupwa porini.
Kesho yake, Agosti 10, mwaka huu, Mganga wa Kienyeji, Nkamba Kasubi alikamatwa na Jeshi l Polisi kwa kuua na kuwafukia watu 10 katika Mikoa ya Dodoma na Singida. Baadhi yao walizikwa wakiwa hai.
Katika Mkoa wa Tabora, Agosti 14, mwaka huu, Juliana Mbogo (40) alinyongwa hadi kufa na mwenza wake na mwili wake kufichwa uvunguni mwa kitanda. Wivu wa mapenzi ulitajwa kama moja ya sababu.
Mwili wa mfanyabishara ndogondogo maarufu Machinga, John Gerald (30) umekutwa umetupwa baada ya kuuawa kwa kuchomwa visu kadhaa tumboni mkoani Dodoma Agosti mwaka huu.
Agosti 28, mwaka huu mkoani Dodoma, Michael Richard alipoteza uhai baada ya kuuawa kisha nyumba yake kuchomwa moto, hali iliyowajeruhi mkewe na mwanawe. Sababu inadaiwa ni kisasi.
Maadili ni tatizo
Akizungumza na Mwananchi jana, Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kulitheri Tanzania (KKKT), Askofu Alex Malasusa alihusisha mwenendo huo na kukithiri kwa mmomonyoko wa maadili uliosababishwa na binadamu kuacha kumwamini Mungu.
Hali hiyo kwa mtazamo wa Askofu Malasusa, imesababisha binadamu kuamini katika ushirikina, jambo linalowafanya wengi kujikuta katika matendo ya mauaji.
Alieleza matukio hayo si hatari kwa binadamu pekee, bali ni chukuzi kwa Mungu na maombi ya kuzitakasa roho ziondokane na fikra za mauaji ndiyo silaha njema itakayokabili changamoto zilizopo.
“Kwanza matukio haya ni chukizo mbele za Mungu. Watu wote tunahimizwa kuomba ili roho ya mauaji itoweke ili watu wasiishi kwa hofu,” alisema.
Umuhimu wa elimu hasa za kidini ndilo jambo alilopendekeza, ili kuwafanya binadamu watambue baadhi ya matendo hayampendezi Mungu.
“Tutambue kuwa ushirikina ni chukizo kwa Mungu. Ushirikina ni kazi ya shetani. Watu wamrudie Mungu na kuachana na imani potofu,” alisisitiza.
Sauti ya pamoja kukemea vitendo hivyo, alisema ndiyo njia muhimu inayopaswa kutumika kupunguza au kumaliza kabisa mwenendo huo.
“Upendo wa Mungu ukitawala hatutakuwa na roho ya mauaji,” alisema Askofu Malasusa.
Dalili za mwisho wa ulimwengu
Kwa mtazamo wa kiroho matendo hayo ni dalili za mwisho wa ulimwengu, kama inavyofafanuliwa na Mkuu wa Habari na Mawasiliano wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Mchungaji John Kamoyo.
“Labda siyo rahisi kupata jibu la moja kwa moja. Nikiwa mchungaji na mtumishi wa mambo ya kiroho mimi nitakupeleka katika mambo ya kiroho zaidi, hii ni dalili ya mwisho wa maisha,” alisema.
Aliujenga mtazamo wake huo kwa kurejea kitabu cha Biblia Timotheo 3:1-5, akisema kuna aya zinazoakisi namna binadamu tunavyoishi siku za mwisho ambazo huwa ni za hatari.
“Ukisoma aya hiyo utaona inaeleza watu wenye kujipenda wenyewe na wasiowapenda wa kwao,” alieleza.
Kujenga hofu ya Mungu mioyoni mwa watu, Mchungaji huyo aliitaja kama suluhu pekee ya matendo hayo, huku akisisitiza umuhimu wa kuwafundisha watu kuziepuka jamii zenye tabia mbaya.
“Tuwafundishe watu kuwa na hofu ya Mungu, japokuwa unabii huu utaendelea sana mpaja Yesu atakaporudi. Kuwafundisha watu wajiepushe na watu wa namna hiyo wakimwamini Yesu kweli kweli,” alieleza.
Uelewa duni na umasikini
Mwanazuoni wa masuala ya ustawi wa jamii, Dk Zena Mabeyo alisema uelewa duni wa namna sahihi ya kuishi na kutimiza malengo ndiyo sababu kuu ya vitendo hivyo.
Katika ufafanuzi wake, alisema baadhi ya watu wanakwenda kwa waganga na kushauriwa wauwe ili kupata utajiri, wanajikuta wakitekeleza kwa sababu hawana uelewa wa njia sahihi za kutajirika.
Hata wale wanaouwa kwa sababu ya wivu wa mapenzi, alisema ni kwa sababu hawana uelewa wa mbinu za kukabili hisia zao au kudhibiti matendo yatakayowasababishia wivu huo.
“Kwetu (Tanzania) kuna shida ya elimu na uelewa sahihi wa nini binadamu anatakiwa afanye ili kufikia malengo yake,” alisema.
Umasikini uliopitiliza nao ni sababu nyingine iliyotajwa na Dk Zena kama chanzo cha watu kujihusisha na vitendo vinavyokatisha maisha ya wengine.
“Umasikini wa mali unasababisha umasikini wa fikra hatimaye kila unachoshauriwa unajikuta unafanya, ndiyo hawa tunaowaona wameua kisa watajirike na vinginevyo,” alisisitiza.
Lakini yote hayo, Dk Zena alisema msingi wake ni uelewa duni wa namna ya kuishi, akifafanua iwapo watu wangeelewa kwamba kiungo cha mtu hakiwezi kukusababishia mafanikio wasingevitafuta.
Mwanazuoni huyo ambaye pia ni Mhadhiri katika Taasisi ya Ustawi wa Jamii, alisema kunahitajika nguvu ya pamoja kukabili vitendo hivyo, isiachiwe Serikali pekee.
“Tunapaswa kujengeana uwezo wa kiuchumi kwa sababu wengine wanaingia huko kwa sababu za kukosa njia ya kujiinua kiuchumi,” alisema.
Lakini kuchukuliwa kwa hatua kali dhidi ya watakaobainika kufanya vitendo hivyo ni suluhu nyingine kwa kuwa inajenga woga kwa wenye matarajio ya kufanya hivyo.
Dk Zena, alisema ni vema kuwa na mbinu za kudhibiti mapema, wale wote wanaoibuka kutaka usajili wa kutoa huduma mbalimbali mathalan za tiba asili au za kiroho.
“Tunapaswa kudhibiti watu kuanzisha asasi mbalimbali za kiroho na kidini, wanaotaka usajili wachunguzwe wanakotoka na mwenendo wa maisha yao,” alisema.
Afya ya akili
Akizungumzia mwenendo huo, Rais wa Chama cha Wanasaikolojia Tanzania, Dk Magolanga Shagembe alisema ni dalili ya kukithiri kwa matatizo ya afya ya akili miongoni mwa wananchi wengi.
Tatizo la afya ya akili kwa mujibu wa Dk Shagembe, linaathiri uwezo wa binadamu kufanya maamuzi sahihi na hisia zake kwa ujumla, hivyo mara nyingi anajikuta akiangukia kuamua vibaya.
Katika ufafanuzi wake huo, alieleza hata anayefanya mauaji kwa sababu za kishirikina, aghalabu hujikuta katika kitendo hicho baada ya kujiuliza maswali mengi na uwezo wake wa kufanya maamuzi umepungua kiasi cha kumshinikiza aue.
“Mtu mwenye akili timamu lazima atajiuliza kuna faida gani ya kupata ninachokitaka kwa mganga kama nitapoteza uhai wa mtu wangu wa karibu, kwanini nifanye hivi kutimiza mahitaji yangu.
“Akijiuliza hayo kama akili yake ipo sawa kabla hajafikia kutoa uhai wa mtu mwingine anakuwa ameshapata majibu yanayomuondoa kwenye nia ya kufanya mauaji,” alisema.
Dk Shagembe alisema kwa mtu mwenye matatizo ya akili anapojiuliza maswali kama hayo, mara nyingi hapati majibu chanya na ndipo anajikuta akifanya mauaji kama alivyoelezwa na mganga.
Mazingira hayo hayo, alisema ndiyo yanayowakabili wale wanaokatisha uhai wao, akifafanua hufanya hivyo baada ya kujiuliza maswali mengi na kushindwa kupata majibu sahihi.
Lakini, mwenendo huo, Dk Shagembe alisema unaashiria uwepo wa ombwe la upatikanaji wa huduma za afya ya akili na msaada wa kisaikolojia katika jamii.
“Tunahitaji kufikiria namna ya kuzitoa huduma hizi nje ya hospitali na katika ustawi wa jamii ili kuruhusu hata watoa huduma binafsi waanzishe vituo vyao kwenye vijiji na mitaa ili mtu akipata changamoto ajue eneo la kukimbilia kabla hajafanya maamuzi hatari,” alieleza.
Malezi ni sababu nyingine iliyotajwa na Dk Shagembe, akifafanua baadhi ya watu wamelelewa kushindwa kukabiliana na changamoto za maisha na hivyo inakuwa rahisi kuamua vibaya pale anapokabiliwa nazo.
Ili kukabiliana na hayo, alisema ni muhimu kutoa elimu kwa jamii iwe na utambuzi wa masuala ya kisaikolojia na kuwawezesha wananchi kutatua changamoto zinazowakabili.
Alieleza elimu hiyo ni vema ijikite kuwajuza wananchi kuwa haiwezekani kunufaika au kutatua changamoto zako kwa kukatisha uhai wa mwingine.
Alipendekeza uwekezaji ufanyike kwenye utafiti wa kubaini sababu za kina za matendo hayo na mbinu za kitaalamu za kuyakabili.
Kadhalika, alitaka Serikali ije na sheria inayowatambua, kuwasajili na kuwasimamia watoa huduma za afya ya akili, saikolojia ili kuhakikisha huduma zinatolewa kwa kuzingatia maadili.
“Kumekuwa na wimbi la watu wanaozitoa hizi huduma badala ya kusaidia watu, wanawaumiza zaidi hali inayosababisha wanakata tamaa na kujikuta wakifanya maamuzi yasiyofaa,” alisema.
Alieleza kuna umuhimu wa shuleni kutolewa elimu ya stadi za maisha zitakazomwezesha mtu kukabili changamoto na ajue wapi anakopaswa kukimbilia pindi atakapotatizwa.
|
End of preview. Expand
in Data Studio
README.md exists but content is empty.
- Downloads last month
- 2